MPOX nchini Kenya


Wakati Wizara ya Afya ya Kenya ilipothibitisha visa vya kwanza vya maradhi ya mpox ,iliyokuwa ikijulikana kama monkeypox mwezi Julai 2024, watu wengi hapa nchini walishanga kwa sababu ,hawakuwa na Habari kuhusu ugonjwa huo  ambao ,unasemekana kuenea katika Afrika ya Kati. Kwa vyovyote vile, ugonjwa wa Mpox.

Wakenya wafikiri huu mi ugonjwa wan Ndui au smallpox ambao uliangamizwa ulimwenguni pote mwaka wa 1980.Isitoshe,  kumekuwa na hofu huku wengi wakishagaa  kwa nini tunasikia kuhusu virusi vya ndui tena?

Ukweli ni kwamba mpox imekuwapo kwa miongo mingi, lakini hadi hivi majuzi ilionekana hasa katika Afrika ya Kati na ya Magharibi. Kwa sas visa vya ugonjwa huo vimeripotiwa katika nchi kadhaa za Afrika Mashariki hususani Kenya.

Mpox huenea vipi?

Mpox husababishwa na virusi vya familia  ya ndui au smallpox. Inasambazwa kupitia mahusiano ya karibu  yaani ngozi kwa ngozi, umajimaji wa mwili, nyuso zilizochafuliwa, na wakati mwingine kutoka kwa wanyama hadi kwa wanadamu.


Zaidi ya hayo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imekuwa kitovu cha maambukizi haya  kwa miaka mingi. Kati ya  mwaka 2023-2024, nchi hiyo iliripoti zaidi ya visa 14,000 vya wagonjwa na vifo zaidi ya 650. Variant au virusi yenye nguvu zaidi, iitwayo clade Ib, imefanya mambo yawe mabaya zaidi, ikisambaa kwa kasi mno na kushambulia kwa nguvu zaidi. Bali na DR Congo, ugonjwa huo umeenea hadi nchi jirani kama vile Burundi na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Matukio ya kwanza Kenya

Mnamo Julai 2024, Kenya ilithibitisha visa viwili vya kwanza vya mpox katika Kaunti ya Taita Taveta. Mgonjwa mmoja alitoka   Kaunti ya Kiambu, wakati mwingine alikuwa raia wa Kongo. Kwa kusikitisha, majuma machache baadaye, inadaiwa kuwa Kenya ilirekodi kifo chake cha kwanza kinachohusiana na mpox, mtu anayeishi na virusi vya UKIMWI ambaye alipata matatizo makubwa.

Kufikia mapema mwaka 2025, Kenya ilikuwa imethibitisha visa 33 katika kaunti 12, na maafisa wa afya walikuwa wamefuatilia zaidi ya watu 200 waliowasiliana na virusi hivyo. Wengi wa maambukizi walikuwa wanaohusishwa na madeleva wa lori ambao husafiriki kutoka nchi za Afrika mashariki hadi Nchi ya DR Congo na pia  vituo vya mijini ambapo watu hujumuika kwa wingi.

Kulingana  na Wizara ya Afya ,Kenya ,Kaunti ya Mombasa ina idadi kubwa zaidi ya maambukizi kwa 146, ikifuatiwa na Busia na maambukizi 63, Nakuru (21), Kilifi (19), Nairobi (17), na Makueni (13). Taita-Taveta na Uasin Gishu wamerekodi visa vitano kila mmoja, wakati Bungoma ina visa vinne. Kajiado, Kakamega, na Kiambu kila moja imeorodhesha maambukizi matatu.

Hadi sasa, kulingana na takwimu, watu nchini Kenya ni wachache  sana ambao wamepatikana na ugonjwa huo ikilinganishwa na DRC. Lakini wataalamu wanaonya kuhusu changamoto kadhaa kama vile

Uchunguzi mdogo: Uchunguzi wa mpox chini ya 500 ulifanywa katika miezi saba ya kwanza, ikimaanisha kuwa visa vingine havijatambuliwa.

Ufahamu mdogo: Watu wengi bado wanachanganya mpox na ndui au smallpox wanafikiri kwamba huathiri vikundi fulani tu. Hilo hupunguza namna au hali ya kutafuta matibabu ya kiafya na pia  kutoa ripoti kuhusu maambukizi.

Unyanyapa: Kama ilivyokuwa wakati virusi vya UKIMWI vilipoanza, familia fulani huficha watu wa ukoo walio wagonjwa kwa kuogopa kuhukumiwa na jamii , jambo ambalo linaweza kufanya ugonjwa huo kueneea zaidi.

Mbinu za kukabiliana na Mpox

Ni muhimu kwa nchi kuchukua hatua mwafaka ili kuudhimiti ugonjwa huo.Kenya imeongeza ukaguzi wa mipaka, imeweka tahathali za kusafiri, na kampeni za uhamasishaji wa umma. Jambo la  muhimu ni kwamba, Kenya imefanya   mipango ya  kutoa chanjo kwa mikoa, na pia Shirika la Afya Duniani(WHO) na washirika wake wamejiandaa kutoa dozi 50,000 za chanjo ya mpox kwa matumizi nchini Kenya na nchi nyingine za Afrika.

Maafisa wa afya wanasema chanjo hiyo itapelekwa kwanza kwa wafanyikazi wanaofanya na mashirika ya afya au wahudumu wa afya, watu wenye kinga dhaifu, na makundi wenye kuwa  hatarini kama vile madereva wa malori ambao husafiri kwa kuvuka mipaka.

Ingawa Mpox sio mpya, lakini kuenea kwake nchini Kenya ni ukumbusho kwamba magonjwa ya kuambukiza hayana mipaka. Habari njema ni kwamba Kenya inaweza kujifunza kutokana na mapambano ya ulimwenguni kote dhidi ya ndui au smallpox: kwa kutumia mbinu kama  chanjo, elimu, na ufuatiliaji, hali inaweza kubadilika.

Kwa sasa, umuhimu  ni kuwa na ufahamu. Kujua dalili kama vile  - homa, maumivu ya mwili, kuvimba kwa lymph nodes, na upele unaogeuka kuwa vidonda vilivyojaa maji - kunaweza kuwasaidia watu kutafuta matibabu mapema na kuepuka kueneza virusi.

Mlipuko wa mpox nchini Kenya bado ni mdogo, lakini ni sehemu ya hadithi kubwa zaidi ya kikanda. Kwa kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inakabiliwa na maelfu ya visa, na nchi jirani zinaripoti milipuko yao ya kwanza, inadhibitisha kuna hatari ambayo sharti ikabiliwe mapema.

Kama vile ugonjwa wa ndui ulivyoshambuliwa kwa jitihada za pamoja, mpox pia inaweza kudhibitiwa ikiwa tunawekeza katika afya ya umma, ushirikiano wa mipaka, na ufahamu wa jamii.

 

 

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Global Health Leaders Rally in Bogotá to Tackle Reproductive Health Gaps

Unsafe Abortion