Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2012

Mzee Nelson Mandela apata matibabu

Picha
Aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini mzee Nelson Mandela aendelea kupata nafuu baada ya kutoka hospitalini , alikolazwa kutokana na maumivu ya tumbo ambaye yamekuwa yakimtatiza kwa muda mrefu. Hapo awali, taarifa kutoka ofisi ya Rais Jacob Zuma ilisema Mzee Nelson Mandela alilazwa hospitalini na akawaomba   Waafrika Kusini kumuombea nafuu ya haraka. Mzee Mandela, mwenye umri wa miaka 93 hajaonekana hadharani kwa muda mrefu sasa kufuatia kudorora kwa afya yake . Wananchi wengi nchini Afrika Kusini walipokea habari za kulazwa kwake hospitalini kwa hofu na huzuni tele, lakini wakasema wanaendelea kumuombea apate afueni ya haraka. Mbali na hayo,mzee Mandela aligunduliwa   kuugua saratani ya tezi dume,2001 na baada ya matibabu akapona, kwani iligunduliwa mapema. Alikuwa Rais wa kwanza mweusi katika nchi hiyo kuanzia mwaka 1994 na kisha akaachia ngazi mwaka 1999. Mandela anatambulika kote duniani kwa juhudi zake za kupambana na utawala wa kibaguzi wa Makaburu kwa muda mrefu na...

Njenga Karume aaga dunia

Picha
Marehemu Njenga Karume  Aliyekuwa waziri wa ulinzi na mbunge wa zamani wa Kiambaa, Njenga karume amefariki dunia. Karume ameaga dunia katika hospitali ya Karen hapa Nairobi ,alipokuwa akipokea matibabu, baada ya kuugua saratani. Marehemu Karume amefariki akiwa na umri wa miaka 83. Rais Mwai Kibaki ametoa salamu zake za rambi rambi kwa jamaa na marafiki wa Marehemu huku akisema amempoteza rafiki wa dhati. Karume alikuwa kigogo wa siasa na alimuunga mkono rais Mwai Kibaki katika juhudi zake za kuimarisha siasa za chama cha Democratic party(DP). Karume alikuwa mwanabiashara mashuhuri ambaye alikuwa na bidii kama za mchwa.Alijizatiti kuwa mmojawa   matajiri watajika hapa nchini,licha ya kuanzia chini sana. Katika kitabu chake, alichoandika kuhusu maisha yake, Karume alisema vile alijitahidi kutoka uchomaji wa makaa hadi dhahabu. Anatajwa pia kama aliyepigania uhuru, aliyehakikisha tamaduni zinahifadhiwa. Alikuwa mbunge wa kiamba lakini 2007 alipoteza kiti ...
Hii ni aina ya saratani inayokumba tezi ya thyroid. Ikumbukwe kuwa tezi ya thyroid ipo sehemu ya mbele ya shingo ya mwanadamu ikiwa na sehemu mbili (lobes) moja kila upande wa shingo. Visababishi na ukubwa tatizo Saratani ya thyroid huwapata watu wa umri mbalimbali, kuanzia watoto mpaka watu wazima. Watu waliowahi kupigwa mionzi sehemu ya mbele ya shingo wapo katika hatari kubwa ya kupata aina hii ya saratani. Kadhalika watu wazima ambao waliwahi kupigwa mionzi kipindi cha utotoni nao pia wana hatari kubwa zaidi ya kupata saratani ya thyroid hata kama hawakuwahi kupata tatizo hilo wakati wanakua. Tiba ya mionzi maeneo ya shingoni ilikuwa ikitumika sana zamani kwenye miaka ya 50 mpaka 60 kwa ajili ya matibabu ya uvimbe wa tezi ya thymus, mafindofindo (tonsils), au baadhi ya magonjwa ya ngozi. Hata hivyo ni nadra sana kwa tiba hii kutumika katika zama hizi. Vihatarishi vingine vya saratani ya tezi ya thyroid ni pamoja na kuwepo kwa historia ya tatizo hili miongoni mwa wanafamilia na kuw...

Marehemu Michuki aombolezwa

Picha
 Marehemu John Michuki  Wakenya wa tambaka mbalimbali waendelea kuomboleza kifo cha aliyekuwa waziri wa mazingira John Njoroge Michuki aliyefariki dunia jumanne,kwa mstuka wa moyo,  katika hospitali ya Chuo Kikuu cha Aga Khan. Akizaliwa 1932 katika kitongoji cha Jimbo la Kagema katika wilaya ya Muranga. Alipata masomo yake ya upili katika shule ya Mangu pamoja na rafikiye wa dhati  rais Mwai Kibaki. Aliendelea na masomo yake katika chuo cha Worcester,Oxford huko Uingereza. Wengi wamemtaja michuki kama kiongozi  mchapa  kazi , aliyedumisha nidhamu ya hali ya juu kazini na aliyejitolea kwa kila alilofanya. Rais Mwai Kibaki ambaye ni rafikiye marehemu alisema kuwa Michuki alikuwa mwanasiasa hodari,aliyetekeleza kazi yake kwa uadilifu.Pia mwana biashara stadi. Kulingana na mhariri wa habari wa kujitengemea Onesmus Kilonzo Michuki atakubukwa kwa kulainisha sekta ya matatu,na uhifadhi wa mto Nairobi miongoni mwa mengine “kila ofisi aliohudumia ilipata ufa...

WHO yasema depo provera ni salama

Picha
Shirika la Afya Duniani ( WHO) limeondolea lawama shindano ya Depo Provera kuwa inachangia maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU). Shirika hili (WHO) linahakikishia  wanawake wanaotunia aina ya uzazi wa mpango wa homoni kuwa hakuna hatari ya kutumia aina hii, kama ilivyo daiwa hapo wali. Hata hivyo (WHO) imeonya  kuwa  ni aina moja pekee ya uzazi wa mpango inayozuia maambukizi ya Virusi  Vya Ukimwi - kondomu au mpira. Huku likisisitiza kuwa ni muhimu kwa wale wako kwenye hatari ya kuambukizwa Virusi Vya Ukimwi kuchukua tahadhali. Zaidi ya hayo, Shirika la Afya Duniani utafiti unafanywa kwa nia ya kuhakikisha malengo ya milenia ya afya imefikiwa. Uvumbuzi kuwa utumiaji dawa ya upangaji uzazi ya homoni ijulikanayo kama Devo Provera unachangia ongezeko la maabukuzi ya ugonjwa hatari wa ukimwi, miezi michache iliyopita, uliwaacha wanawake wengi na hofu na husuni tele. Inakadiriwa kuwa takribani millioni 12 ya wanawake wenye um...

Saratani ya tezi kibofu cha mkojo (Prostate)

  Saratani ya tezi kibofu ni ugonjwa ambao   huwa kati ya wanaume.kama aina nyingine za saratani, inapogunduliwa mapema inakuwa ni rahisi kutibiwa. Zaidi ya hayo, walio  hatarini ya kuambukizwa Ugonjwa huu ni   wanaume walio na umri wa miaka 55 na zaidi. Hivi majuzi, ugonjwa wa saratani umetia wengi kiwewe.Siku baada ya siku kuna habari kuwa mtu fulani ana ugonjwa wa saratani.Waume kwa wanawake,vijana   kwa watoto wote wako hatarini ya kuabukizwa ugonjwa huu. Watafiti bado hawajapata uvubuzi ni nini haswa inayo sababisha ugonjwa huu hatari. Hata hivyo inakisiwa kuwa  mazingira tunayoishi, kwa njia moja ua nyingine yanachangia kuwepo kwa maradhi haya. Hapa nchini Kenya waziri wa   afya ya umma Mheshimiwa Beth Mugo alitangaza kuwa amegunduliwa kuugua saratani ya matiti na kwa sasa anaendelea na matibabu huko Marekani. Waziri Mwenzake, Prof. Anyang Nyongo pia aligunduliwa kuugua saratani ya tezi kibofu.Kwa bahati nzuri, iligunduliwa mapema na baada y...