Jumamosi, 7 Desemba 2013
Ijumaa, 6 Desemba 2013
Mandela aaga dunia akiwa na umri wa miaka 95
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza Ijumaa usiku kwamba rais wa zamani mpinzani mkuu wa ubaguzi wa rangi Madiba Nelson Mandela amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu. Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ametangaza Ijumaa usiku kwamba rais wa zamani mpinzani mkuu wa ubaguzi wa rangi Madiba Nelson Mandela amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Akilihutubia taifa Rais Zuma alisema "Taifa letu limempoteza mwana wake mkuu shujaa. watu wetu wamempoteza baba yao"
Mandela alikuwa rais wa Kwanza muafrika kuchukua madaraka kutoka kwa utawala wa ubaguzi wa rangi kutoka kwa wazungu walowachache 1994. Kwa wengi alikua shujaa, mtu shupavu na mwenye mtizamo.
Mara kwa mara alikuwa mnyenyekevu, mchangamfu, muaminifu na mtu ambae aliwajali wananchi wote.
Wasifu wa Mandela
Mwaka 1962, Madiba jina lake maarufu huko Afrika Kusini alikamtwa na kushtakiwa kwa tuhuma za kufanya vitendo vya kutaka kuihujumu serikali. Hata hivyo alijitetea akisema hivyo vilikuwa vitendo vya kuwakomboa waafrika walowengi. Miaka miwili baadae alihukumiwa kifungo cha maisha katika kiswa cha Robben kwenye pwani ya mji wa magharibi wa Cape Town.
Mandela aliachiwa huru miaka 27 badae, ikiwa mwaka 1990 pale serikali ya wazungu wachache iliyokua inaongozwa na Rais Frederik De Klerk kuhalalisha vyama vyote vya kisiasa na kuwafungua wafungwa wote wa kisiasa.
Utawala wa mpito ulienddelea na majadiliano ya kutayarisha katiba na utawala wa kidemokrasia ulianza ukiongozwa na Mandela na De Klerk. Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vyote na watu wa kabila zote ulifanyika 1994 na Mandela kuchaguliwa akiwa na umri wa miaka 74.
Mandela na mkewe Winnie walikuwa pamoja baada ya kuachiliwa huru kutoka gereza la Robben Island, lakini hai8kuchukua muda wakaachana. Na katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake alipotimiza miaka 80 alimuoa Graca machel, mjane wa rais wa zamani wa Msumbiji Samora Machel.
Alibaki madarakani kwa mhula mmoja wa miaka mitano, na kuanza kampeni chungu nzima moja wapo ikiwa ni kutetea haki za watoto na kupambana na ugonjwa wa Ukimwi. Akiwa madarakani alikosolewa kwa kutokubali kuchukua hatua za nguvu kupambana na janga hilo.
Miaka miwili baada ya kuondoka madarakani mtoto wake wa kiume alifariki kutokana na ukimwi na hapo ndipo aliongeza juhudi zake za kupambana na ugonjwa huo.
Akiwa na umri wa miaka 85 hapo mwaka 1999 Mandela alitangaza kwamba anastahafu kabisa kutoka kazi za umaa lakini aliendelea kufanya kazi kutetea haki za watoto.
Mnamo maisha yake yote alipokea mamia ya tunzo lakini tunzo kuu ni ile ya amani ya Nobel ya 1993aliyopata pamoja na hasimu wake rafiki yake Bw De Klerk.
VOA
Alhamisi, 5 Desemba 2013
Masuala ya Jamii
Ripoti ya Ufaransa: Arafat hakufa kwa sumu
Uchunguzi uliofanywa na wanasayansi wa Ufaransa kuhusu kifo cha kiongozi
wa zamani wa Palestina, Yasser Arafat, umeonyesha kuwa kiongozi huyo
hakufa kutokana na sumu ya Polonium, bali alikufa kifo cha kawaida.
Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi wa wanasayansi hao, vipimo vimeonyesha
kuwa Arafat alikufa kutokana na uzee baada ya kupata maambukizi na sio
kutokana na sumu ya polonium, ingawa wamesema kulikuwa na ishara za
plotunium.
Matokeo hayo yanatofautiana na ripoti iliyotolewa awali na maabara moja ya Uswisi, iliyoeleza kuwa Arafat alikufa kutokana na kiwango kikubwa cha sumu ya polonium, baada ya kuigundua sumu hiyo kwenye nguo zake.
Ripoti hiyo ya Ufaransa imepingwa vikali na mke wa Arafat, Suha Arafat, ambaye amesema kifo cha mumewe kilikuwa ni mauaji ya kisiasa yaliyofanywa na mtu wake wa karibu. Akizungumza mjini Paris, Suha amesema ameshangazwa na taarifa zinazokinzana kutoka kwa waatalamu wa Ulaya.
Ripoti hiyo iliyokabidhiwa kwa Suha, haitachapishwa, lakini ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali imesema uchunguzi uliokamilika unaoonyesha kuwa Arafat hakuuawa kwa sumu ya polonium.
Arafat, aliyesaini makubaliano ya mjini Oslo ya mwaka 1993 na Israel, alifariki Novemba mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 75, katika hospitali moja nchini Ufaransa.
Kifo chake kilitokea wiki nne alipougua baada ya kula chakula na hivyo kusababisha kutapika na kuumwa tumbo. Taarifa za kitabibu zilionyesha kuwa alikufa kutokana na kutokwa damu katika ubongo, lakini hakukuwa na maelezo ya nini kilisababisha hali hiyo.
Palestina yapuuzia uchunguzi wa Ufaransa
Afisa mwandamizi wa Palestina, Wasel Abu Yousef, ameipuuza ripoti hiyo ya Ufaransa akisema kuwa iko kisiasa zaidi na iko kinyume na ushahidi unaothibitisha kuwa Arafat aliuawa kwa kupewa sumu.
Wapalestina wengi wanaamini kuwa Israel inahusika na kifo cha kiongozi wao, tuhuma ambazo Israel imezikanusha.
Mkuu wa kamati ya Palestina inayochunguza kifo cha Arafat, Tawfik Tirawi amesisitiza kuwa Israel inahusika na awali alisema atataja majina ya watu wanaoaminika kuhusika na kifo cha kiongozi huyo.
Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Israel, amesema kuwa ripoti ya matokeo ya Ufaransa si ya kushangaza na kuelezea matumaini yake kwamba sasa Arafat atapumzika kwa amani.
Mwaka uliopita, mjane wa Arafat aliitaka serikali ya Ufaransa ifanye uchunguzi wa kifo cha mumewe, baada ya kituo cha televisheni cha Al Jazeera kuripoti kwamba nguo za Arafat zilikutwa na sumu ya polonium.
Waendesha mashitaka wa Ufaransa walianzisha uchunguzi na hatimaye wataalamu wa kupekuwa ushahidi kutoka Uswisi, Urusi na Ufaransa, walichukua sampuli za mabaki ya mwili wa Arafat, baada ya kufukuliwa mwaka 2012.
Matokeo hayo yanatofautiana na ripoti iliyotolewa awali na maabara moja ya Uswisi, iliyoeleza kuwa Arafat alikufa kutokana na kiwango kikubwa cha sumu ya polonium, baada ya kuigundua sumu hiyo kwenye nguo zake.
Ripoti hiyo ya Ufaransa imepingwa vikali na mke wa Arafat, Suha Arafat, ambaye amesema kifo cha mumewe kilikuwa ni mauaji ya kisiasa yaliyofanywa na mtu wake wa karibu. Akizungumza mjini Paris, Suha amesema ameshangazwa na taarifa zinazokinzana kutoka kwa waatalamu wa Ulaya.
Ripoti hiyo iliyokabidhiwa kwa Suha, haitachapishwa, lakini ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali imesema uchunguzi uliokamilika unaoonyesha kuwa Arafat hakuuawa kwa sumu ya polonium.
Arafat, aliyesaini makubaliano ya mjini Oslo ya mwaka 1993 na Israel, alifariki Novemba mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 75, katika hospitali moja nchini Ufaransa.
Kifo chake kilitokea wiki nne alipougua baada ya kula chakula na hivyo kusababisha kutapika na kuumwa tumbo. Taarifa za kitabibu zilionyesha kuwa alikufa kutokana na kutokwa damu katika ubongo, lakini hakukuwa na maelezo ya nini kilisababisha hali hiyo.
Palestina yapuuzia uchunguzi wa Ufaransa
Afisa mwandamizi wa Palestina, Wasel Abu Yousef, ameipuuza ripoti hiyo ya Ufaransa akisema kuwa iko kisiasa zaidi na iko kinyume na ushahidi unaothibitisha kuwa Arafat aliuawa kwa kupewa sumu.
Wapalestina wengi wanaamini kuwa Israel inahusika na kifo cha kiongozi wao, tuhuma ambazo Israel imezikanusha.
Mkuu wa kamati ya Palestina inayochunguza kifo cha Arafat, Tawfik Tirawi amesisitiza kuwa Israel inahusika na awali alisema atataja majina ya watu wanaoaminika kuhusika na kifo cha kiongozi huyo.
Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Israel, amesema kuwa ripoti ya matokeo ya Ufaransa si ya kushangaza na kuelezea matumaini yake kwamba sasa Arafat atapumzika kwa amani.
Mwaka uliopita, mjane wa Arafat aliitaka serikali ya Ufaransa ifanye uchunguzi wa kifo cha mumewe, baada ya kituo cha televisheni cha Al Jazeera kuripoti kwamba nguo za Arafat zilikutwa na sumu ya polonium.
Waendesha mashitaka wa Ufaransa walianzisha uchunguzi na hatimaye wataalamu wa kupekuwa ushahidi kutoka Uswisi, Urusi na Ufaransa, walichukua sampuli za mabaki ya mwili wa Arafat, baada ya kufukuliwa mwaka 2012.
DW.DE
Ijumaa, 22 Novemba 2013
Mpango mpya kuboresha huduma za uzazi wa kupanga baada ya kujifungua mimba: WHO
Unyonyeshaji mtoto baada ya kujifungua ni mojawapo ya njia za uzazi wa mpango- WHO
Jumatano, 16 Oktoba 2013
Saratani tezi
Huku ukiwa mwezi wa kupambana na janga la ugonjwa wa saratani,watu wengi hawapendi kwenda hospitalini kwa uchunguzi,huku wakihofia kugunduliwa na maradhi ya saratani.
Hii ni baadhi ya sababu zinazopelekea ongezeko la saratani nchini kenya na kanda la afrika kwa jumla.
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu elfu moja(1,000) huugua saratani huku zaidi ya 850 wakifariki kila mwaka.
Takwimu pia zinaonyesha idadi ya saratani ya tezi kibofu inaongezeka marudufu.
Saratani ya tezi kibofu ni ugonjwa ambao huwa
kati ya wanaume.kama aina nyingine za saratani, inapogunduliwa mapema
inakuwa ni rahisi kutibiwa. Zaidi ya hayo, walio hatarini ya
kuambukizwa Ugonjwa huu ni wanaume walio na umri wa miaka 55 na zaidi.
Kulingana na watalaamu wa afya watu wengi hutafuta tiba wakati ugojwa umeenea zaidi.
Hivi
majuzi, ugonjwa wa saratani umetia wengi kiwewe.Siku baada ya siku kuna
habari kuwa mtu fulani ana ugonjwa wa saratani.Waume kwa
wanawake,vijana kwa watoto wote wako hatarini ya kuabukizwa ugonjwa huu.
Watafiti bado hawajapata uvubuzi ni nini haswa inayo sababisha ugonjwa huu hatari.
Hata hivyo inakisiwa kuwa mazingira tunayoishi, kwa njia moja ua nyingine yanachangia kuwepo kwa maradhi haya.
Waziri
Mwenzake, Prof. Anyang Nyongo pia aligunduliwa kuugua saratani ya tezi
kibofu.Kwa bahati nzuri, iligunduliwa mapema na baada ya matibabu ya
muda, madaktari walimhakikishia kuwa amepona.
Pia
mwanahabari mashuhuri Jerry Okungu ana saratabni ya tezi kibofu.Amekuwa
akikabiriana na ugonjwa huu kwa muda sasa.Afueni ni kuwa haja kata
tamaa na ameanzisha wakfu wa saratani ili kuwaelimisha na kuwasaidia
wale wasioweza kugharamia matibabu.
Matibabu ya saratani huwa ghali mno,hivyo basi wale wanaougua wanakubwa na matatizo ya kutafuta matibabu,hii huchangia kuzorota kwa afya na hata maafa.
Ugonjwa huu ambao huambukiza chini ya kibofu cha mikojo,huwapata wanaume weusi kwa asili mia kubwa ikilinganishwa na wale wa asili zingine ulimwenguni.
Ili kutambua kuwa mtu anaugua saratani ta tezi kitofu, wataalamu wa afya hufanya uchunguzi kwa kutumia kemikali ya “Prostate specific antigen” au PSA katika damu ya mgonjwa, ikiwa kuna idadi ya juu ya PSA , waweza kuwa na ugonjwa huu.
· Wanaume wengine wamo hatarini kupata saratani ya mamalia dume:
· Wanaume ambao wamekuwa na jamaa kama baba au kaka ambao washauguwa ugonjwa huu.
· Kula vyakula vingi vya mafuta, nyama nyekundu, siagi na maziwa.
Dalili ya saratani ya mamalia dume:
· Kukojoakojoa kila mara hasa wakati wa siku.
· Kuwa na shida za kuanza kukojoa au kusitiri mikojo.
· Kukojoa kwa matone matone.
· Kuhisi uchungu au moto unapokojoa
· Kuhisi uchungu unapomwaga manii.
· Kukojoa mikojo iliyochanganyika na damu.
Alhamisi, 10 Oktoba 2013
The 2013 International Conference on Family Planning:
Katika juhudi za kuboresha afya ya akina mama,shirika la mpango uzazi duniani litafanya Mkutano wa Mpango uzazi nchini Ethiopia mwezi wa Novemba mwaka huu.
Mkutano huu unafanyika huku karibu watu millioni 900 kote duniani wakikumbatia uzazi wa mpango.
Hata hivyo, sio wote wanaoweza kufanya uzazi wa mpango wakati wanapotaka kufuatia changamoto kadha wa kadha.
Mkutano huu utawajumuisha watafiti wa afya,madaktari na wadau wengine katika sekta ya afya.
Inaaminika
kuwa wazazi wengi ambao wangependa kupanga uzazi wanasubuka sana.Hata
kabla wapate huduma hiyo muhimu wanagundua kuwa ni wajawazito.Idadi ya
wanandoa walio kwenye hali hii ni zaidi ya millioni 215 kote duniani.
Uzazi wa mpango unawezesha wanandoa kufanya maamuzi ya uzazi na ni moja ya njia ya gharama nafuu kwa ajili ya kuboresha afya ya familia.
Uzazi wa mpango unawezesha wanandoa kufanya maamuzi ya uzazi na ni moja ya njia ya gharama nafuu kwa ajili ya kuboresha afya ya familia.
Kilingana na takwimu za shirika laThe Bill & Melinda Gates idadi ya 287,000 ya wanawake hufariki kila mwaka katika hali ya ujauzito.
saratani ya shingo ya uzazi (Cervical cancer)
Huku dunia ikiendelea kuadhimisha mwezi wa saratani duniani,idadi ya wanawake wanaoendelea kufariki kutokana na saratani ya shingo ya uzazi inazidi kuongezeka.
Aina hii ya saratani inasababisha vifo vya wanawake wengi nchi Kenya na duniani kwa ujumla.
katika shughuli zangu za kutafuta habari kuhusu ugonjwa wa saratani,nilipata fursa ya kuwahoji baadhi ya akina mama waadhiriwa na pia waliopona baada ya muda mrefu wa matibabu.
Mama Muthoni Kimani anasema alipona kutokana na ugonjwa huu kugunduliwa mapema,ijapokuwa aina ya matibabu na pia gharama ni ghali mno.
Wetende Ruth anasema kuwa angali anapokea matibabu na hakika ana imani atapoka.Jambo la muhimu ni kujipa moyo,anadokea watende.
"kabla
madaktari kugundua maradhi niliyokuwa nikiugua, nilikuwa nina maumivu
sana.Pia nilikuwa napata hedhi kila wakati,lakini si kufahamu kwamba
nilikuwa tayari naugua saratani ya shingo ya uzazi.
Kwa bahati nzuri.watalamu wa afya walitambua ni saratani ya shingo ya uzazi na papo hapo alianza matibabu".
Kwa sasa amepona na anatowa wito kwa aki mama wenzake wajipimishe mapema ili kuepana na hatari au tishio la ugonjwa huu.
Kulingana
na tarifaa za WHO ugonjwa huu unasabambishwa na virusi viitwavyo Human
Papiloma (HPV) ambavyo dalili zake huanza kuonekana miaka kumi baada ya
mgonjwa kuvipata.
Inakisiwa
kuwa idadi ya wanaougua ugonjwa huu unaongezeka kasi zaidi nchini
Kenya.Huku asilimia 35 wanawake wakihofiwa kuwa na virusi ya Human
Papilloma.Virusi hivi huambukizwa wakati wa kujamiana au kufanya ngono
ambapo mwanamke na mwanaume huambukizana virusi hivi.
Dalili
za ugonjwa huu,ni pamoja na kutokwa na damu ukeni wakati wa tendo la
ndoa, kuvuja damu hata baada ya hedhi,kuwa na maumivu wakati wa kufanya
ngono na pia kutoa harufu mbaya.
Mwaka
wa 2007,serikali ya Kenya ilianzisha mpango wa wanawake kujipimisha
ilikutambua mapema endapo wanaugua ugonjwa huu.Pia akina mama
wanashauriwa kupima kila mwaka, kwa kuwa wengi hupatwa na viashiria vya
saratani hii bila wao kutambua.
Kwa
kuwa kila mwanamke ambaye ameshiriki ngono yuko hatarini ya kupata na
ugonjwa huu.Serikali imetoa rai kwa kila mwanamke ambaye hana ugonjwa wa
saratani ya uzazi kupata chanjo inayopatikana katika vituo vya afya
nchini.
Jumanne, 8 Oktoba 2013
Mwezi wa Oktober ni mwezi wa kuelimisha umma jinsi ya kupambana na ugonjwa hatari wa saratani hususan ile ya matiti.
Hata hivyo juhudu za kupambana na saratani haziridhishi kutokana na ukosefu wa vifaa vya kugundua na kuutibu.
Baadhi ya wakenya wamelalamika kuwa vifaa duni katika hospitali za umma kunachangia ongezeko la idadi ya wanaofariki kila siku kutokana na saratani.
Pia,Upungufu wa watalaamu wa saratani huku baadhi yao kukikimbilia hospitali za binafsi ambapo wanapata mishahara yakulidhisha.
Hivyo basi ni jukumu la serikali kuhakikisha kuna vifaa vya kisasa.Na kuongeza mishahara kwa watalaamu wa afya.
Kwa sasa,idadi kubwa ya wakenya hutafuta matibabu ya saratani nchini India ambapo ghalama ya matibabu ni nafuu.
Hata hivyo, sio kila mtu au jamaa inaweza kugharamia matibabu ya saratani India.
Ni jukumu ya serikali kuhakikisha kuwa wanachi hawafariki kutokana na ugonjwa huu kwa sababu ya gharama au musongamano wa wangonjwa unaopelekewa na upungufu wa vifaa vya matibabu.
Ugonjwa huu umekuwa tishio nchini kenya na pia nchi zinachoendelea.
Hata hivyo,kuna sababu ya kutokufaa moyo ,kwani ugonjwa unapogunduliwa mapema,mgonjwa anaweza akapona.
Baadhi ya dalili ni kama vile;
-Kuwepo kwa uvimbe kwenye sehemu za kwapa
-Sehemu ya titi kuingia ndani
-Mabadiliko kwenye chuchu
-kidonda kwenye chuchu
-chuchu hutokwa damu au maji yasiyo ya kawaida
-ngozi kuwa na rangi nyekundu.
Jumatatu, 27 Mei 2013
midwife
Usimtukane mkunga na uzazi ungalipo.Hii
ni methali inayotuonya tusiwadharau au kuwatukana watu tunaowahitaji kwa jambo
moja au nyingine, maishani
Kwa muda mrefu,wakunga wamekuwa wakitoa huduma zao kwa kina mama wajawazito
hivyo basi wanaheshimika sana katika jamii.
Wiki iliyopita ilikuwa ni wiki muhimu sana kwani umoja wa mataifa ulitenda
siku ya kuadhimisha Fistula
na pia mkutano wa wakunga duniani
unaofanyika Kuala lumpur
Hii ni dhahiri kuwa afya ya uzazi inapewa kipao mbele duniani.
Wakati wa kujifungua kwa mwanamke, anakuwa kwenye hatari zaidi.
Wengi huvuja damu hadi kufa, wengine hupangi na tundu katika sehemu zao za
uzazi-fistula.Pia anaweza akampoteza mwanawe katika hali ile ya kujifungua.
Ni kwa sababu hii akina mama wanahimizwa kuhudhuria vituo vya afya kwa
uchunguzi na mafunzo ya kiafya.
Kulingana na taarifa za Umoja wa Mataifa,Wakunga wamechukua wajibu mkubwa
katika jitihada za kupunguza hatari zinaowakumba wanawake wanapojifungua.
Wakiwa na ujuzi wa juu, wakunga sasa wanaweza kukubiliana na hatari
zinaowakumba akina mama na wana wajibu mkubwa wa kuyaweka maisha ya mama
kuwa salama kote duniani.
Wakunga huwauguza akina mama kabla na baada ya kujifungua, wanalinda afya za
watoto wanaozaliwa , wanatoa ushauri kuhusu upangaji uzazi, wanazuia maambukizi
ya ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na wanafahamu wakati wa
kuitisha huduma za dharura.
Inakadiriwa kuwa wakunga walio na mafunzo na wanaopata msaada wanaweza
kuokoa maisha ya zaidi ya wanawake 200,000 kila mwaka na mara kumi zaidi
ya watoto kiasi hicho.
Washiriki katika kongamano na kuala lumpa wanasema kuna haja ya kuongeza
idadi ya wakunga duniani ilikuepuka maafa yanayotokea wakati wakujifungua.
Pia hamazisho kwa akina mama ni muhimu;jambo ambalo mataifa yanayositawi na
pia yaliostawi yanalitilia mkazo.
Ingawa pia wakunga wa jadi wanaheshimiwa kwa huduma zao, mara kwa mara
hawana vifaa maalum endapo mama atashindwa kujifungua kwa njia ya kawaida.Hivyo
basi wanahitaji kuelimishwa jinzi ya kukambiliana na hali za dharula.
Gharama za matibabu na umbali wa vituo vya afya ni changamoto ambalo pia
ninastahili kushughulikiwa kwa haraka na serikali husika.
Endapo malengo yamilenia ya afya ya uzazi itaafikiwa basi ni sharti
wahudumu wa afya washirikishwe .
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)