Jumatatu, 7 Septemba 2015

Flibanserin -Tembe ya kusisimua mapenzi


Image result for flibanserin
jambo la kutosisimuka kwa kimapenzi uwa ni jambo ambalo halizungumziwi kila mahali kwani akina mama wengi wanaliona la aibu.
Lakini wataalamu wa maswalaFlibanserin 




Tembe ya kusisimua mapenzi


Wanawake kupungukiwa na nguvu na hamu ya kufanya mapenzi imek la afya ya akina mama wanaliona swala la kawaida ambalo linaweza kurekebishwa kwa matibabu.

Lakini habari njema ni kuwa vidonge vya kuwaimarishia  wanawake hamu au hisia za kitendo cha ngono imeidhinishwa.Hii ni afueni ambayo itaondoa aibu au kufujika kwa ndoa kutokana na kutoridhisha waume wao.

Wataalamu wa afya wanasisitisha kuwa kuna tofauti ya tembe hizi na zile za kiume za Viagra .

Shirika moja la Amerika la kuidhinisha na kusimamia dawa liliidhinisha tembe za Flibanserin kutumiwa kusisimua akina mama kimapenzi baada ya kufanya utafiti na kupata kuwa tembe hizi ni salama.

Ingawa madaktari wanasema kunatofauti kubwa kati ya tembe hizi na zile za kiume ,wakenya wanasitaja kama Viagra ya wanawake.
Wanawake wanaopata hedhi na wanaopungukiwa na hamu ya kimapenzi ndio wanakusudiwa kufaidika kutokana na usiduzi huu.

Kuna hali ya msisimuko kwa wanawake lakini itakuwa ni muhimu kutumiwa kufuatia ushauri wa daktari kuepuka madhara ya kiafya yanayosababishwa na matumishi mabaya ya dawa yeyote.

Wataalamu wa tiba hii wa kampuni ya Sprout Pharmaceticals ambayo tayari  inayopatikana  Marekani itatibu wanawake wasio changamka kimapenzi.

Tafiti zinaonyesha kuwa kati ya wanawake kumi mmoja anakubwa na hali ya kutochangamka kimapenzi.
Mabadiliko ya homoni mwilini,kutojidhamini, matatizo ya akili na matatizo mengine ya kisaikolojia yanachagia upungufu wa kuchangamka kimapenzi kwa akina mama.

Kufuatia uzinduzi huu baadhi ya akina mama niliyowahoji hawajachangamkia au hawajafurahishwa na hali hii.Wanasema japo litasaidia,itakuwa kwa labda asilimia 60 lakini kuna haja ya kutafuta suluhu ya kudumu .”hili ni tatizo la kisikolojia na kuna haja akina mama pia watafute matibabu zaidi kuliko kutegemea hii tembe pekee yake,alinifahamisha Janet Kavindu ambaye ni mkazi wa Machakos.

Margaret Wathoni anasema ni jambo la kutia moyo kwa uvumbuzi huu na atatafuta ushauri wa daktari ilikujua zaidi,akisisitiza kuwa ni kama vile anautafuta ushauri wa kiafya anapotaka kutumia dawa za uzazi mpango.

“Nina raha asana kusikia kuna tiba ya tatizo hili.Nitataka kujua zaidi ili ni chukue hadua mwafaka kwangu mimi,anasema Wathoni.

Lakini kuna wanaume ambao wanaona kama temebe hizi ni tatizo kwani sitaleta mchangamko hadi akina mama wengine waamue kutoke nje ya ndoa.
Muda tu ndio utaonyesha endapo tembe hii itatatua shida za kimapenzi baina ya walioko kwenye ndoa na yeyote ule au itakuwa ni tatizo.








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni