Hitilafu
ya mashine ya miyale ya umeme (Radio therapy machine)
Mashine
inayotumia miyale ya umeme kutoa matibabu ya saratani na hali duni ya vifaa
hivyo katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta yatishia maisha ya wagonjwa wa
saratani nchini.
Imekuwa
ni hali yakughadhamisha katika hospitali kuu ya kenyatta hapa jijini Nairobi wakati
wagojwa wa saratani wanapofika kwa matibabu lakini wanakabiliana na hali ngumu
kufuatia upungufu au kuharibika kwa mashine za matibabu mara kwa mara.
Kufuatia
hali hii wagonjwa wengi wasio na uwezo wa kutafuta matibabu kwingineko ,huteseka
na hali zao kudhoofika wasijue la kufanya.
Hata
hivyo hospitali ya Kenyatta kupitia wakuu wake wametafuta matibabu hayo katika
hosptali za binafsi kwa wagonjwa wanaohitaji matibabu ya dhalura.Lakini swali
ni je hali hii inaendelea hadi lini?
Hii
si mara ya kwanza au ya pili kwa vifaa
hivyo kupata hitilafu.Miezi mitatu tu, iliyopita wagonjwa walijipata hatarini wakati
mashine zilipata hitilafu ,huku mmoja wao wagonjwa akisusia chakula na
kujifungo minyororo kwenye kizingiti za mti nje ya mlango wa matibabu ya dharula.
Swali ni je hali hii itaendelea hadi lini?
Selikali
ya kitaifa imetengea hela sekta ya afya
kuhakikisha matibabu yanapatikana bila matatizo katika hospitali zetu .Hata
hivyo vifaa vinavyohitajika kwenye hospitali huwa ni vichache au havipo.
Hakika
wagonjwa wanahofia kuwa hali hii ikiendelea bila hatua ya kudumu kuchukuliwa au
kurekebisha hali hii,maisha yao yatakuwa
hatarini.
Asili
mia 80 ya wagonjwa wanaofika Kenyatta kwa matibabu wanatoka mashinani au majimbo,kwa
dhana kuwa hospitali ya Kenyatta
hospitali inazo mashine za hali ya juu kiteknolojia ,wala kwa sasa hali
si hivyo.
Mmoja
wa wagonjwa hao ni Mariam ambaye ni mkaazi wa Mombasa na amefika katika
hospitali ya Kenyatta kufuatia maagizo ya daktari ,kuwa kila baada ya mwezi
inambidi aendelee na matibabu yake.
Lakini
la kuhuzunisha ni kuwa alipofika ,alipata habari kuwa matibabu yake
hayataendela kama alivyotarajia kufuatia vifaa” kugoma kufanya” kazi..
Kufuatia
hali hii hana budi kusubiri hadi mashine zirekebishwe au mpya zinunuliwe.
Hana
raha,afya yake imedhoofika na pia ni mchofu kufuatia safari ndefu kutoka Mombasa
hadi Nairobi.
Ni
jukumu la kila mgonjwa kufuatilia matibabu kama anavyoagizwa na daktari,lakini
mara kwa mara hali hii inakuwa mbaya wakati mgonjwa analazimika
kurudi nyumbani bila matibabu au kusubiri kwa muda mrefu,kutokana na utepetevu
wa wahusika wakuu katika wizara za afya au wasimamishi wa hosptali hii.
Maoni
Ni
jukumu la serikali kuchukuwa hatua za dharura kurekebisha hali hii ambayo ni ya
kughadhabisha katika hospitali kuu ya kenyatta.
Hii
ni hospitali inayotegemewa na mamilioni ya wakenya kutoka kote nchini.Kenyatta
ni hospitali ya rufaa huku hospitali za majimbo zikiwatuma wagonjwa wanaohitaji
matibabu ya dharura Kenyatta,kutokana na ukosefu au upungufu wa vifaa vya
matibabu vinavyoabatana na techonolojia ya kiasasa.
Hivyo
basi ni jambo la kuhuzunisha kwa wagonjwa na wakenya kwa jumla kuona kuwa
tegemeo lao la kupata matibabu limekuwa kama kitendawili au ndoto tu>>
Matibabu
ya miale au radiotherapy inahitajika kwa asilimia 80 kwa wanaougua saratani na kila
mgonjwa analazimika kulipa shilingi 500 kwa kila wakati anapofika kwa matibabu.
Kusubiri
kwa muda mrefu huku ugonjwa ukiendelea kuenea mwilini si jambo la
kupendeza.Itapata mgonjwa anaugua lakini kufuatia idadi ya wagonjwa inambidi
kusubiri zaidi ya mwaka mmoja au miwili ilianze kupata matibabu.
Hii
hupelekea vifo ambavyo vingezuiliwa endapo matibabu ya haraka au wakati ufaao
yalitolewa.
Hili
ni swala anbalo linastahili dharura maana hapa tunaangazia afya na maisha ya mwanadamu ambayo ni yadhamana.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni