COP26 Glasgow,Scotland
Viongozi na wajumbe kutoka takriban nchi 200 wanakongamana kwenye kongamano la Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya hali ya anga,ambalo limengoa nanga huko Glasgow,Scotland,leo Katika mkutano huu wa COP26, maswala kadha yatajadhiriwa hususan jinsi ya kupunguza utoaji gesi ya carbon kufikia mwaka 2030 na kunusuru dunia kutoa kwa adhari za mabadiliko ya hali ya anga. K ongamano hili litafanyika kwa majuma mawili,huku fursa ya kwanza ikitolewa kwa Shirika la utabiri wa hali ya anga duniani ili kutoa ripoti kuhusu hali ya anga ilivyo kufikia sasa.Lengo likiwa kutathmini viwango vya joto duniani kufikia mwaka huu na miaka ya awali. Zaidi ya hayo, ripoti imeandaliwa na itatolewa na wanasayansi wa hali ya anga. Hali ya anga imebadilika kwa kasi huku shughuli za wanadamu zikitolewa kama chanzo kuu cha mabadiliko hayo. Viwango vya juu zaidi vya joto, mafuriko na moto misituni inazidi kuongezeka,jambo ambalo linatia hofu. Mkutano huu una...