Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2011

kongamano la uzazi mpango Dakar,Senegal

Picha
Kongamano kuhusu afya ya uzazi yaanza leo jijini Dakar nchini Senegal. Mkutano huu unafanyika huku karibu watu millioni 900 kote duniani wakikumbatia uzazi wa mpango. Hata hivyo, sio wote wanaoweza kufanya uzazi wa mpango wakati wanapotaka kufuatia changamoto kadha wa kadha. Mkutano huu utawajumuisha watafiti wa afya,madaktari na wadau wengine katika sekta ya afya. Kufanyika kwa mkutano huu katika Afrika Magharibi,ni jambo la muhimu ikifahamika kuwa nchi za Afrika Magharibi zinaongoza kwa idadi ya watu kwani mpango wa uzazi ungali haujapewa kipao mbele. Pia kupata hutuma ya uzazi wa mpango ni shinda. Inaaminika kuwa wazazi wengi ambao wangependa kupanga uzazi wanasubuka sana.Hata kabla wapate huduma hiyo muhimu wanagundua kuwa ni wajawazito.Idadi ya wanandoa walio kwenye hali hii ni zaidi ya millioni 215 kote duniani.   Uzazi wa mpango u nawezesha wanandoa kufanya maamuzi ya uzazi na ni moja ya njia ya gharama nafuu kwa ajili ya kuboresha afya ...

FGM (ukeketaji) Kenya

Ukeketaji Ni asubuni na mapema,jua linapoanza kuchomoza,katika kijiji kimoja katika Mkoa wa Mashariki. Kundi la akina mama linafululiza hadi kwa mama mwenzao, huku wakiimba nyimbo za kitamaduni. Kisa na maana ; hajakeketwa. Nia yao haswa ni kutumia nguvu kumkeketa kwani ni kero kwa wanawake wa kijiji chao. Kulingana na mila na desturi ya jamii hiyo ni sharti mwanamke akeketwe anapokaribia kuvunja ungo.Lakini kwa mama Matani* aliolewa kabla hajakeketwa. La kuhuzunisha ni kwamba yeye ni mjamzito na kitendo hiki kinaweza kuhatarisha maisha yake. Kwa bahati nzuri,anaepuka gadhabu ya akina mama hao baada ya chifu wa kijiji hicho kuingilia kati.Wanarudi makwao huku wakiapa kumuadhibu mama Matani* baadaye. Wakati wakujifungua ,yule mama hana budi kuwaita baadhi ya wale wanawake kumsaidia kujifungua. Sasa wanapata nafasi ya kumkeketa katika ile harakati ya kuzaa.Anajifungua mtoto na afya zake,anakeketwa na sasa ni mama kamili…..unyama ulioje?  Hii si hadithi bali ndivyo hali ilivyo katika ...

wakunga wa jadi na uzazi

Wakunga wa jadi na uzazi Katika kitongoji duni cha Korogocho,kundi la akina mama wajawazito wamepiga foleni wakisubiri kuhudumiwa. Baadhi yao wana uchungu ambao unadhihirika wazi unapowatazama. wana matumaini watapata afueni punde tu watakapomwona mama ambaye wanamuenzi. Mama huyu,Jacinta Akinyi, anajulikana kama daktari katika kijiji hiki.Hakika ni kuwa hana elimu yeyote katika taaluma ya udaktari. Yeye ni mkunga ambaye ana juhudi kama ya mchwa."Daktari" huamka asubuhi na mapema ili kuwahudumia akina mama ambao hawana uwezo wakutafuta matibabu au uchunguzi wanapokuwa katika hali ya ujauzito,katika hospitali za umma. Gharama ya kujifungua hapa nchini Kenya ni ghari mno,ikilinganishwa na ya wakunga.  Pia hali ya ukosefu wa usalama katika  mitaa duni ni changamoto kwa mama anayepata uchungu wa kujifungua wakati wa usiku. Mama Ona ni  baadhi ya akina mama wanaosubiri kujifungua. ingia kwenye chumba ambacho ndani kuna kitanda ambacho kimefichwa na pasia. mkunga akotayari k...

family planning(uzazi wa mpango)

Picha
Aina ya uzazi wa mpango Kuna   aina za uzazi wa mpango ambazo   mama au baba anaweza kutumia ili kuepuka kupata watoto wasiotarajiwa. Aina ya uzazi wa mpango Mpira au kondomu Kuna kondomu za akina baba na mama pia. mwanamume anapotumia kondomu inazuia mbegu zake kuingia kwenye mji wa uzazi wa mwanamke. -Ni rahisi kutumia -inakinga magonjwa ya zinaa na virusi vya HIV -Inazuia mwanamke kupata mimba isiotarajiwa Shindano(Depo Provera) Hii njia inafaa kwa mama ambaye hapendi kumeza vidonge na ambaye ameshazaa. Mwanamke hupata sindano hii ya homoni kila baada ya miezi mitatu. Hata hivyo mwanamke anapochagua kutumia aina hii ya uzazi wa mpango ni sharti aelewe kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo atakubana nayo kama vile;Kukosa hedhi au kupata hedhi kiasi kidogo. Pia kuna uwezekano wa kukawia kupata mtoto baada ya kuacha kutumia shindano kwa matarajio ya kutunga mimba. Vijiti Hivi ni vijiti vya plastiki vinavyowekwa chini ya ngozi ya mama.vinatolewa kila baada ya miaka mi...

population (idadi ya watu)

Huku idadi ya watu ikifikia billioni 7 duniani, kuna haja ya kuudwa kwa mikakati mwafaka, ili kukabiliana na changamoto zinazoabatana na ongezeko la watu.   Kulingana na takwimu zilizotolewa na umoja wa mataifa, idadi ya watu, inakadiriwa kuongezeka hadi billioni 9 ifikapo mwaka wa 2050. Barani Afrika hivi sasa idadi imefika billioni moja na inatarajiwa kuongezeka marudufu ifikapo 2050. Zaidi ya hayo, Bara la Afrika lina kibarua kigumu kutafuta shuluhu la haraka na la kudumu   ili kuhakikisha idadi ya   watu imedhibitiwa. Umaskini, uhaba wa vituo vya afya,upungufu wa madawa ni baadhi tu ya changamoto nyingi ambazo zimeendelea kuwa tishio. Ili kufikia malengo ya milenia ya afya sharti maswala ya elimu, matibabu(afya), usalama wa chakula na ajira yatiliwe maanani. Baadhi ya suluhu ni kuimarisha kampeni ya uzazi wa mpango.Hata hiyo kampeni hizo zisiwalenge pekee akina mama bali akina baba wahusishwe pia. Kwa muda mrefu mwanamke ndiye anayelengwa na uzazi wa mpango h...

shindano ya homoni ya depo provera

Uzazi wa mpango Ni ile hali ya mume na mkewe kukumbaliana jinzi au namna ya kupunguza mimba zisizotarajiwa. Serikali ya kenya imetilia mkazo umuhimu uzazi wa mpango.Zaidi ya hayo, kuna namna   na aina tofauti za uzazi wa mpango. Kuna vidonge vya kumeza, shindano ijulikanayo kama Depo provera, Vijiti, kitanzi, mpira wa mama au baba,kufunga kizazi kwa mama au baba na njia za asili. Ukweli ni kuwa, ni mpira pekee kati ya   aina zote za mpango wa uzazi inayozuia maambukizi ya ugonjwa. Aina zinginezo hazizui kupata magonjwa ya zinaa na pia virusi vya ukimwi. Bali na hayo, kuna dhana potofu kwa baadhi ya watu   wanaoamini kuwa matumishi ya auna hizi zote za uzazi wa mpango zinazuia maambukizi ya magonjwa ya zinaa na virusi ya ukimwi. Kulingana na utafiti uliofanywa na shirika moja la afya la Marekani na kuchapishwa na jarida la The Lancet, akina mama wanaotumia aina hii ya upangaji uzazi wako   hatarini ya kuambukizwa au kuwaambukiza waume wao virusi vya HIV,kuliko w...