Kuna aina za uzazi wa mpango ambazo mama au baba anaweza kutumia ili kuepuka kupata watoto wasiotarajiwa.
Aina ya uzazi wa mpango
Mpira au kondomu
Kuna kondomu za akina baba na mama pia.
-Ni rahisi kutumia
-inakinga magonjwa ya zinaa na virusi vya HIV
-Inazuia mwanamke kupata mimba isiotarajiwa
Hii njia inafaa kwa mama ambaye hapendi kumeza vidonge na ambaye ameshazaa.
Mwanamke hupata sindano hii ya homoni kila baada ya miezi mitatu.
Hata hivyo mwanamke anapochagua kutumia aina hii ya uzazi wa mpango ni sharti aelewe kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo atakubana nayo kama vile;Kukosa hedhi au kupata hedhi kiasi kidogo.
Pia kuna uwezekano wa kukawia kupata mtoto baada ya kuacha kutumia shindano kwa matarajio ya kutunga mimba.
Vijiti
Hii aina inafaa akina mama ambayo wana watoto na wanataka kupumzika kuzaa kwa muda mrefu.
Kitanzi
Hiki pia ni kifaa cha plastiki ambacho tofauti na vijiti kinakaa kwenye mji wa mimba.
-Inafaa kwa mwanamke aliye na mpenzi mmoja.
-Mbegu za mwanamumu zinazuiwa na kitanzi kukutana na yai la mwanamke.
-Inadumu kwa miaka kumi.
-Punde tu baada ya kutolewa mwanamke anaweza kutunga mimba.
-Inaweza kutolewa wakati wowote.
Adhari
Ni hatari kwa mwanamke aliye na wapenzi wepenzi wengi.
Kufunga kizazi
Hii ni operesheni au upasuaji unaofanywa kuzimba njia ya mayai ya mama au bengu za baba ili zisikutane.
Aina hii inamanufaa kwa mama na baba ambao wana watoto na hawataraji kuzaa tena.
Pia njia hii haizui kujamiana(tendo la Ndoa)
Isitoshe, namna hii, haina madhara yeyote.
Tembe (vidonge)
Mama humeza kidoge kimoja au viwili kila siku
-Haizui magonjwa ya zinaa .
-Mama pia anahitaji kupimwa shinikizo la damu mara kwa mara.
La muhimu ni kujua kuwa aina hizi haizui mtu kupata magonjwa ya zinaa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni