Alhamisi, 5 Julai 2012

Arafat

Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat watoa majibu nusu.


marehemu Arafat wakati akiwa mwenye afya nzuri

marehemu Arafat baada ya kuugua
 
 Uchunguzi wa kisayansi uliyofanywa kuhusu kifo cha aliyekuwa kiongozi na rais wa Wapalestina umetoa majibu nusu tangu kuanza kwa uchunguzi huo.
Rais Yasir Arafat ambaye alifariki dunia nchini Ufaransa ambapo alipelekwa kwa ajili yamatibabu baada ya kuugua wakati akiwa amefungiwa  kutoka katika mji wa Ramallah na serikali Izrael.
 
Dr Francois Bochud ambaye ni mtaalamu wa Radiophysique iliyopo nchini Switzerland alisema " naweza kusema tumekuta aina ya gesi inayo julikana kama polonium-210 ambayo inaweza kuwa chanzo ca kifo chake na tunaweza kupata jibu sahihi ikiwa baadhi ya viungo vya marehemu Yasir Arafat vitapatikana kwa  uchunguzi zaidi."
 
Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat ulikuja baada ya mkewe Suha Arafat  kuruhusu uchunguzi kuendelea na kutoa ruhusa ya kuwa mwili wa Yasir Araf ufukuliwe kwa uchunguzi zaidi  na kuiomba serikali ya Wapalestina kushirikiana naye.

Wasifu wa arafat
Alikuwa kiongozi shupavu wa Palestina  aliyeenziwa na wale alioongoza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni