Waziri wa afya ya umma Beth Mugo apona kansa.ugonjwa wa kanza ume kuwa tishio hapa nchini Kenya na pia mataifa mengi ya Afrika.
hata hivyo kulingana na waziri beth Mugo ugonjwa huu unaweza kudhibitiwa na kupoona endapo utagunduliwa mapema.
Akizungumza
jana baadha ya kuasiri kutoka Marekani ambako amekuewa akipokea
matibabu ya kansa, waziri Mugo ametangaza kuwa kenya itafungua kituo cha
Kansa nchini ilikuwatibu watu wanaougua ugonjwa huo.
Bi
mugo aligunduliwa kuugua kanza ya matiti na kwa bahati nzuri
iligunduliwa kabla haijaenea na kwa sasa anasema ako salama salimini.
Pia
waziri mugo alionya wakenya kuhakikisha kuwa wanaishi kwenye mazingira
safi, kwani uhalibifu wa mazingira hunachangia kuenea kwa ugonjwa hatari
wa kansa.
"Hewa safi, mazingira mema na lishe bora ni muhimu kwa kuepa maradhi ya kansa.
Ni
jukumu letu kama wakenya kudumisha usafi na pia upanzi wa miti ili
kupata hewa safi.Hii itakuwa ni njia moja ya kuepuka maradhi hatari ya
kansa.
Hivi majuzi rais Mwai kibaki aliidhinisha mswada wa kansa nchini,hii inapika hatua kupwa ya kukabiliana na ugonjwa huu.
matibabu
ya kasa hapa nchini yamekuwa wa changamoto kadha wa kadha; kama vile
ukosefu wa vifaa vya ukaguzi wa saratani, kampeni ya kuwafahamisha
wananchi madhara na dalili za saratani,ghalama ya juu ya kutibu ugonjwa
huu baadhi ya matatizo mengine.
Sadifa ni kuwa waziri
wa afya ya umma na mwenzake wa humuda za afya Anyang Nyongo wamekuwa
wakiugua saratani lakini wote wamepona, baada ya kupokea matibabu
marekani.
Baadhi ya saratani ambayo inaadhiri wa kenya
wa kike ni;saratani ya sehemu ya uzazi na ile ya matiti, huku wanaume
wakiugua saratani ya koo na ya prostate.
Endapo
serikali itachukua jukumu ya kutafuta yamna ya kukomesha kuenea kwa
saratani hapa nchini ,itakuwa afueni kwa wananchi ambao gharama ya
matibabu imekuwa ni ghali mno hadi wanaamua kutotafuta matibabu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni