Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson
Mandela, anaendelea kupokea matibabu hospitali mjini Pretoria ambako anatibiwa kwa ugonjwa wa
mapafu.
Mzee Mandela alipelekwa na kulazwa hospitali,
Jumamosi(wiki moja iliyopita).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Rais Jacob Zuma, aliyemtembelea, Mandela naendelea kupata nafuu.
Mapema mwaka huu, Mandela alilazwa hospitali ili kutibiwa matatizo ya tumbo yaliyokuwa yamemsumbua kwa muda mrefu.
Homa ya mapafu, husababishwa na viini tete vijulikanavyo kama (Streptococcus pneumoniae) na huathiri sehemu za kupumua kwenye mapafu.
Bwana
Mandela amewahi kutibiwa kwa mara nyingine ugojwa wa kifua kikuu unaoathiri mapafu.
Magonjwa
mengi ya mapafu hutibiwa kwa madawa , mgonjwa kupumzika au kupata
vinywaji vingi.
Wazee na watu ambaom hawakinga ya mwili ndiyo
huadhiriwa na maradhi haya.
Bwana Mandela ana miaka 94.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni