MTANGAZAJI AUGUA SARATANI
Mtangazaji Janet Kanini Ikua
amegunduliwa kuna anaigua saratani ya mapafu.
Kanini alisema kupitia mtandao kuwa
ako nchini India ambako anaendelea kupokea matibabu.
Hapo awali Kanini alikuwa pia
alipatikana na ugonjwa wa damu kuganda kwenye misipa inayopeleka damu kwenye
roho.
Kiinim chake hasa kuzuru India ilikuwa ni kupokea matibabu ya ugonjwa huo ujulikanao kwa kimombo kama Deep Vein Thrombosis.
Dalili ya ugonjwa huu ni kufura miguu na pia kuwa na uchungu miguuni unaomfanya mgonjwa kuwa na matatizo ya kutembea.
Daktari wake aliyemtaja kama wakutajika nchini India amemhakikishia kuwa akiendelea na matibabu kwa muda wa miezi sita au zaidi atapona,ingawa unaweza ukarudi.
Kwa sasa anapokea matibabu kuhakikisha damu iliyoganda haifiki kwenye roho au moyo ambazo ni viungo muhimu sana mwilini.
deep vein thrombosis,
deep vein thrombosis,
deep vein thrombosis,
Hata baada ya hali yake hiyo Kanini
alisema anahakika kuwa Mola atamponya na atarejea nyumbani Kenya baada ya
matibabu.
ALISEMA nia ya kusema kuhusu hali yake
ilikuwa kuwapa motisha wengi wanaopitia hali kama hiyo ili wasife moyo na
waendelee na kutafuta matibabu bila wasiwasi.
Kulingana na takwimu za shirika la
afya ulimwenguni WHO idadi ya wanaougua ugonjwa wa saratani unaendelea
kuongezeka.
Ingawa ugomjwa huu ni baadhi ya
maradhi hatari ,inatibiwa na mgonjwa akapona,mradi atafute tiba mapema.
Kwa upande wa Kanini matibabu
yanachukuwa muda.Pia gharama ya matibabu nchini India gharama ni nafuu ikilinganishwa
na nchini Kenya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni