Jumatatu, 15 Februari 2016


Masaibu ya wagonjwa katika hospitali ya Mama Lucy Kibaki

Mama Lucy Kibaki hospitali iliyoko Embakasi imegonga vyombo vya habari kwa sababu za kuhuzunisha.

Image result for mama lucy hospitalHuduma duni za matibabu,ufisadi ni baadhi ya madai yanayotolewa na wagonjwa ambao wameadhirikakwa njia moja au nyingine.

Visa vya wagonjwa kutohudumiwa ipasavyo na madai ya ukosefu wa vifaa vya matibabu vinahusunisha.

Kisa cha kustajabisha ni kuwa madaktari walimwacha mama mja mzito bila kuhudumiwa kwa muda hadi wanawe mapacha kufia kwenye kizazi.

Imedaiwa kuwa mtoto aliyekuwa na majeraha ya ajari aliruhusiwa kwenda nyumbani hata kabla ya uchunguzi wa kina kuhakikisha kuwa maisha yake hayakuwa hatarini

Mamake mtoto anasema mwanawe aliaga dunia siku oja baada ya kwenda nyumbani.

Baadaye daktari katika hospitali hiyo wakamfahamisha kuwa alivuja damu kwa ubongo,kwani alikuwa na majeraha jichoni.

Hayo ni baadhi ya masaibu yanayowakuba wagonjwa kwenye Hospitali ambayo ni ya pili kwa ukubwa jijini Nairobi na ya tatu nchini.

Madhumuni ya kuanzisha hospitali hii ilikuwa kupunguza idadi kubwa ya wagonjwa katika hospitali kuu ya Kenyatta




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni