Ijumaa, 31 Mei 2019

Women deliver,Vancouver,Canada 2019



Women Deliver 2019 Conference 

Shirika linalo ongoza katika juhudi za kutetea haki na afya ya akina mama , Woman Deliver imetayarisha kongamano la usawa wa jinsia,haki na ustawi wa wasichana na wanawke utakaofanyika huko Vancouver nchini Canada mwanzoni mwa mwezi wa Juni mwaka huu.
Mkutano huu unalenga maswala ya jinsia na afya ya akina mama na wasichana katika karne ya 21.

Wadau kutoka sekta ya afya,vijana,wasomi,wanaharakati na waandishi wa habari kutoka nchi zaidi ya elfu sita(6,000) wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huu.Waakilishi kutoka  Shirika la afya ulimwenguni,WHO watajiunga na wadau hawa katika mkutano huu unaotajwa kama mkubwa kufanyika Canada.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO Daktari Tedros Adhanom Ghebreyesus, anasema usawa  wa kijinsia lazima uwe msingi wa afya kwa wote .
Rais wa Women deliver Katja Iversen anasema shirika lake limejitolea kuwapa matumaini akina mama kwa vitendo na sio kwa maneno matupu.
Image result for dr tedros adhanom ghebreyesusAnasema kuwa huu ni mkutano wa tano kufanyika duniani na canada imepiga hatua ya kuigwa na nchi zingine duniani.Iversen anamatumaini mkutano huu utakuwa na matokeo na faida nyingi kwa wanawake n watu wote kwa ujumla.
Mada kuu ya mkutano huu ni kuhakikisha maswala na akina mama na wasichana napewa kipao mbele ili kufanya duniani bora zaidi.
Haki za mama za kiafya,kielimu na maswala nanayohusiana na uzazi wa mama unatiliwa maanani hapa huku ikifahamika kuwa akina mama wanachanga moto za kifya .Mwanamke mwenye afya bora anatekeleza majukumu yake bila tatizo.Hii inachangia kwenye uchumi wa nchi kwani akina mama wana changia kukua kwa chumi za nchi kote duniani.
Idadi ya akina mama pia inaongoza ikilinganishwa na ya wanaume kote duniani.
Hivyo basi mchango wao hauna budi kuheshimiwa.

Changamoto zipo zinazowakabili akina mama kila siku kama vile ukosefu wa huduma za afya karibu na makazi yao.Hasa akina mama wajawazito ambao hulazimika kutumbea muda mrefu kutafuta huduma za afya.Nchi zinazoendelea zikiadhirika zaidi.Bei ya matibabu ni swala ambalo pia limekuwa ngumu.
Sio wengi hususani akina mama wa mashambani wanao uwezo wakulipa gharama ya matibabu.

Katika mkutano wa Canada maswala yote haya yatatafutiwa mikakati mwafaka na suluhu kuhakikisha akina mama na wasichana wamepata haki zao za kiafya na kijumla.
Waziri mkuu wa Canada ,Justin Trudea  amewakaribisha wanaohudhuria kongamano.
Image result for women deliver presidentImage result for women deliver 2019Amewataka kutumia muda wao kujadili maswala ya jinsi ;na kutafuta mikakati ya kudumu.

 Elimu ya uzazi wa mama pia ni ya muhimu,kupitia hii elimu mwanamke anaelimika na kujua haki zake za uzazii ,jinsia na jinsi ya kuzitekeleza au kufuata haki hizo anapokuwa kwenye tatizo fulani la kiafya au kiajamii.
Bila kutatua changamoto hizi itakuwa ni vugumu kufikia malengo au agenda ya afya na maendeleo endelevu ifikapo mwaka wa 2030.
Kongamano hii inafanyika wakati muhimu sana katika maisha ya wanawake kiafya ,kielimu na kiuchumi.

Hasa nchini Canada wamepiga hatua marudufu kuhakikisha haki hizi zimetekelezwa.
Kuna pia baadhi ya nchi za Afrika ambazo zimepiga hatua na kuweka maswala ya jinsia  mstari wa mbele ili kuendeleza jamii na taifa kwa jumla.
Mkutano huu utafuatilia kwa kina maswala yaliojadiliwa hapo mwanzo katika kongamano lililofanyika Copenhagen,Denmark mwaka wa 2016.

Namna ya kutatua ,Ndoa za mapema ,sodo za wanawake na ukeketaji ni maswala yaliojadiliwa hapa.

Rais wa Ethiopia,Sahle Work Zewde na Mke wa Waziri Mkuu wa Canada,Sophie Trudeau ni miongoni mwa watakaohutubia kikao hiki.

Kongamano la shirika la Women Deliver hufanyika kila baada ya miaka mitatu. 




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni