Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta ataondoka
nchini wiki ijayo kuelekea nchini Canada kuhudhuria kongamano la maswala ya jinsia na afya ya akina mama na wasichana ilioadaliwa na shirika la Women
Deliver.
Rais Kenyatta ni miongoni mwa wakuu wa
mataifa na serikali waliopokea mwaliko wa waziri mkuu wa Canada Justin Trudeau.Mkutano huo utaadaliwa jumatatu hadi jumatano
wiki hii ,utaangazia maswala ya ya jinsi, afya na haki za wanawake.
Nchini ya kenya ni miongoni mwa nchini
ambazo zinajitahidi kupiga hatua katika maswala na jinsia na haki za akina
mama.
Serikali,kupitia bima ya afya ya kitaifa
inatoa huduma ya linda mama ;huduma hii inasaidia wa mama kupata huduma ya
matibabu ya bure wanapoeenda kujifungua popote nchini kenya.
Mama waTaifa ,Margaret Kenyatta pia amekuwa
katika mstari wa mbele kuchangia katika afya ya akina mama hasa wenye uja
uzito.
Amekuwa akifanya mbio za kuchangisha pesa
ili kuhakikisha akina mama waja wazito na waliojifungua na watoto wao wanapata
matibabu bila malipo.Huduma hii inawasaidia walio mashinani kufikiwa na huduma
za afya bila vikwazo.
Rais atahutubia mkutano huo na pia atafanya
mikutano ya mubadala na mwenyeji wake Justin Trudeau.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni