Huku
dunia ikiadhimisha siku ya hedhi, maswala ya hedhi na usafi wake yangali ni
changamoto hususan barani Afrika.
Yeye ni mwanafunzi wa shule ya msingi
darasa la nane katika maeneo ya Kabiti Muranga.
Kwa muda mrefu Muthoni amekubwa na changamoto
tele wakati wa hedhi.
Pia ana ona haya kwenda shuleni kwa kuogopa
hedhi kuvuja na kuchekelewa na wenzake.
Hii imepelekea yeye kupotesa muda wengi
kila mwezi na mwaka kwa jumla.
Masomo yake yameadhirika pakubwa na amewahi
kurudia darasa kotokana na matekeo duni ya mtihani wa kila mwaka.
Angetaka serikali iweke mikakati ya
kuhakikisha kila mtoto wa kike ambaye anapata hedhi ,ana taulo au sodo kila
mwezi na pia maji iwepo shuleni ilikudhumisha usafi.
Anasema vyoo wanavyo tumia pia ni changamoto
kwani ni chafu na ambazo hazistahili kutumiwa.
Anapendekeza;kuwe na vyoo na vyombo maalum
za kuhifadhia sodo baada ya matumizi
Muthoni ni baadhi ya wasichana wanaolengwa
kupata elimu kuhusu hedhi na umuhimu wa usafi wakati wa hedhi na mashirika
isiyo ya kiserikali na watu binafsi wanaojitolea kuhakikisha wasichana hawakosi
masomo juu ya hedhi.
Jacinta Wanjiru pia ni mwanafuzi wa kike
anayeishi na kusomea Korogocho katika mtaa duni.
Maisha katika mtaa huu ni magumu Zaidi;ukosefu
wa maji safi,vyoo na hata kupata pesa za kujikimu kimaisha ni changamoto.
Yeye kama wenzake alipata hedhi kwa mara ya
kwanza mwezi uliopita na hakuwa na habari ya kutosha jinsi ya kujistiri wakati
huo.
Anasema vijana shuleni walimchezea
alipojipata amevuja damu wakati wa hedhi.Anasema alipata pia changamoto ya
kupata sodo kwani wazazi wake hawakuwa na uwezo.Ilibidi abaki nyumbani hadi
siku ya tatu huku akidanganya mwalimu wake kuwa alikuwa anauguwa.
Ilibidi afanye urafiki na kijana wa jirani
ambaye alimsaidia kupata hela ya kununua sodo.
Wasichana wengi hapa hufanya mapenzi na
wanaume ili wapate pesa za kununua sodo.”usipofanya hivyo utaumia wewe mwenyewe
,anafichua Wanjiru.
Anasema wazazi pia wanajukumu lakuelimisha
wasichana changamoto za hedhi na kuwasaidia katika vipindi hivyo.
Wazazi wengi huwaachia majukumu ya mafunzo
ya kijamii waalimu lakini si vema.wanapaswa watusaidie pia ,Wanjiru anasema.
Nchi zinazoendelea zina sababu ya
kuelimisha watu umuhimu wa usafi na utumiaji wa vifaa vya hedhi vilivyokanguliwa
viwango vyake na kukubalika kama kamili kutumiwa.
Mataifa ya Afrika yametilia mkaso elimu ya
hedhi na pia gharama yake ,yaani bei ya sodo.
Bali
na hayo ni wachache hasa sehemu za nashambani walio na uwezo wa kugharamia sodo
kulingana na ukosefu wa hela.
Baadhi ya
wasichana kama Muthoni na pia akina mama
hutumia matope ,magada ya ndizi au hata matabara wakati wa hedi . vifaa wanavyotumia
vipindi vya hedhi huwa havistahili kutumiwa na vina madhara yake
Hali hii
imepelekea serikali na wadau kutafuta mbinu ya kupata sodo kwa bei nafuu na
kupeleka shuleni bila malipo.
Wasichana
wanapewa sodo kila mwezi bila malipo na kufunzwa jinsi ya kudumisha usafi
wakati wa hedhi.
Itakuwa ni vema
endapo serikali za mashinani zitatilia maanani swala hili kuhakikisha kila
msichana hasa wale walioko shuleni wamebahatika na mchango was ono na elimu ya
hedhi kupelekwa kote nchini ili kutatua tisho na aibu inayotokana na hedhi.
Vikopo
vya hedhi na jinsi ya kutumia
Zaidi ya hayo,
kuna vikopo vya hedhi ambavyo vimetolewa na vinaweza kutumika kwa muda mrefu
bora.Ingawa vikopo hivi vina bei ya juu vinadumu kwa muda mrefu na havivuji
hivyo basi kuondoa hofu ya aibu kwa wanaovitumia.
Linalo hitajika
ni kuosha punde tu baada ya matumizi.
Takwimu
zinakadilia kuwa asilimia 65 ya wnawake wanatumia sodo zakujitengenezea wenyewe
huku asilimia 42 ya wasichana walioko shuleni wakisema hawajawahi tumia sodo.
Asili mia 25 ya
akina mama hutumia bidhaa za kienyeji wengi walikwa mashambani.
Zamani ilikuwa
mwiko kuzungumzia maswala ya hedhi lakini mambo yamebadilika .Tuungane
kuwasaidie wasichana kuboresha elimu na maisha yao kwa kuongea kuhusu hedhi
bila uoga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni