Alhamisi, 30 Mei 2019

Tobacco day 2019 -Tumbaku



Maadhimisho ya siku ya kimataifa duniani ya kutovuta tumbaku yatafanyika kesho, Ijumaa.
Shughuli hii hufanyika kila mwaka ,lengo likiwa kuwatahadharisha watu adhari za ufutaji au utumiaji wa tumbaku kwa afya ya watu.
Mwaka huu kauli mbinu ikiangazia matumizi ya tumbaku na adhari zake kwa mapafu ya mwanadamu,”Usikubali tumbaku ichukue pumzi yako
Shirika la afya ulimwenguni, WHO inakadilia kuwa zaidi ya asilimia 40 ya vifo vihusianavyo na utumiaji wa tumbaku ni kama vile magonjwa ya saratani, magonjwa sugu ya njia ya hewa na Kifua Kikuu.WHO inataka serikali na wadau wana jukumu la kuhakikisha hatua za kulinda watu dhidi ya tumbako zimeongezwa.
Mkurugenzi WHO,Daktari Tedros Ghebreyesus  amenukuliwa akisema kuwa,kila mwaka watu wapatao millioni  nane hufariki kutokana na matumizi ya tumbako.
Zaidi ya hayo,mamilioni ya watu duniani wanaishi na magonjwa  yanayosababishwa  na madhara ya utumiaji tumbaku.
Anasema Dkt Ghebreyesus kuwa kwa mtu kuishi maisha marefu na kuwa na mapafu yenye afya ni sharti ajiepushe na tabia za kutumia tumbaku.
Watu wengi huadhirika na matumizi ya tumbaku hasa marafiki ,jirani au jamii inayokaa pamoja na watu au mtu anayetumia tumbaku.
Kulingana na wataalamu wa afya anayeadhirika Zaidi ni yule asiyetumia lakini ako mkabara au karibu na mtumiaji.
Watoto pia wameadhiriwa na hali hii.WHO inasema Zaidi ya watoto elfu sitini(60,000) wenye umri wa chini ya miaka 5 hufariki dunia kutokana na kuvuta moshi wa wavutao sigara.
Pia wanaoishi hadi kufikia utu uzima wao huwa kwenye hatari ya kupata magonjwa hatari ya mapafu na njia ya hewa.
moshi wa sigara na adhari zake
 Nukuu za WHO sinaonyesha kuwa mvuto mmoja tu wa moshi wa sigara una mamia ya kemikali za sumu ambazo huharibu mapafu pole pole hadi inafika kiwango cha hatari kinacho haribu mapafu.
Sumu iliyomo kwenye tumbaku hudhoofisha mifumo ya kusafisha makohozi na uchafu huku ikiadhiri mapafu.
Image result for tobacco act in kenya
Hali hii imechangia mtu kukosa pumzi au kuwa na ugumu wa kupumua huku njia za hewa zikipata uvimbe na kujenga kohozi na mwishowe mapavu yanaharibika kabisa.Mwishowe ni kudhoofika kwa afya na baadaye kifo mbacho kingeepukika endapo utumiaji wa sigara ungetupiliwa mbali.
 Nchini kenya hatua zimechukuliwa kuhakikisha kuwa watu wameelimishwa kuhusu madhara ya tumbaku.
Kwenye ofisi za umma na za kibinafsi kuna vibao vinavyotua ilani kuwa ufutaji sigara au tumbaku kunadhuru afya ya mtu.Lakini hata baada ya mafufuku ya uvutaji sigara kutolewa wengi huwa hawavitilii maanani,wanapuuza bila kujali afya yao.
Suluhu
Shirika la fya duniani WHO inasisitiza haja ya serikali kutokomeza janga la tumbaku kwa kutekeleza kwa kina mkataba wa kimataifa wa kudhibiti matumzi ya tumbaku, na kuimarisha hatua dhidi ya matumizi ya tumbaku.
HIi imeafikiwa kwa kiwango Fulani nchini kenya kwani kodi za sigara zimewekwa juu zaisi
Pia maeneo yametengwa kwa wavuta sigara ili wasitangamane na wasiovuta
Kuelimisha jamii madhara ya sigara na mbinu za kujiepusha na matumizi;serikali pia imepiga hatua kuona kuwa elimu inatolewa mara kwa mara kwa jamii.
 Endapo suluhu hizi zitakuwa na mafanikio,basi ifikapo mwaka wa 2030 idadi ya wanaoadhiriwa na hali hii itapunguka kwa kiwango cha theluthi moja.






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni