Alhamisi, 16 Mei 2019

kung'atwa nyoka anti venom


Kungatwa na nyoka na adhari zake      
Jane nduku  ni mkaazi wa Kitui na ameadhirika na kuuguza majeruhi ya kungatwa na nyoka mwenye sumu.Anasema nyoka alimungata usiku alipokuwa amelala na ni kwa kudra zake mola ako hai leo.

Nduku ni miongoni mwa wakenya ambao wamejipata mashakani baada ya kungatwa na nyoka wenye sumu.
Sio wengi wamekuwa na baahati kama nduku kwani wengi hufariki hata kabla ya kufika hospitalini.

Pia kuna changamoto za kupata dawa ya kutibu hali hii katika hospitali nyingi hasa za mashinani.
Image result for anti snake venom
Kulingana na shirika la afya duniani, bara la Afrika na Asia 
ni moja wapo wa bara ambazo zimeadhirika Zaidi.Huku juhudi za kutafuta mbinu na tafiti za kutafuta kinga zikiendelea.


Muadhiriwa anapofika hospitalini hulazimika kueleza au kupeleka nyoka aliyemungata ili kupata tiba ya anti venom jambo ambalo si rahisi mgonjwa aliye na maumivu ,majeraha na anayevunja damu kukubuka kupereka nyoka.
Dawa pia zafaa kufanyiwa majaribio ili kuhakikisaha kuwa kila nyoka ana tiba yake.
Shirika la afya duniani inasema Zaidi ya watu elfu 138,000 huku 185,000 wakiachwa na majeraha makali ya kungatwa na nyoka.
Nyoka wa sumu hupatikana sana barani Afrika na Asia sehemu za joto kwa wingi.
Watu wanaoadhirika sana na kungatwa na nyoka ni wale wanaishi mashambani.Wanajipata wamekutana na nyoka katika shughuli zao za kila siku au nyoka wanaingia nyumbani mwao wakati wa kiangazi wkitafuta maji.
Kujiepusha na kukumbana na nyoka ni vema kuacha maji nje ya nyumba na pia kuwa waangalifu watua wanapoenda shambani endapo hii wkati mwingine ni ngumu kufanyika kwani nyoka anajificha na kuvamia kwa ghafla.Nchini Kenya ,maeneo ya Kitui, baringo ,pokot Magharibi na Turkana yameathirika zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni