COVID-19
Kenya waalimu
Huku chanjo dhidi ya Covid -19 ikitarajiwa
kutolea baadaye mwezi wa Februari,serikali imesema kuwa Walimu watapewa nafasi ya kwanza,miongoni mwa wafanyikazi
wengine walioko kwenye hatari ya kupata maabukizi ya Covid-19.
Hata hivyo,Wizara ya Afya inasema kuwa wanafunzi
hawamo kwenye mpango wa chanjo kwa sababu majaribio ya chanjo ya kliniki kwa
watoto bado hayajakamilika.
Awamu ya kwanza ya Zoezi la chanjo
litalenga watoa huduma muhimu, pamoja na wafanyikazi wa afya na vikosi vya
usalama.
Wazee na wale walio magonjwa mengine kama
kisukali,shinikizo la damu,figo na mengine watapewa kipaumbele .
Tangazo hilo lilitolewa na Katibu wakudumu katika
Wizara ya Afya Dkt Mercy Mwangangi Jumatano.
Alisema Kenya imepata dozi zake za kwanza
milioni 24 za chanjo kupitia Covax, mpango wa nchi 189 ambao unakusudia kupata
na kusambaza chanjo za Covid-19 kwa vikundi vilivyo hatarini ya maabukizi.
Alisema Kenya hadi sasa imejaribu zaidi ya
watu milioni moja dhidi ya Covid-19 na imeweka
mikakadi madhubuti kuzuia maambukizi ya coronavirus baada ya shule kufunguliwa Jumatatu
wiki hii,nchini.
Hapo awali,Bi Henrietta Fore Mkurugenzi wa
Shirika la umoja wa mataifa la watoto(UNICEF) alitaka selikali pia kutoa chanjo
kwa wanafunzi na waalimu,ili kuzuia madhara kwenye sekta ya elimu.
Hata hivyo alisema uamuzi wa hatua hiyo uko
mikononi mwa serikali husika.
Takwimu zinaonyesha kuwa watoto hubaki bila
dalili. Watoto kati ya miaka mitano na 19 hawako katika hatari kubwa ya
kuambukizwa Covid-19 lakini wanaweza kubeba virusi na wanaweza kuambukiza watu
wazima.
Kenya ina zaidi ya walimu 340,000
wanaofanya kazi chini ya Tume ya Huduma ya Walimu (TSC) na karibu wengine
160,000 wanaofanya kazi katika shule za kibinafsi.
Kumekuwa na hofu ya kuambukizwa kwa wingi
mashuleni baada ya kufunguliwa Jumatatu baada ya fungwa tangu Machi mwaka jana.
kulikuwa na visa kadhaa vya walimu ambao
walipata virusi hivyo na vifo vingine viliripotiwa,baadaya taasisi zilipofunguliwa
mnamo Oktoba,mwaka jana.
Kulingana na Dkt. Mwangangi Kenya
itategemea sana chanjo ya AstraZeneca kwa sababu ya kubadilika kwake kwa mifumo
ya sasa ya kuhifadhi baridi nchini.
Pfizer na Moderna pia wameanzisha chanjo za
Covid-19 lakini hizo zinahitaji kuhifadhiwa kwa joto la chini sana.Alitangaza kuwa wizara yake, pia itasambaza
programu ya simu ya rununu,ijulikanayo kama M-Dharura ili kupata taarifa na pia
kutoa habari kuhusu kesi za Covid-19.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni