Chajo ya Oxford-AstraZeneca
Huku chanjo dhidi ya virusi ya Corona yaani COVID -19 ikianza kutolewa kwenye mataifa yalioendelea,kenya inatarajiwa kuanza kutoa chanjo hiyo mwanzoni mwa januari mwaka huu.
Hapo awali,
Wizara Ya Afya ilitoa taarifa kuwa Shehena ya chanjo ya Covid-19 inatarajiwa
nchini Kenya mwezi huu, huku walengwa wa kwanza wakiwa vikundi vilivyo katika
hatari kubwa ya kuambukizwa virusi.
Isitoshe,Kenya imeagiza dozi milioni 24 za chanjo ya Chuo Kikuu cha Oxford-AstraZeneca ambayo ni ya bei nafuu na inahifadhiwa kwa urahisi.
Baadhi ya
walio kwenye hatari ya maambukizi ya virusi vya Corona ni pamoja na Wafanyikazi
wa afya, maafisa wa polisi, wazee na walimu .
Chanjo ya
Chuo Kikuu cha Oxford-AstraZeneca itatolewa katika robo ya kwanza ya mwaka huu.
Kulingana
na Wizara ya Afya watu ambao wanaokuwa kwenye mukushanyiko wa umati na wale
walioadhirika na magonjwa mengine ya kiafya watakuwa wa kwanza kupewa chanjo
dhidi ya coronavirus.
Inakadiriwa
asilimia 20 ya idadi ya watu nchini watapokea chanjo katika awamu ya kwanza.
Zaidi ya
hayo, serikali inachunguza njia za kushirikiana na mashirika mengine kama yale ya
Wachina ambayo yameunda vidonda vya Covid-19 na wengine.
Kwa sasa,
madawa na Moderna inayotolewa kwa matumizi ya dharula.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni