Jumatano, 6 Januari 2021

WHO -China Ujumbe

 

China yawazuia wataalam wa afya wa WHO kuingia nchini humo.

Shirika la Afya Ulimwenguni(WHO) limekemea hatua ya Uchina,kuwazuia kuingia nchini humo kwa timu inayochunguza asili ya janga la coronavirus.

Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Dkt.Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema wanasayansi wawili wa timu ya Umoja wa Mataifa tayari walikuwa wameondoka nchi zao kuelekea Wuhan, walipoambiwa kuwa maafisa wa China hawajapitisha idhini zinazohitajika kuingia nchini.

 Dkt.Ghebreyesus alisema alikuwa akiwasiliana na Uchina kabla ya ziara ya wawili hao kuanza, na kila kitu kilikuwa kamili baina yake na China.

Akihutubia wanahabari kutoka makao makuu ya shirika hilo,huko geneva,uswizi,Dkt.Ghebreyesus alisema,"Nimesikitishwa sana na habari hii."

 "Nimekuwa nikiwasiliana na maafisa wakuu wa China na nimeelezea kuwa ujumbe huu ni kipaumbele kwa WHO na timu ya kimataifa."

 azimio la kutaka uchunguzi huru.

Tedros alisisitiza kuwa madhumuni ya mkutano huo ilikuwa kutaadhmini hali hilivyo kuwa na kiini cha mripuko wa coronavirusi,kama ilivyopi asimiwa na mataifa mia moja ,mei mwaka uliopita.

 Hapo awali, uchina ilikuwa imewahakikishia kuwa ilikua kwenye harakati za kujiadaa kupokea ujumbe huo.

Maafisa wa WHO kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya mazungumzo na Beijing kuruhusu timu ya wanasayansi wake kupata fursa kuchunguza asili ya virusi – vilivyo gunduliwa kwanza huko Wuhan mnamo Desemba 2019.

 Katika mkutano na waandishi wa habari Jumatano, msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje ya China, Hua Chunying, alisema Uchina imekuwa na mtazamo wazi, uhuru na uwajibikaji kila wakati katika harakati za kutafuta asili ya coronavirusi.

 Hua alisema,hapo awali nchi yake,ilikuwa imekaribisha wataalam wa WHO nchini na akasema kuwa timu ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa na wataalam wa China wakuwa na ushirikiano wa mara kwa mara.

 Alisema,ili kuhakikisha kuwa kikundi cha wataalam wa kimataifa kinachokuja China kinaweza kufanya kazi vizuri, inahitajika kutimiza taratibu zinazohitajika na kufanya mipango maalum inayofaa.

Beijing imekuwa ikiishutumiwa jinsi inavyochukulia swala hili hasa katika kuchunguza kiini za maambukizi ya virusi vya COVID 19.

Hii imepelekea uhusiano wake na marekani kuzorota.

Rais wa Merika Donald Trump amekuwa akilaumu China mara kwa mara kwa kuregea kwake kukabili janga hili.

Kufuatia uhusiano mbaya kati ya nchi hizi mbili,Marekani itasitisha uhusiano wake na WHO, ikisema kuwa Uchina haikuripoti habari sahihi iliyokuwa nayo juu ya coronavirus na ilishinikiza WHO "kupotosha ulimwengu."

Marekani imetaka uwazi katika shughuli za WHO nchini China.

 Pia inadaiwa kuwa maafisa wa China walitoa habari za kupotosha kuhusu idadi ya kesi wakati wa hatua za mwanzo za mlipuko wa Virusi ya Corona.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni