Kongamano la saratani
Mkutano kuhusu ugonjwa hatari wa saratani umeanza hii leo mjini Windhoek,Namibia.
Mkutano huu hulifunguliwa na rais Hifikepunye Pohamba huku akisema ni muhimu kwa umoja wa Afrika na pia mataifa tofauti Afrika kutafuta binu na mikakati ya kuangamisha saratani.
Mada ya mkutano huu ni kuendelea na mikakati ya kutambua na kutibu saratani ya shingo ya uzazi yaani cervical cancer imekuwa donda ndungu kwa wanawake .Saratani ya matiti pia inaenea kwa haraka barani Afrika.
Malengo mengine ni kutafuta binu ya kuzuia kenea kwa saratani ya shingo ya uzazi ifikapo mwaka wa 2030.
Rais Pohamba alilalama kuwa zaidi ya watu millioni 28 hufariki kutokana na maradhi ya saratani kila mwaka jambo ambalo nila kuhuzunisha.
Mkewe Rais wa kenya Margaret Kenyatta ni miongoni mwa wake wa marais wanane wanaohudhuria kongamano hii ya siku tatu.
Bi Kenyatta amekuwa mstari wa kwanza kama mama wa taifa kuangamizia na kupigia debe maswala ya afya na akina mama.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni