Ijumaa, 18 Julai 2014

Joep Lange


Jeop Lange mtafiti wa tiba ya makali ya ukimwi aaga dunia.

-Sekta ya afya na tiba, na dunia kwa jumla inaomboleza kifo za Jeop Lange, mtafiti wa tiba ya makali ya ukimwi dunia.




Mtafiti stadi wa afya duniani ni miongoni mwa  abiria waliofariki baada ya ndege ya Malaysia,waliokuwa wakisafiria, kuanguka huko Ukraine.

Joep Lange alikuwa mwanasayansi mashuhuri ambaye pamoja na watafiti wenzake
lifanya juu chini kutafuta tiba ya ugonjwa wa ukimwi duniani. 

Lange Pia ni raia wa Uhoranzi.

Lange alikuwa profesa na mkurugenzi kuu wa kitengo cha afya na utabibu katika chuo kikuu cha Amsterdam,uholanzi.Amekuwa katika mstari wa mbele kutafuta tiba ya makali  ya ukimwi kwa miaka thelathini.Mkewe pia alifariki kwenye ajari hiyo.

Mtafiti kutoka Amerika,Dkt Rick Elion alimtaja Lange kama mtu mwenye roho ya dhahabu,mkarimu na mwenye bidii kama ya mchwa.

Inakisiwa baadhi ya  abiria kwenye ndege hiyo  ya Malaysia  walikuwa wataalamu wa afya na watafiti  wa maswala ya ukimwi waliokuwa safarini   kuelekea Melbourne , Australia kuhudhuria mkutano wa  kimataifa kuhusu ukimwi utakaoanza Jumapili.







Watu 298 waliokuwa katika ndege hiyo ya shirika la Malaysia iliyokuwa ikisafiri kutoka Amsterdam kuelekea Kualar Lumpur wamefariki ,huku taarifa zikionyesha kuwa  raia wa Uhoranzi kuwa wengi.

Kifo cha  Lange ni pingo kwenye rubaa za kitaifa na sekta ya afya duniani. Husuni na simanzi zimetanda kote.

Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinaonyesha upungufu wa idadi ya Maambukizi ya  ukimwi.

Mola amlaze Lange na wote walifariki kwenye ajari hiyo pema peponi.

....
Mkutano wa ukimwi
Mkutano wa kimataifa kuhusu ukimwi unatarajiwa kuanza jumapili mjini Melbourne, Australia.watalaamu wa afya na watafiti wa makali ya ukimwi duniani kote wamealikwa.

Habari njema ni kuwa maambukizi ya ukimwi imepunguka kote ulimwenguni .

Shirika la Ukimwi duniani linabaini   kuwa idadi ya vifo vinavyosababishwa na ukimwi duniani vimepungua kwa kasi mwaka 2013 sawa na asilimia 11.8% ndani ya mwaka mmoja.

Zaidi ya hayo UNAIDS inasema kwamba lengo la pambano hilo mwaka huu ni kusisitiza kuwahudumia ambao wamesahauliwa kama vile wafungwa, wafanyabiashara ya ngono, wanaofanya mapenzi ya jinsia moja na kadhalika.

Hii ni idadi ya waathiriwa wa ukimwi duniani ambayo imetolewa na taasisi ya Umoja wa Mataifa inayokabiliana na ukimwi katika ripoti ya mwaka 2013, kabla ya kikao cha Melbourne kuhusu ukimwi.

Kwa jumla mwaka 2013, takribani watu milioni 35 walikua wakiishi na virus vya ukimwi duniani, huku watu milioni 1.5 walifariki kutokana na ukimwi mwaka 2013.Mwaka huo huo wa 2013, watu milioni 2.1 duniani waliambukizwa virus vya ukimwi, huku idadi hio ikishuka mwaka 2001 kwa asilimia 38.Watoto 240.000 walizaliwa na virus vya ukimwi mwaka 2013, huku asilimia 87.7 wakiwa ni watoto kutoka katika nchi za Afrika ziliyoko kusini mwa jangwa la Sahara.

Eneo hili lilioko kusini mwa jangwa la Sahara linaendela kuathirika zaidi na ugonjwa huu wa ukimwi, likiwa na asilimia 70.6 ya watu walioathirika duniani. Ugonjwa huu unawaathiri kwa sehemu kubwa wanawake ambao wamefikiya sasa asilimia 58 ya walioambukizwa katika eneo hili la kusini mwa jangwa la sahara.

Ugonjwa wa kifua kikuu ni moja ya sababu kuu ya vifo kwa watu wanaoathika na virus vya ukimwi.Dola bilioni 19.1 ziliwekezwa mwaka 2013 kwa kupambana na ugonjwa wa ukimwi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni