Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2011

Ovarian Cancer(saratani ya mfuko wa mayai)

Hii leo nitaandika zaidi na kuwaelimisha kuhusu saratani ya mfuko wa mayai yaani ovarian cancer. Je wajua kuhusu Saratani ya kifuko cha mayai ya uzazi ? Mwanamke ana vifuko viwili vidogo vilivyo kila upande wa   mfuko wake wa uzazi.Kwa mujibu wa tafiti,ni vigumu kuitambua saratani hii. Hivyo basi ni muhimu kutembelea daktari kila mwaka kwa uchukuzi wa kina.Dalili zake huonekana ugonjwa ukiwa umeenea mno. Walio   kwenye hatari ya kupata saratani hii ni v      -Wanawake wenye zaidi ya umri wa miaka 50 wako hatarini ya kuambikizwa ugonjwa huu. v      mwanamke tasa v      Ikiwa umewahi kuwa na saratani ya matiti v      Ikiwa kuna mtu wa familia ambaye amewahi kuugua ugonjwa huu. v      Kupata hedhi katika umri mdogo Hata hivyo, kama saratani yingine,inapogunduliwa mapema mtu anaweza kupona. Ni muhimu kula vyakula kama mboga, matunda ambavyo vinafahamika kupunguza hatari ya s...

wasifu wa Mama Wangari Maathai

Picha
Taarifa ya   kifo cha aliyekuwa mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel, Wangari Maathai, imepokelewa kwa huzuni. Watu wa tabaka mbalimbali wamenukuliwa wakitoa rambi rambi zao, huku wakimumiminia sifa chungu nzima . Ni wazi kuwa   kifo chake Maathai si pigo tu kwa wanaharaki wa mazingira nchini Kenya lakini kwa ulimwengu wote. Prof.Maathai akipanda mti Mama Mathaai aliaga dunia katika hospitali ya Nairobi   alikokuwa akitibiwa saratani ya mfuko wa uzazi(Ovarian Cancer) Umaarufu wa Mathaai ulitokana na ari yake ya Mazingira.Alikuwa kwenye mstari wa mbele kuelimisha wakenya na ulimwengu kwa ujumla umuhimu wa   kuhifadhi na kutunza mazingira. Pia alipigia debe jitihada za kutimiza lengo la milenia la kutunza na kulinda mazingira.  Karne tatu zilizopita, Maathai aliasisi shirika la mazingira nchini Kenya, Kenya Green Belt Movement. Alikuwa mama shujaa na pia   mkakamavu ambaye hakutishwa na yeyote.Alifanya kazi yake aliyoienzi kwa dhati. Wanyakuzi...

Prof.Wangari Mathaai

Picha
 Kifo cha shujaa wa Mazingira   Mama Wangari Maathai  Hongera Mama Mathaai kwa kazi yako nzuri ulioifanya.  Chemichemi za maji ukahakikisha zimelindwa. Shughuli ya ukataji miti misituni ukapigwa marufuku. Upanzi wa bangi Mlima Kenya ukakoma. Majereha ukapata kwa ajili ya mangizira. Katunukiwa Tuzo ya Nobeli kwa ukakamavu wako Hongera! Hongera! Mama Mathaai Mola akuweke pema peponi.

Polio(ugonjwa wa kupooza)

Serikali ya Kenya imezindua kampeini ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa upooza Septemba 23, 2011.Kampeni hiyo inalenga maeneo ambaye dalili ya ugonjwa huu imeanza onekana, kama vile Migori, Homa-Bay, Kisii, Nyamira na Transmara. .watoto walio chini ya miaka mitano watachanjwa. Hivi majuzi waziri wa Afya ya Umma, Beth Mugo alitangaza kuwa Kenya inakabiliwa na hatari   ya mkurupuko wa ugonjwa wa kupooza baada ya kijana mwenye umri wa miaka mitatu kupatikana virusi ya polio katika Wilaya ya Rongo, Mkoani Nyanza. Ugonjwa wa polio husababiswa na virusi na kwa hivyo ni vingumu kutibiwa, punde tu mtu anapoambukizwa. Mwongozo wa shirika la Afya duniani(WHO) unabainisha kuwa ili kudhibiti mzunguko wa virusi pori vya ugonjwa wa kupooza,ni muhimu kutoa chanjo za zaidi kwa njia ya kampeni kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 angalau kwa awamu mbili. Chanjo hii inatolewa na wataalam wa afya kwa njia ya matone kinywani kwa watoto wote, bila kujali kama walipata chanjo hiyo hapo awal...

saratani ya shingo ya uzazi (Cervical cancer)

Picha
  Ikiwa kuna ugonjwa ambao unasababisha vifo vya   wanawake wengi hapa nchi na duniani kwa ujumla, basi si mwingine ila ule wa saratani. Kuna aina kadhaa za saratani zinazo waathiri wanawake. Saratani ya shingo ya kizazi ni baadhi tu ya aina kadhaa za ugonjwa huu hatari. Mama Hannah Mwendeo* anafahamu vyema jinsi ugonjwa huu umekuwa tishio kwa wanawake wengi. "kabla madaktari kugundua maradhi niliyokuwa nikiugua, nilikuwa nina maumivu sana.Pia nilikuwa napata hedhi kila wakati,lakini si kufahamu kwamba nilikuwa tayari naugua saratani ya shingo ya uzazi. Kwa bahati nzuri.watalamu wa afya walitambua ni saratani ya shingo ya uzazi na papo hapo alianza matibabu". Kwa sasa amepona na anatowa wito kwa aki mama wenzake wajipimishe mapema ili kuepana na hatari au tishio la ugonjwa huu. Takwimu zilizotolewa na   shirika la afya duniani (WHO) , asilimia 3.2 ya wanawake nchini Kenya, walio kati ya miaka 18-69 hupimwa kila baada ya miaka mitatu ikilinganishwa na wanawake ...

Uterine Fibroid Embolization

Picha
Uterine Fibroid Embolization Je wajua kuwa ugonjwa wa fibroids yaani uvimbe au vivimbe   ambavyo   huwa   kwenye ukuta wa kizazi (uterus) waweza kutibiwa na mwanamke akawa hana matatizo tena kwenye uzazi wake? Kwa mujibu wa daktari, Timona Obura, ambaye ni mtaalam (Gynaecologist) katika hospitali ya Aga Khan, Hii inawezekana kutokana na tecnhologia ya kisayansi ambayo inajulikana kama Uterine Fibroid Embolization. Vivimbe hivyo vinaweza kuwa vidogo Kama ncha ya kidole au vikubwa Kama viasi .Pia vinaweza kugunduliwa, kwa kutumia tecnologia inayojulikana kama Ultrasound.   Mwanamke anaweza akawa kwenye hatari ya mimba kutoa(miscarry) kwani,uvimbe unaweza kujaa kwenye sehemu anayokaa mtoto. Ingawa kuna   aina za upashuaji zinazotumiwa kuondoa Fibroids,Daktari Obura anasisitiza kuwa Embolization ni namna maalum ambayo haihitaji upasuaji wa kawaida.Pia hamna madhara kama upasuaji wa kawaida. Hapa mwanamke au mgonjwa anaelimishwa kuhusu jinsi upasuaji unav...

Obstetric fistula

Picha
Fistula Katika baadhi ya mikoa hapa nchini Kenya, akina mama waja wazito hulazimika kutembea   mwendo   mrefu kutafuta matibabu.Baadhi yao   hulazimika kujifungua nyumbani ,jambo ambalo husababisha madhara ya kiafya. Uchungu wa muda mrefu,kutokana na ukosefu wa huduma za matibabu   au kujifungua katika mazingira yasiyofaa ni chanzo cha ugonjwa unaojulikana kama fistula. Kulingana na daktari wa afya ya uzazi katika hospitali moja hapa jijini Nairobi,Fistula ni tatizo linalotokana na jeraha wanalopata kina mama wakati wa kujifungua baada ya kupata uchungu kwa muda mrefu na pia kuwa na njia ndogo ya uzazi kiasi kwamba kichwa cha mtoto kinashindwa kupita kwa usalama wakati wa kujifungua. Hali hii humfanya mama kushindwa kujizuia wakati anapotaka kwenda haja ndogo na wakati mwingine hata kubwa bila mpangilio. Ugonjwa huu ,umehatarisha maisha ya akina mama wengi.   Wengi wao hutengwa na jamii kwani wanakuwa hawawezi kufanya lolote,na pia wanatoa harufu inayosamb...

afya ya uzazi

Picha
  Kuna haja ya kutoa elimu ya afya ya uzazi shuleni.Ili kupunguza ongezeko la Ujauzito Kwa vijana wakiwa wadogo. Kulingana na mila na tamaduni za kiafrika baadhi wa walimu na pia wazazi hawataki kuzungumzia maswala ya ngono kwa watoto. Hizi ni mila ambazo zimepitwa na wakati na ni jukumu     letu kulitilia maanani   elimu ya afya ya uzazi. Kulingana na watalamu ya afya, unaweza kutungwa mwanamke au msichana mimba   anapokaribia kupata hedhi kufanya tendo la ndoa pasipo kutumia mbinu yoyote ya kuuzuia. Hivi majuzi visa vya wasichana wa chini ya miaka kumi kutunga mimba   vimeripotiwa nchini Kenya. La kusikitisha ni kwamba wengi hawana habari kuhusu afya ya uzazi Pia waohupata   matatizo ya kujifungua kwani viungo vyao kama vile mishipa ya uzazi haijakomaa. Zaidi ya hayo,ugonjwa wa fistula unaweza ukatokea baada ya kujifungua. Kwa hivyo elimu ya afya ya uzazi ni muhimu zaidi kwa kundi hili la vijana wasichana kwa wavulana. Hivyo basi, kuna haja y...

afya ni uhai

Picha
Afya ni uhai Mazingira machafu ni chimbuko la magonjwa chungu nzima. Mamia ya watu kote duniani, huadhirika kiafya na hata kufariki kufuatia hali hii. Hivyo basi, ni jukumu la kila mtu kuhakikisha ya kwamba hali ya usafi unadumishwa kila wakati. Kwa mfano ugonjwa wa kipindupindu unahatarisha maisha ya watu wengi. Waswahili husema kuwa kuzuia ni bora kuliko kuponya.Fauka ya hayo, itakuwa ni jukumu ya kila mtu kuhakikisha anaishi katika mazingira safi,ilikuepuka magonjwa kama hayo. Kipindupindu Kipindupindu ni kuharisha papo hapo.Huu ni ugonjwa  ambao unaweza kuua ndani ya masaa kama ukiachwa bila kutibiwa. Mara tu baada ya  ugonjwa kupatikana  ni jambo la  muhimu kutafuta matibabu ya haraka. Utoaji au utumiaji wa maji safi,vyoo bora na elimu ya afya kwa umma na usafi wa mazingira,ni baadhi tuu ya  namna ya kupunguza madhara au kukabiliana na tishio la ugonjwa wa kipindupindu. Afya yako iko mikononi mwako.Kampeni ya kuosha m...