Fistula
Katika baadhi ya mikoa hapa nchini Kenya, akina mama waja wazito hulazimika kutembea mwendo mrefu kutafuta matibabu.Baadhi yao hulazimika kujifungua nyumbani ,jambo ambalo husababisha madhara ya kiafya.
Uchungu wa muda mrefu,kutokana na ukosefu wa huduma za matibabu au kujifungua katika mazingira yasiyofaa ni chanzo cha ugonjwa unaojulikana kama fistula.
Kulingana na daktari wa afya ya uzazi katika hospitali moja hapa jijini Nairobi,Fistula ni tatizo linalotokana na jeraha wanalopata kina mama wakati wa kujifungua baada ya kupata uchungu kwa muda mrefu na pia kuwa na njia ndogo ya uzazi kiasi kwamba kichwa cha mtoto kinashindwa kupita kwa usalama wakati wa kujifungua.
Hali hii humfanya mama kushindwa kujizuia wakati anapotaka kwenda haja ndogo na wakati mwingine hata kubwa bila mpangilio.
Ugonjwa huu ,umehatarisha maisha ya akina mama wengi.
Takwimu za Shirika Afya Duniani (WHO) sinadhihirisha ya kuwa zaidi ya wanawake milioni nne ulimwenguni kote wanaishi na fistula .
Daktari wanatilia mkazo haja ya wanawake wajawazito kutembelea kliniki za afya mara tu wanapotunga mimba ,ili kupata utalamu na mawaidha ya afya,hili kupunguza hatari.
Nchini Kenya kuna baadhi ya mashirika ya afya yaani mashirika yashiyo ya serikali ,yanayotoa matibabu ya bure kwa baadhi wa wanawake ambao wamejikuta kwenye lindi hili na masonokeko.
Jambo la kutia moyo ni kuwa tatizo hili linaweza kutatuliwa.Baadhi ya wanawake niliowahoji wanasema kuwa baada ya upasuwaji na watalaamu wa afya ya uzazi,walirejea katika hali zao za kawaida.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni