Ijumaa, 27 Machi 2020

America COVID- 19


Marekani yaongoza duniani kwa idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona
Chuo Kikuu cha Johns Hopkins kimetoa takwimu kuwa  watu 85,996 wameripotiwa kuambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani. 

Hivyo basi,  Marekani imekuwa nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu walioambukizwa virusi hivyo duniani.Huku idadi ya Vifo ikifika 1,195.

Idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo imeongezeka kwa zaidi ya watu elfu kumi ndani ya saa tano nchini Marekani,inasema ripoti hiyo.

 Pia Tafiti zinaonyesha  idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona imefika  542,788 na 24,361 wamefariki kwa virusi hivyo duniani.

Kwa sasa Marekani imeipita Uchina na Italia kwa visa vya Corona vilivyothibitishwa.
Hata hivyo,bado Italia inaongoza kwa vifo 8,000 huku Uchina ikifuata na idadi ya vifo 3,000 hadi sasa.

Ugonjwa wa Corona unaenea kwa kasi huku mataifa ya dunia yakijukakamua kukabiliana na hali kwa kuweka mikakati thabiti ya kukomesha maamukizi Zaidi.

Hiyo jana Kenya ilirekodi kifo cha kwanza cha mgonjwa aliyekuwa akipokea matibabu kwa muda.


Mkenya huyo wa miaka 66 alikuwa amezuru nchi ya uswatini Afrika kusini .



kifua kikuu-WHO


Kifua kikuu --mikakati yabuniwa

Dunia imeadhimisha siku ya kifua kikuu,huku idadi ya maambuziki ikizidi kuongezeka.

Hali hii imepelekea wataalamu wa afya duniani kutafuta mikakati itakayo badili hali ili kupunguza idadi ya wagonjwa na walioko kwenye hatari ya maambukizi.

Takwimu zinaonyesha kuwa robo ya watu duniani wana backeria ya kifua kifuu mwilini na wako hatarini ya maambukizi,hasa wale walio na kinga dhaifu.

Kufuatia haya,Shirika la Afya Duniani,WHO limetoa mapendekezo, kuongezwa kiwango cha matibabu ya kuzuia Kifua kikuu kati ya idadi ya watu walio katika hatari kubwa.

Mapendekezo hayo ni kama vile:kuboresha ubunifu kuzuia hali ya wagonjwa wa kifua kikuu, watu wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi na pia  wanaoishi katika mazingira yaliyojaa.

WHO inapendekeza kwamba ama majaribio ya tuberculin au interferon-gamma (IGRA) itumiwe kupima ugonjwa wa Kifua kikuu.

Upimaji wa maambukizo ya Kifua Kikuu,ingawa hauhitajiki kabla ya kuanza tiba ya kinga kwa watu wanaoishi na VVU, na watoto chini ya miaka 5.

Pia ,WHO inapendekeza mbinu fupi, jinsi ya kutumia dawa kukabili TB kwa kupunguza muda wa awali wa miezi 6 .

Kifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza unaoongoza kwa maabukizi,mllioni 10  na vifo vya takribani watu million 1.5 duniani mwaka wa 2018.

Juhudi hizi zinafanywa wakati dunia ikikabiliana na jinamizi la Virusi vya Corona huku Mkuu wa WHO Tedro Ghebreyesus akissitiza umuhimu wa kuendele na juhudi za kukabiliana na magonjwa haya yakuambukiza,ili kuokoa maisha.

Ingawa maendeleo yamepatikana kwenye malengo yaliowekwa kupunguza makali ya TB juhudi za nchi wanachama zahitajika zaidi ilikuafikia malengo ya kukomesha Tb ifikiapo mwaka wa 2030.

Kenya yajizatiti kuhakikisha wanaougua Tb wanapokea matibabu na pia lishe bora ili kuimalisha afya na idadi ya maambukizi.
Hata hiyo juhudi zaidi hasa mashinani zinahitajika.juhudi za kuelimisha umma na namna ya kupata matibabu iendelezwe kwa kina.

Mwaka jana Wizara ya Afya kenya ilizidua mwongozo na  malengo yakupunguza maambukizi ya watu 597,000  ifikapo mwaka wa 2023


 










Alhamisi, 26 Machi 2020

Kifo Corona Kenya

Kifo cha Kwanza kutokana na mambukizi ya Corona, COVID 19 cha tangazwa Kenya.


Kulingana na taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya Mutahi Kagwe,  mwadhiriwa amefariki Leo katika hospitali ya Agah Khan alipokuwa akipokea matibabu.

Idadi ya wanaougua Ugonjwa wa Corona yazidi kuongezeka, huku serikali ikitoa makataa yakutotoka nje kutoka alasiri hadi machweo kuanzia hapo kesho, Ijumaa.

Zaidi ya hayo, Kenya ina maambukizi zaidi ya watu 30.

Ijumaa, 20 Machi 2020

Dr Catherine Hamlin afariki



Daktari wa Afya ya akina mama ,Dkt Catherine Hamlin Amefariki Dunia huko Ethiopia akiwa na umri wa miaka 96.

Dkt Hamlin ni mzaliwa wa Australia na alikuja Afrika katika shughuli za kazi ya utaalamu wa afya ya wanawake.
Image result for dr catherine hamlin
Alijitolea kwa moyo wa dhati  kuwasidia akina mama hususan nchini Ethiopia kuwanusuru kutoka kwa ugojnwa wa fistula ambao humwacha mwanamke na fedheha.
Dkt  Hamlin,alikuwa mkarimu ,mwenye upendo na huruma aliye jitolea kuhakikisha mwanamke amepata matibabu yafaayo anapopatwa na hali kushindwa kudhibiti mkojo baada ya kujifungua.
Alipowasiri nchini Ehiopia hakukuwa na hospitali iliyowatibu wagonjwa wa fistula ya akina mama lakini alifanya juu chini kuhakikisha namna ya kurejesha heshima na matumaini kwa  akina mama imepatikana.
Pamoja na mumewe walifanya ubunifu wa kutafuta namna tofauti za kufanya upasuaji wa wanawake waliona fistula ,ubunifu ambao unatumiwa na wataalamu wa afya ya kina mama hadi sasa.
Fistula ni jinamizi linalowaghubika akina mama kote duniani,lakini juhudi zake za kuwanusuru kutoka utumwa wa ugonjwa huu zilifua dafu.
Marehemu atakumbukwa kwa uanzilishi wa hospitali ya Fistula, Addis Ababa kwa ushirikiano na mumewe mwaka wa 1974.
Image result for dr catherine hamlin
Hata baada ya kuachwa mjane na mumewe aliyefariki mwaka wa 1993,dkt Catherine hakukomesha juhudi zake hapo.
Alijikasa kisabuni mpaka jihudi zake zikatabuliwa kote duniani.
Alitunukiwa zawadi nchini Ethiopia na pia nje ya nchi.

Fistula ni ugonjwa ambao husababisha shimo kubwa kati ya njia ya uzazi na njia ya mkojo unatokana na mama kuwa na uchungu wa kujifungua kwa muda mrefu bila kushughulikiwa kimatibabu.

Kwa mujibu wa Shirika la Ulimwengu la idadi ya watu, mara nyingi ugonjwa huu huwapata wanawake na wasichana kutoka nchi zilizobaki nyuma kimaendeleo na waotoka  jamii maskini kabisa.
Wanaopata fistula mara kwa mara wanakubwa na unyanyapaa mkubwa kwa jamii.
Image result for dr catherine hamlinLicha ya kutaka kutafuta matibabu,wao kukosa uwezo wakupata hela ili kwenda hospitalini na kuishi na hali ya kudharauliwa na pia kutengwa na jamii.
Ni haki ya kila mtu kupokea matibabu ,anapopata hali hii.

Pia ni jukuma la mama na wasichana kuhakikisha wanafuata maagizo ya wauguzi wanapo kuwa na uja uzito ili kuepuka kuwa madhara wakati wa kujifungua.
Isitoshe,tatizo la fistula linaweza kukomeshwa endapo wasichana wa umri mdogo wataepuka kupata mimba za mapema ,mila potovu za ukeketaji na pia kupata huduma za afya mapema wanapopata uja uzito.
Mwaka wa 2018 takwimu zinaonyesha kuwa wanawake millioni 2 waliadhiriwa na Fistula katika Bara la Afrika.
Dkt Catherine alitajwa kama mama aliyekuwa na wasichana 35,000 na wakfu wake alifanya upasuaji wa akina mama na wasichana 60,000.
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani,,WHO Dkt Tedro Ghebreyesus ambaye pia alimfahamu Dkt Catherine wakati akitumika kama waziri wa Afya nchini Ethiopia  alimtaja marehemu kama mtu Mkarimu ,mwenye utu na akasema juhudi zake kitaendelezwa na waliobaki.
Mwanamke Ngangari,Marehemu Catherine Mola ailaze roho yake pema peponi..


Alhamisi, 19 Machi 2020

Aurlus Mabele :COVID 19

Image result for aurlus mabele pix
Ugonjwa wa COVID-19 umepokonya dunia mwanamziki mashuhuri kutoka nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo(DRC).

Papa Aurlus Mabele alifariki hiyo jana baada ya kuambukizwa virusi vya Corona .

Hii ni kwa mujibu was taarifa zilizotolewa na familia ya mwenda zake.

Mwanaye Liza Monet alitangaza kifo cha babake kupitia kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na Instagram alisema" baba amefariki asubuhi ya Leo kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.Alikuwa mwanamziki mashuhuri wa mitindo ya Soukouss ambaye watu was Congo wamempoteza, nakupenda baba Aurlus Mabele."

Hakika ugonjwa wa Corona ni tisho kubwa ambalo linahitaji hatua kali kulikabili.

Mabele ni miongoni mwa watu washuhuri ambao wamepatikana na ugonjwa huu, ingawa wengi wao wamepata au wanaendelea kupata matibabu.

Hatua kali zinahitajika hasa katika Bara la Afrika ambapo mambukizi yanaongezea kila kuchao.
.
Mkuu wa WHO Tedros ametoa changamoto kwa Afrika huku akisema kuwa ugonjwa hunaenea kwa kasi.

Wakati huo huo WHO iko katika harakati ya kutafiti chanjo ya majaribio ya ugonjwa wa Corona ambao kwa hakika unaogovya.

Huku dunia ikihofia maafa zaidi,ni matumaini ya kila mmoja Kuwa shuluhu la dharura litapatikana kukabiliana na janga hili,  ili kuepuka maafa zaidi.

Kampeni pia zinahitajika ili kuwahamasisha wananchi madhara yake na jinsi ya kuepuka mambukizi.

WHO chanjo dhidi ya Coronavirusi


Shirika la Afya Duniani,WHO limezidua rasmi  chanjo  ya majaribio dhidi ya COVID – 19 .
Hatua hii ni kufuatia ongezeko ya maambukizi na vifo duniani.
 Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dkt. Tedros Ghebreyesus amewapongeza watafiti kote duniani ambao wamejumuika  pamoja ili kutaathimini majaribio haya.
Dkt Ghebreyesus akisema hatua hii ni  mafanikio makubwa na kuwa kwa sasa wataalamu wa afya yanafanywa kila juhudi kuhakikisha kuwa tiba yeyote ambayo itasaidia kuokoa maisha imepatikana
Amesema hata kama kuwa uwezekano wa kutofata mafanisi kutokana na majaribio madogomadogo na njia mbalimbali,tiba ya haraka inahitajika na kuna uhakika itapatikana .

Zaidi ya hayo,Dkt. Ghebreyesus,ameongeza kuwa WHO na washirika wake wanaandaa utafiti katika nchi mbalimbali ambapo baadhi ya dawa hizi hazijafanyiwa majaribio zitalinganishwa .
Amesema  utafiti huo mkubwa unaandaliwa kwa minajili ya kukusanya takwimu zinazohitajika ili kubainisha ni matibabu yapi yanafayakazi zaidi.
Licha ya hayo, nchi kadhaa tayari zimethibitisha kwamba zitashiriki utafiti huo wa  Mshikamano wa majaribio.
Nchi hizo ni kama vile, Argentina, Bahrain, Canada, Ufaransa, Iran, Norway, Afrika Kusini, Hispania, Uswisi na Thailand.
Kuna matumaini kuwa nchi zingine ulimwenguni zitajiunga ili kuhakikisha jawabu au tiba ya COVID -19 imepatikana.Jambo ambalo WHO imelichangamkiakwani linatia moyo

 Dkt. Tedros anasema kuwa hatua za mshikamano dhidi ya COVID-19 kumepelekea mchango wa zaidi ya dola milioni 43 kutoka kwa watu zaidi ya 173,000 na mashirika hisani siku chache tu tangu ulipozinduliwa.
FIFA ni baadhi ya mashirika ambayo yamechangia mfuko huu kwa kutoa dola milioni 10.
 Utafiti huo umepewa jina la “Majaribio ya mshikamano”.
Amesisitiza kwamba virusi hivi ni tishio kubwa lakini kwa pamoja litakabiliwa.Isitoshe, WHO imesema kuna hofu jinsi Bara la Afrika linavyochukulia janga hili.
Hapo awali takwimu zilionyesha maambukizi yalikuwa kiwango za chini barani Afrika lakini mambo yamebadilika kwa kasi huku idadi ya maambykizi ya kuongezeka.
Ametaka serikali za Afrika kuchukua janga hili kwa dharula ili kulikabili.
Taharuki imetanda nchi DRC baada ya visa 600 kuripotiwa.
serikali ya Congo imejitahidi kukabiliana na hali hii










Jumanne, 17 Machi 2020

COVID -19 Tanzania

Kisa cha kwanza  cha virusi vya corona kimethibitisha  Arusha,Tanzania
Inasemakana kuwa mgonjwa aliwasiri nchini kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kirimanjaro Mwezi wa Machi,15 mwaka huu.
Mgonjwa huyu ni mwanamke raia wa Tanzania aliye na umri wa miaka 46.
Aliwasiri kutoka Ubelgiji kwa ndege ya shirika la Rwanda
ambaye aliwasiri aliyetangazwa ni mwanamke wa miaka 46 raia wa Tanzania, ambaye aliwasili kutoka Ubelgiji kwa ndege ya shirika la Rwanda.
Mtanzania huyo ambaye kwa sasa anapokea matibabu kwenye hospitali ta Rufaa ya Mt Meru Arusha,alitembelea nchi tofauti katika ziara yake huko Uraya.
Alizuru Denmark,Sweden na Ubelgiji na kurejea nchini ,ingawa maabukizi ya Corona hayakuguduliwa alipowasiri nchini Tanzania.
Baada ya muda,alianza kujihisi vibaya na kwenda hospitalini ambapo sampuli ilichukuliwa  na baadaye ikapelekwa kwa maabara ya kitaifa jiji Dar es salaam kwa uchunguzi.
Kulinga na Waziri wa Afya Tanzania Ummy Mwalimu vipimo vya maabara virithibitisha kuwa mgonjwa huyo ana maambukizi ya virusi vya COVID-19 na kwa sasa anaendelea kupokea matibabu.
Waziri amesema kuwa serikali ya Tanzania imechukua hatua mwafaka kuhakikisha kuwa ugonjwa huu umekabiliwa.
"Vipimo vya maabara vimethibitisha kuwa mtu huyo ana maambukizi ya ugonjwa wa corona, covid -19, Mgonjwa anaendelea vizuri na matibabu."Waziri Ummy ameongeza kusema," Serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha kwamba ugonjwa huu unathibitiwa ili usisambae nchini.



Jumapili, 15 Machi 2020

Coronavirusi Ongata Rongai

Wakenya wamepokea tangazo  la mlipuko was virusi Corona cha Kwanza mtaani Ongata Rongai, Jimbo la Kajiado kwa hofu .

Kufuatia hali hii Wakenya wengi hasa wa Ongata Rongai wamebakia nyumbani hii wikendi  wakihofia maambukizi.

Maadhi ya shule na pia vyuo vikuu vimetoa taarifa kuwataka wanafunzi kubaki nyumbani, hadi Hali iwe sawa.

Jumapili kama kawaida kanisa huwa zimefurika lakini Hali imekuwa tofauti.
Wengi wameamua kufanya maombi nyumbani yote haya yakiwa kuepuka maambukizi ya virusi vya Covid 19.

Ugonjwa huu uenea kwa kasi kwenye mataifa tofauti ulimwenguni.

Ijumaa, 13 Machi 2020

Corona Virusi Kenya


Kenya yathibithisha kisa cha kwanza Corona siku moja baada ya Shirika la Afya Duniani kutangaza mlipuko huu kama janga la kimataifa.

Hii imetangazwa na Waziri wa Afya Mutahi Kagwe.

Waziri alisema virusi hivyo vilitibitishwa kwa mwafunzi wa kike,mkenya ambaye alisafiri kutoka marekani kupitia Uingereza.

hata hivyo mgonjwa huyo yuko katika hali nzuri ingawa atatibitiwa hadi pale hali yake ya afya itathibitiwa kikamilifu.

  • ·         Waziri amesema ni jukumu ya kila mtu kuchukua tahadhari ilikuepuka maambukizi
  • ·         Kunawa mikono mara kwa mara.
  • ·         Kutokaribiana sana na mtu mwingine ambaye anakohoa ama kupiga chafya - simama umbali wa mita moja
  • ·         Watu wanaokohoa ama kupiga chafya wasalie majumbani mwao ama kutojichanganya na makundi
  • ·         ametakiwa kusalia nyumbani.
  • ·          marufuku yotolewa kwa mikutano ya aina yote ikiwemo ile ya umma kama vile ya kidini, michezo, na wanaotaka kwenda ya watu
  • ·         Hakikisha kwamba unaziba pua na mdomo unapokohoa kwa kutumia kitambaa ama tishu.
  • ·         Mtu anayehisi joto ama tatizo la kupumua makanisani na msikitini watalazimika kuosha mikono na sabuni kabla ya kuingia katika sehemu hizo.
  • ·         Michezo yote ya shule imepigwa marufuku ingawa shule zote zitasalia wazi kwa wakati huu.
  • ·         Wachukuzi wa umma wametakiwa kuhakikisha kuwa abiria wanaosha mikono yao kabla ya kuabiri magari hayo.
  • ·         Wakenya kuto toka nje ya nchi isipokuwa wale wenye umuhimu mkubwa wa kusafiri .Hakuna mtu atakayeruhusiwa kuelekea katika mataifa yenye visa vingi vya ugonjwa huo.
  • ·         Serikali imedokeza kwamba itatoa maelezo kuhusu ugonjwa huo kila siku,na kuwataka wakenya kutoeneza habari za uongo za viruzi vya Covid 19 Corona
  •  

Hapo wali serikali ya kenya ilitenga vyumba maalum vya kuwatibia wanaopatikana na virusi vya Corona katika hospitali ya Mbagathi.

Virusi va Corona hafibagui yeyote kwani kwa siku za hivi karibuni watu mashuhuri duniani wameambukizwa.

Wanasiasa ,wanamichezo na waigizaji maarufu ni miongoni mwa waadhirika.
Pia Waziri wa Afya wa Uingereza ,Nadine Dorries ameambukizwa Corona.
Mke wa Waziri Mkuu wa Canada Bi Sophie Tredeau anakisiwa kuambukizwa Virusi vya Corona.


Alhamisi, 12 Machi 2020

WHO Corona janga



Shirika la Afya Duniani, WHO limetangaza mkulupuko was virusi ya Corona kama janga la kimataifa.

Mkurugenzi wa WHO Dkt Tedros amesema viwango vya maambukizi vimeenea katika maeneo mengi nje ya nchi ya Uchina kwa mara 13.


Tangazo hili limetolewa huku nchi ya Italiano ikiwa na idadi kubwa ya maambukizi baada ya Uchina.


Dkt Tedros anasema kuwa "ana hofu kubwa " kutokana na "viwango vya maambukizi " ya virusi.


Hata hivyo, Dkt Tedros ameongeza kuwa kuuita ugonjwa janga haimaanishi kuwa WHO 


inabadilisha ushauri wake juu ya kile mataifa yanapaswa kufanya.

Ametowa wito kwa serikali kubadili jinsi zinavyo shughulikia mlipuko kwa kuchukua hatua za dharura. "Nchi kadhaa zimeonyesha kuwa virusi hivi vinaweza kudhibitiwa ,"amesema.

Virusi vya Corona vilidhihirika mwishoni mwa mwaka jana wa 2019 katika mji wa Wuhan mkoani Hubei mashariki mwa China; na hadi sasa  virusi hivyo vimeenea katika nchi zaidi ya 119 ikiwa ni pamoja na Marekani, Uingereza, Asutralia,Thailand, Korea ya Kusini, Japan, Canada, Ufaransa, Italia, Iran, Saudi Arabia na Imarati  licha ya  kuiathiri mikoa 30 ya China.   
Takwimu zinaonyesha kuwa hadi kufikia sasa watu wasiopungua 119,000 wameambukizwa virusi vya corona duniani.
 Watu 66,000 miongoni mwao wamepona na zaidi ya elfu nne wameaga dunia kwa maradhi hayo.