Alhamisi, 12 Machi 2020

WHO Corona janga



Shirika la Afya Duniani, WHO limetangaza mkulupuko was virusi ya Corona kama janga la kimataifa.

Mkurugenzi wa WHO Dkt Tedros amesema viwango vya maambukizi vimeenea katika maeneo mengi nje ya nchi ya Uchina kwa mara 13.


Tangazo hili limetolewa huku nchi ya Italiano ikiwa na idadi kubwa ya maambukizi baada ya Uchina.


Dkt Tedros anasema kuwa "ana hofu kubwa " kutokana na "viwango vya maambukizi " ya virusi.


Hata hivyo, Dkt Tedros ameongeza kuwa kuuita ugonjwa janga haimaanishi kuwa WHO 


inabadilisha ushauri wake juu ya kile mataifa yanapaswa kufanya.

Ametowa wito kwa serikali kubadili jinsi zinavyo shughulikia mlipuko kwa kuchukua hatua za dharura. "Nchi kadhaa zimeonyesha kuwa virusi hivi vinaweza kudhibitiwa ,"amesema.

Virusi vya Corona vilidhihirika mwishoni mwa mwaka jana wa 2019 katika mji wa Wuhan mkoani Hubei mashariki mwa China; na hadi sasa  virusi hivyo vimeenea katika nchi zaidi ya 119 ikiwa ni pamoja na Marekani, Uingereza, Asutralia,Thailand, Korea ya Kusini, Japan, Canada, Ufaransa, Italia, Iran, Saudi Arabia na Imarati  licha ya  kuiathiri mikoa 30 ya China.   
Takwimu zinaonyesha kuwa hadi kufikia sasa watu wasiopungua 119,000 wameambukizwa virusi vya corona duniani.
 Watu 66,000 miongoni mwao wamepona na zaidi ya elfu nne wameaga dunia kwa maradhi hayo. 








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni