Ijumaa, 27 Machi 2020

America COVID- 19


Marekani yaongoza duniani kwa idadi ya maambukizi ya virusi vya Corona
Chuo Kikuu cha Johns Hopkins kimetoa takwimu kuwa  watu 85,996 wameripotiwa kuambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani. 

Hivyo basi,  Marekani imekuwa nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu walioambukizwa virusi hivyo duniani.Huku idadi ya Vifo ikifika 1,195.

Idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo imeongezeka kwa zaidi ya watu elfu kumi ndani ya saa tano nchini Marekani,inasema ripoti hiyo.

 Pia Tafiti zinaonyesha  idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona imefika  542,788 na 24,361 wamefariki kwa virusi hivyo duniani.

Kwa sasa Marekani imeipita Uchina na Italia kwa visa vya Corona vilivyothibitishwa.
Hata hivyo,bado Italia inaongoza kwa vifo 8,000 huku Uchina ikifuata na idadi ya vifo 3,000 hadi sasa.

Ugonjwa wa Corona unaenea kwa kasi huku mataifa ya dunia yakijukakamua kukabiliana na hali kwa kuweka mikakati thabiti ya kukomesha maamukizi Zaidi.

Hiyo jana Kenya ilirekodi kifo cha kwanza cha mgonjwa aliyekuwa akipokea matibabu kwa muda.


Mkenya huyo wa miaka 66 alikuwa amezuru nchi ya uswatini Afrika kusini .



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni