Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2019

kongamano laicpd 25

Picha
Rais uhuru Kenyatta afungua rasmi Kongamano la idadi ya watu na maendeleo ICPD25 jiji Nairobi . Rais amehakikisha kuwa serikali ya Kenya itaweka mikakati ya kuhakikisha kuwa swala la ukeketaji wa wanawake limekabiliwa . Pia ametaka mataifa menginekuhakikisha haki za wanawake na jamii zinaheshimiwa. Upashaji tohara nchi na pia barani Afrika imekuwa ikiendelea licha ya hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika. Kulingana na tafiti wanawake waliopashwa tohara wanakuwa  hatarini wanapojifungua huku wengine wakifariki wakati wa kujifungua.

ICPD 25 NAIROBI

Picha
Kongamana kuu la kimataifa limengoa nanga   nchini Kenya huku maswala ya afya ya uzazi yakiorodheshwa kuwa kipaombele kati ya maswala nyeti yatakayo jadiliwa. Isistoshe,malengo makuu tano yanayolengwa katika mjadala wa siku tatu wa kongamano la (ICPD25) ni kama vile ; haki ya afya ya uzazi,dhuluma za kijinsia na tabia tofauti ambazo zinaadhiri wanawake. Hata hivyo kuna baadhi ya vikundi ambavyo vina tofautiana na mkutano huu, hususan kuhusu maswala   ya uaviaji mimba na ngono za jinsia sawa yaani ushoga na ushagaji. Mashirika ya kidini yalipinga kuwa endapo maswala haya yatapewa nafasi ya kwanza, hawatahudhuria,huku wakisisitiza kuwa yanapinzana na desturi na mwelekeo wa dini. Vingozi wa dini wanakashifu hatua ya mkutano huu kwa kusema kuwa uaviaji mimba ni kitendo ambacho ni dhambi na pia ushoga hauna nafasi katika dini . Kwa mfano kanisa katoliki duniani hawaruhusu matumizi ya aina yeyote ya uzazi mpango hospitali wanazomiliki na zsisitiza ni dhambi. ...

WHO -UHC (universal health Coverage)

Picha
Azimio la afya kwa wote Sekta ya afya duniani imepata mafanikio   mwafaka baada ya Viongozi wa ulimwengu kupitisha rasmi Azimio la Kisiasa la Umoja wa Mataifa kuhusu afya kwa wote   (UHC) ifikapo mwaka wa 2030. Kwenye kikao cha ngazi ya juu kuhusu afya kwa wote, katika Makao Makuu ya   Umoja wa Mataifa jijini New york, Marekani ,Viongozi walitoa hoja kuwa ni muhimu swala la afya kwa wote lishighulikiwe kwa haraka na wakaridhia lipitishwe rasmi na baraza kuu. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutumu kwenye kikao hicho alisema,ingawa afya ni haki ya kila mtu, bado nusu ya watu ulimwenguni   wanakosa haki yao ya msingi.   Dk. Tedros Adhanom Ghebreyesus, Mkurugenzi Mkuu wa WHO amesema kuwa hii ni hatua muhimu na ni jukumu ya mataifa husika kuhakikisha malengo haya yameafikiwa ifikapo mwaka wa 2030. Dk Ghebreyesus akisema Ulimwengu umebakisha miaka 11 kuyatekeleza majukumu haya mwafaka ya afya. Aliwapongeza viongozi kwa kuchu...

chanjo ya malaria

Jaribio la chanjo ya malaria Huku ugonjwa wa malaria ukiwa miongoni mwa magonjwa hatari duniani,mbinu za kuukabili ugonjwa huu zinaendelea kuguduliwa kila uchao. Hii leo,nchi ya  Kenya itakuwa miongoni mwa nchi tatu barani Afrika zinazozindua majaribio ya chanjo ya kwanza ulimwenguni dhidi ya malaria. Nchi zingine kuzindua na kushiriki   katika mpango huu ni Ghana na Malawi. Zaidi ya watoto 300,000 chini ya miaka miwili wanatarajiwa kupewa chanjo hiyo kila mwaka Katika nchi zote tatu. Chanjo hiyo inayofahamika kama RTS,S ina mchanganyiko wa dawa inayoisaidia mfumo wa kinga mwilini kukabiliana na mbu wanaosababisha malaria. Hapo awali majaribio madogo yalionyesha kuwa karibu watoto wanne kati ya 10 kati ya umri wa miaka mitano na 17, waliopata dozi zote nne za chanjo hiyo, walilindwa. Chanjo hii imekuwa ikifanyiwa utafiti kwa zaidi ya miaka 30. Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) linasema hii inaweza kubadilika mchezo, lakini inasema chanjo hiyo in...

Augmentin bandia

Picha
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya dhidi ya matumizi ya dawa bandia ijulikanayo kama   Augmentin,nchini Kenya na Uganda. Shirika hilo limetoa tahadhari wakati kukiwa na ongezeko la ununuzi wa dawa bila ushauri wa wataalam wa afya nchini Kenya.   WHO imewataka  wakenya wawe waangalifu dhidi ya dawa hiyo bandia ya (antibiotic) inayoamikika kuuziwa wagonjwa katika sehemu mbalimbali za nchi. Augmentin,ni dawa ambayo hutumika dhidi ya maambukizi ya vidudu mwilini na imeorodheshwa na WHO kama mojawapo ya dawa muhimi na inapatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa. Kwenye taarifa yake kwa umma, WHO imesema dawa bandia ina muonekano unaokaribiana sana na dawa halisi inayotengenezwa na kampuni ya madawa ya GlaxoSmithKline (GSK). Dawa hizo bandia zilibainika baada ya   utafiti wa kukagua ubora wa dawa za antibiotic zinazouzwa kwa wagonjwa. Baada ya vipimo kwenye maabara za kudhibiti ubora ilibainika kuwa baadhi ya dawa ya Augumentin hazikuwa na viungo muhimu...

breastfeeding week

Picha
Huku dunia ikiadhimisha wiki ya kimataifa ya kunyonyesha mtoto kuna changamoto kibao ambazo zinazokumba akina mama katika shughuli za kuhakikisha mtoto amenyonya. Itafahamika kuwa maziwa ya mama yana faida kwa kukua kwa mtoto ikwemo umarishaji wa akili katika maendeleo ya mtoto pia inalinda mtoto dhidi ya magojwa. Aidha,inalinda akina mama wanaonyonyesha dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi na matiti. Katika miji ilioendelea watoto hawanyonyeshwi kulingana na mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) linalosizitisha kuwa mtoto anastahili kunyonyeshwa  kutoka saa moja anapozaliwa hadi anapofikisha miezi sita.Watoto wa umri huu wanategemea maziwa ya mama pekee. Hali ni tofauti kwa kiwango cha juu katika maeneo ya mashambani,kwani akina mama wanaoishi maeneo hayo  wanajikakamua kuhakikisha watoto wangenyonyeshwa kikamilifu. Zaidi ya hayo, shirika la WHO linasema kuwa zaidi ya maisha ya watoto 800 000 walio na umri wa chini ya miaka 5 yanaweza k...

Dkt. Sobbie Mulindi aaga dunia

Picha
Dkt. Sobbie Mulindi Saratani imepokonya nchi ya Kenya Mtafiti wa Virusi Vya Ukimwi na mhadhiri mwandamizi katika idara ya magonjwa ya akili ya Chuo Kikuu cha Nairobi,Dkt Sobbie Mulindi. Hadi kifo chake hiyo jana,Dkt. Mulindi alikuwa mashuhuri katika janja ya afya. Ustadi na ukakamavu wake wa utafiti na elimu ya kupunguza maambukizi ya VVU/IKIMWI ulijulikana sio Kenya tu lakini Afrika na dunia yote kwa jumla.   Pia Mulindi alikuwa Naibu Mkurugenzi wa zamani wa Baraza la Udhibiti wa Ukimwi la Taifa (2008-2014) Dk Sobbie Z. A. Mulindi alianza masomo yake katika Chuo Kikuu cha Nairobi, na baadaya akawa mkufunzi kwenye chuo hiko. Zaidi ya hayo,alitumika katika hospitali kuu ya Kenyatta na katika Hospitali ya wagonjwa wa kiakili ya Mathari kufuatia uzoefu kwake katika nyanja ya wagonjwa na kiakili yaani maswala ya kisaikolojia. Amekuwa mhadhiri katika chuo cha Nairobi kwa zaidi ya miaka 30 Isitoshe,alishiriki katika kukuza Mikakati ya Kitaifa ya kuzuia VV...

Dolutegravir(DTG) dawa ya VVU

Picha
Shirika la Afya Duniani (WHO) limependekeza dawa ya Dolutegravir(DTG) katika mapambano yake dhidi ya virusi vya Ukimwi,licha ya dawa hiyo kushukiwa kuwa na madhara kwa akina mama waja wazito. Pendekezo hili limetolewa siku mmoja baadaya ya shirika hilo ,kuchapisha taarifa inayoonyesha   kuwa mapambano dhidi ya Virusi Vya Ukimwi bado yanaendelea. WHO inapendekeza    matumizi ya Dolutegravir(DTG) kama njia ya kwanza na ya pili ya matibabu  kwa watu wote,wakiwemo akina mama wajawazito na pia wenye uwezo wakupata ujauzito. Tafiti za awali, zilitia shaka    uwezekano wa kuwepo kwa uhusiano kati ya dawa ya DTG na tatizo linalosababisha watoto kuzaliwa na tundu kwenye uti wa mgongo na ubongo,yaani Spinal bifida. Tatizo hili hutokea punde tu mama anapopata ujauzito huku akitumia dawa ya DTG. Kenya ni miongoni mwa nchi ambazo zilitoa tahadhari dhidi ya matumizi ya dawa ya DTG baadaya ya utafiti uliofanywa nchini Botswana kuonyesha kuwa dawa h...

chanjo ya polio(polio vaccine)

Maisha ya watoto milioni ishirini yako hatarini kufuatia taarifa za umoja wa mataifa kuwa watoto hawakupata chanjo dhidi ya magonjwa yanayozuilika mwaka wa 2018. Magonjwa yanayozuilika ni kama vile,ugonjwa wa kupooza surua,Dondakoo na pepo punda. Takwimu hizi zimetolewa na   shirika la afya dudniani(WHO) kwa ushirikiano na Shirika la watoto duniani (UNICEF). Huku chanjo asilimia 86% ikitolewa kuokoa maisha ya watoto,bado kiwango kinachotakiwa cha asilimia 95% duniani kote hakijafikiwa. Tangazo hili la umoja wamataifa linatia hofu huku ikifahamika kuwa mlipuko Zaidi waweza kutokea endapo hali hii haita shughulikiwa ipasavyo. Shabaha ya kutoa chanjo ni kuimarisha afya ya watoto na kuepusha hatari ya milipuko ya wagonjwa yanayozuilika. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Bwana Tedros Adhanom Ghebreyesus amesisitiza kuwa huduma ya chanjo ni muhimu ili kuzuia milipuko ya magonjwa. Kiwango cha chanjo kwa watoto wasiopata chanjo hasa ni kutokana na hal...

Ebola Goma

Ebola Goma Shirika la Afya Duniani(WHO) litafanya kikao cha dharula hii leo kutathmini hatari ya Ebola nchini Congo. Mkutano huu unafanyika siku moja, baada ya kifo cha kasisi mmoja aliyefariki baada ya kusafiri Butembo kufanya maombi. Taarifa inasema mhubiri huyu alizuru eneo la Butembo ambalo ni baadhi ya maeneo yanayokabiliwa na ugonjwa wa Ebola kwa muda. Katika shughuli zake za maombi aliguza wagonjwa na huenda hapo ndipo alipoabukizwa maradhi hayo makali. Alirudi Goma huku anaumwa na punde alipoenda kutafuta matibabu kwenye zahanati ,akapatikana na ugonjwa wa Ebola. Moja kwa moja wataalamu wa afya wakachukua hatua kumsafirisha moja kwa moja hadi Butembo kupokea matibabu ya dharula, lakini kwa bahati mbaya akafariki. Goma ni mji ulio na idadi ya watu milioni moja ,kwenye pwani ya Ziwa Kivu, karibu na Rwanda.  Ni mara ya kwanza ugonjwa huu kuripotiwa Goma huku wasiwasi ukitanda katika nchi jirani ya Rwanda.Kuna shughuli nyingi hufanyika kila ...