Alhamisi, 27 Juni 2019

Trachoma


Trachoma (Vikope)

Trachoma au vikope ni ugonjwa unaosababisha upofu.isitoshe,maabukizi yake yanatokana na bakteria aina ya Klamidia Trakomati.

Ugonjwa huu unaweza kuthibitiwa ukitibiwa mapema.


Mazingira machafu na ukosefu wa maji safi huchangia maabukizi ya maradhi haya.

Nchini kenya jamii za wafungaji wa kuhamahama huadhrikika Zaidi.

Hata hivyo idadi ya magonjwa imepungua kwa asilimia 91 kote duniani

Kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO), idadi ya watu walio kwenye hatari ya maabuziki imepungua kutoka 1.5 billioni mwaka wa 2002 hadi 142 millioni mwaka  2019.

Tafiti zinaonyesha kuwa ,kati  ya nchi 44 ambazo ziko Afrika na Asia, zilikubwa na ugonjwa huu lakini umethibitiwa kwa kiwango cha juu kwa sasa.

WHO inasema kuwa, idadi ya waliohitaji upasuaji kurekebisha hali ya upofu ya trachoma imepungua kutoka millioni 7.6, mwaka  2002 hadi millioni 2.5 mwaka 2019.


Mbali na hayo,serikali ya Kenya imeweka mikakati ya kutokomeza tishio hili .

Mwaka wa 2015,Wizara ya Afya ilizidua mpango na miradi ili kuhakikisha Trachoma imekabiriwa mwaka 2019.


Mpango huu wa miaka mitano, ambao unatarajiwa kukamilika mwaka huu ulilenga kufanya upasuaji wa macho 40,000-katika maeneo yaliyo adhirika Zaidi. 

changamoto ya maambukizi


Kajiado,Samburu,isiolo,Laikipia,Baringo,Turkana,Meru Kaskazini ni baadhi ya maeneo 12 yaliotarajiwa kufaidika na mpango wa kukomesha Trachoma.

Watu Zaidi ya 2.9 millioni watapata matibabu, elimu ya afya ya umma kuhusu Trachoma,jinsi ya kujikinga, namna  yakudumisha usafi na mazingira masafi.

Hii ni hatua nzuri kwa serikali  kuhakikisha inatokomeza maambukizi mapya ya Trachoma kwa kuendelea kutoa dawa katika wilaya 12 zilizotajwa na kuwafanyia upasuaji wagonjwa ambao wamefikia hatua ya kupata upofu.

Serikali ya Kenya imekua ikishirikiana na serikali  Uingereza kupitia taasisi ya UK aid na Queen Elizabeth Diamond Jubilee Trust na shirika la Ugeremani la Christian Blind Mission katika kuhakikisha wagonjwa wa Vikope wanafikiwa na kupata huduma za matibabu pamoja na kufanyiwa upasuaji kwa wale ambao walio kwenye hatari ya  kupata upofu.


Majimbo ya Kajiado na Samburu yanaongoza kwa kiwango cha juu cha Trachoma.

Dalili
·         Macho kuwa mekundu.
·         Macho kutoa machozi kila wakati.
·         Maumivu na kuwasha macho.

Madhara

·         Kushindwa kustahimili mwanga na maumivu ya macho kwa watoto.

·         maamivu makali mgojwa anapopepesa macho kutokana na kuchomwa na vikope


·         kufifia uwezo wa kuona.

·         upofu kutokana na makovu kwenye kioo cha mbele ya jicho. 


·              Kinga

·         Kudumisha usafi wa mwili na mazingira ya makazi .


Matibabu
·         Matibabu ya mapema hupunguza vimelea vinavyoleta ugonjwa huu

·         Operesheni ndogo, kwa wagonjwa waliokwisha kupata vikope.







Ijumaa, 21 Juni 2019

ugonjwa wa kifafa


David Kamau ni mkaazi wa Mowlem viungani vya jiji la Nairobi.
Toka utotoni yeye anaishi na ugonjwa wa kifafa.Kwa muda mrefu,wazazi wake walitafuta tiba za kienyeji kwa waganga wa kienyeji bila mafanikio.

Walisema mtoto wao amefanyiwa uchawi ila hawakufahamu kuwa aliugua kifafa.
Mara kwa mara Kamau alipoteza fahamu na kuzimia,alianguka na akapoteza muda mwingi kutafuta tiba.Hakuendelea na masomo yake baaada ya kidato cha nne.

Kamau ni miongoni mwa watu robo tatu walio na ugonjwa wa kifafa katika nchi zenye kipato cha chini , na ambao hawapati matibabu wanayoyahitaji.

Hii inachangia kuwepo hatari ya kufa kabla ya wakati wao. Kulingana na  ripoti mpya ya shirika la afya duniani WHO baadhi ya wagonjwa wa kifafa hawapati matibabu inavyostahili.

Zaidi ya hayo wengine wanaogopa kwenda hospitalini kwa sababu ya unyanyapa,na pia Imani potovu zinazohuzishwa na ugonjwa huu.

WHO inasema endapo wagonjwa wangepata matibabu na kwa haraka hali yao ya kiafya ingekuwa bora.

WHO inasema pengo la ukosefu wa matibabu au huduma za afya karibu na waathiriwa linaweza kizibwa .Asili mia 70 wana kifafa.

Inasema kuwa hali si sawa katika mataifa yenye chumi ndogo ikilinganishwa na mataifa yaliyostawi kiuchumi.Vifo vya mapema ni Zaidi katika nchi zenye chumi ndogo.Watu wenye kifafa wanakunwa na magonjwa mengine ya kiakili na hii inashababisha kuzorota kwa hali ya mtu.

WHO inakadiria kuwa kuna wa millioni mia tano (500) wenye kifafa kote duniani.
Nchini kenya hali sio tofauti .Watu millioni moja wana kifafa huku wawili kati ya mia hawajapata tiba au hawafahamu kuwa wana hali hii.

Watu  millioni 2.4 hupatikana na kifafa duniani kote kila mwaka.
Vifo hutokea hasa wakati mtu anapozama maji,majeruhi ya kichwa au kuchomeka mtu anapopata mshtuko.

Jinsi ya kumsaidia mtu anapopata mshtuko wa kifafa.             
  • Unastahili kushikilia kichwa cha mgonjwa
  • Kichwa kinapaswa kugeuswa kwa upande
  • Usijaribu kufungua kinywa au kuweka kijiti au kijiko
  • Endapo shambulio litapita dakika tano,unapaswa kutafuta ambulensi kwa dharula.
  • Asipewe chakula wala maji
  • Shambulio hudumu dakika 2-3 kwa kawaida.
  • Usimuamushe hadi apate fahamu

Hali ikizidi tafuta usaidizi wa mtaalam wa afya.

Jumatatu, 17 Juni 2019

WHO in Uganda


Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus,azuru Uganda kutadhimini hali ilivyo kwa sasa,baada ya mripuko wa Ebola huko Kasese, Uganda.

Who 703x422
WHO photo
Dkt Ghebreyesus aliwasiri Uganda kutoka Congo ambapo alitembelea maeneo ya mkurupuko wa Ebola,huko Butembo na Katwa.
Kwenye taarifa, Mkurugenzi mkuu alitoa hakikisho kuwa shirika lake litajitahidi kuhakikisha kuwa ugonjwa wa Ebola umekabiliwa.

Alisema hali sio nzuri, hadi ugonjwa wa Ebola ukabiliwe Congo.

Hata hivyo alisema kuna mafanikio ya kupungua kwa maradhi hayo hasa Butembo na katwa.

Isitoshe, kwenye kikao katika nchi hizo mbili,alitilia mkaso kuwa endapo idadi ya maabukizi ya Ebola yamepungua, si vema kuweka Imani kuwa hali iko sawa.

Dr Tedros holds discussion with Prof Omaswa and WHO Representative in Uganda Dr Yonas Aliongeza kuwa ni muhimu kwa wadau wa afya na serikali kulichukualia kwa uzito tishio hili ili kuepuka milipuko Zaidi.

Alisema sehemu ya Mabalako ambapo ugonjwa huu ulipolipuka mara ya kwanza  mwaka wa 2018,imekuwa ni sehemu ambapo milipuko Zaidi imeripotiwa.

Hii pia ni sehemu watu waliopatikana na Ebola Uganda walitokea.

Nchi za Uganda na Kenya zimeweka tahadhari mipakani tangu kuzuka kwa ebola na kifo cha kijana mmoja aliyetokea huku Jamhuri ya Demokrasia ya Congo wiki moja iliyopita.
Photo PPU


Baadaye Dkt Ghebreyesus,akiadamana naWaziri wa Afya na maafisa wa afya alikutana na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Mseveni kuhusu tishio la Ebola Uganda.
Alipongeza Uganda kwa hatua walizochukua kufuatia mlipuko wa ebola hivi majuzi.





Alhamisi, 13 Juni 2019

world blood donor day 2019



Kesho (June 14, 2019) ni siku ya maadhimisho ya utoaji damu duniani.

Image result for done la damu
Siku hii  ambayo huadhimishwa kila mwaka,imelenga kuwashukuru watu wote wanaojitokeza kutoa damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya wagonjwa waliopungukiwa na damu na pia  walio kwenye  hatari ya kupoteza maisha kwa kukosa damu.
 Shirika la Afya duniani (WHO) na nchini wanachama wake zimelenga  kuwaelimisha watu   umuhimu wa kujitolea kutoa  damu mara kwa mara ili kuongeza paini za damu safi na salama kote duniani

Nchini Kenya kumekuwa na upungufu wa damu katika kituo cha Kitaifa cha kuhifadhi damu maana wakenya wengi hawapendi kutoa damu.

Mila,tamaduni na pia Imani za kidini zikichangia katika hali hii.

Serikali imekuwa katika harakati za kuwahamazisha wakenya umuhimu wa kutoa damu ilikuokoa maisha ya maelfu ya watu wanaokumbana na matatizo ya ukosefu wa damu ya kutosha mwilini.

Maadhimisho haya yatafanyika nchini Rwanda, maudhui yakiwa “damu salama kwa wote (safe blood for all).

Utoaji wa damu unasaidia kuokoa maisha ya mamilioni ya watu kila mwaka kwani wagonjwa wanaougua na kuhatarisha maisha huokolewa na damu ambayo iko katika hifadhi au benki ya damu.

Wagonjwa wa dharula, wanaofanyiwa upasuaji wakiwemo wamama wanaotoka kujifungua ni miongoni mwa wale wanaonufaika na damu iliotolewa na watu kwa hiari.

Nchi nyingi zinakumbana na tatizo la upungufu wa damu katika benki za damu na tatizo la kupata damu safi na salama .
Ni jambo la muhimu watu kuelimishwa na kutambua mafanikio yanayotokana na kuchanga damu safi na salama.

Hatua hii itasaidia watu wengine walioko hospitalini wanaoteseka na tatizo la upungufu wa damu mwilini.

Shirika la kuhifadhi damu nchini Kenya (KNBTS),) inasema kuwa Kenya haijafikia viwango vya paini za damu iliyowekewa  na  shirika la Afya Duniani,kwa nchi wanachama wake.

Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), nchi inapaswa kuwa na paini 400,000 za damu kila wakati.

Hata hivyo,kiwango hiki kinaweza kufikiwa iwapo asilimia moja ya watu wangetoa damu mara moja kwa mwaka
sababu ikiwa  watu wengi hawapendi  kutoa damu na pia watu kukosa kuelewa umuhimu wa kutoa damu.
 Kwa muda mrefu  KNBTS imekuwa ikihamasisha Wakenya kujitokeza kutoa damu kupitia mitandao ya kijamii vyombo vya habari na mabango.
ajari za barabarani, mashambulizi ya kigaidi na kuongezeka kwa magonjwa yanayohitaji damu Zaidi yamechangia upungufu wa damu katika hifadhi.
Utoaji wa damu Kenya uko chini sana huku idadi ya wanaohitaji damu ikiongezeka kila siku.
Itakuwa changamoto kwa wakenya nan a watu wote kujitolea kutoa damu ili kuokoa maisha ya marafiki,wapendwa wetu n ahata watu tusiowafahamu.


Ebola death Uganda



Kenya imechukua hatua za dharula kuthibiti ugonjwa wa ebola baada ya kijana mmoja kufariki huko Kasese ,Magharibi mwa Uganda . 

Wizara ya Afya imesema kuwa wataalamu wa afya wamepelekwa   kwenye  vituo vya mipaka yake kuthibitisha virusi vya Ebola.

Doria imewekwa  mipakani  hasa katika viingilio vyaa Busia ,Malaba na pia kwenye Viwanja vya ndege.

Image result for kenya boader surveillance ebola
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya Kenya, wageni  wanaoingia kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Uganda,Rwanda ,Burundi  na nchi nyingine wanafanyiwa uchunguzi na watalamu wa afya ,kabla kuruhusiwa kuingia nchini.
Watapimwa viwango vya joto mwilini.
Katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta, Chumba maalum cha uchunguzi kimetengwa ili kukabiliana na maradhi haya endapo yatagunduliwa .Pia kuna Sehemu maalum ya matibabu (Vituo vya udhibiti)katika hospitali kuu ya Kenyatta.

Uganda ilitangaza kesi mbili za Ebola baada ya kugunduliwa kwa kijana mwenye umri wa miaka mitano na virusi .

Duru sinasem Mvulana huyo, alisema kuwa alisafiri pamoja na mama yake kutoka DRC Jumapili, alifariki Jumanne usiku.

Image result for uganda ebolaZaidi ya wasafiri mia tatu 300 kutoka mataifa tofauti wamechunguzwa tangu serikali imarishe doria.

Kufuatia mlipuko wa Ebola shirika la Afya Duniani likishirikiana na Serikali ya Uganda na mataifa jira inachukua hatua za dharula kuhakikisha hali imethibitiwa.

WHO imesema wahudumu wa afya 4700 wamepewa chanjo ya kuzuia maambukizi na wamejiandaa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.


Dalili za ebola       
·         Homa

·         Kufuja damu

·         Hutabulika baada ya siku ishirini na moja 21
·         Joto jingi mwilini ya Zaidi ya kipimo  cha 38 degree Homa
·         Kichefuchefu na kutapika
·         Kuharisha
·         Vidonda vya koo
·         Kuumwa kichwa
·         Maumivu ya misuli
·         Kusumbuliwa na tumbo
·         Kuchoka
·         Kukosa hamu ya chakula
Kinga
·         Osha mikono na sabuni: Jiepusha na tabia ya kutoosha mikono
·         Jiepushe na hali ya kumkaribia/kumguza mtu aliyeabukizwa virusi vya Ebola
·         Epuka nyama ya pori
·         Epuka miili ya waliofariki kutakana na maabukizi ya Ebola

Mwanzoni mwa Mwezi huu,shirika hilo la afya ulimwenguni lilisema takriban watu 2,000 wameambukizwa ugonjwa huo nchini Congo.  


Jumatano, 12 Juni 2019

The WHO Academy Lyon hub



Image result for who LOGO
(WHO photo)
Shirika la afya duniani likishirikiana na serikali ya Ufarasa imeweka mkataba wa pamoja kushirikiana katika harakati zake za kuanzisha chuo cha mafunzo ya afya duniani huko Lyon,Ufaransa.

Makubaliano hayo yalifanywa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom Gebreyesus na  Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron huko Geneva,Uswizi.

Chuo hicho kinatarajiwa kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya na kiafya na wadau wake  duniani kote.

WHO Academy Lyon Hub kama kitakavyojulikana,kitakuwa ni chuo cha hali ya juu yenye mafunzo na teknologia ya kisasa.

Wabunifu watapata fursa kuonyesha ubunifu wao na kuchangia katika mundo mbinu ya afya,katika harakati za kuinua viwango na huduma za afya duniani.

Kulingana na Shirika la Afya Duniani(WHO)lengo la kufanya maazimiyo hayo na  nia ya kuanzisha chuo cha mafunzo ya afya ni kufanikisha shabaha ya WHO la kuhakikisha kuwa ifikiapo mwaka wa 2023 watu billioni moja watafaidika kutokana na huduma bora za afya kote duniani.

Mafunzo yatatolewa na wataalamu wa afya kulingana na kanuni na malengo ya shirika la afya duniani(WHO).

Viongozi,wasomi,watafiti ,wafanyi kazi wa WHO, watu wote duniani waliohitimu watapewa nafasi ya masomo katika chuo hiki.Ni sharti watoke nchi wanachama wa WHO.

Shirika la Afya Duniani(WHO) limekuwa kwenye mstali wa mbele kuhakikisha wato kote duniani wamepata huduma bora ya afya .