Jumatano, 29 Aprili 2020

Silas Njiru-Askofu


Bishp silas njiru | Malimwengu KEAskofu mstaafu Silas Njiru Afariki dunia
Virusi vya Corona vimepokonya kanisa katoliki na Kenya kwa jumla Askofu Mstaafu wa Jimbo la Meru,Silas Njiru .
Askofu Njiru alifariki mapema Jumanne nchini Italia baada ya kuambukizwa Covid-19.

Askofu wa Meru Salesius Mugambi ambaye alichukua hatamu za uongozi wa jimbo hilo baada ya kustaafu kwa marehemu, alisema Askofu huyo mstaafu alikuwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Rivoli ambapo alikuwa amelazwa kwa siku tatu.
Hapo awali Asofu wa jimbo la Embu kupitia ujumbe kwenye mtando, aliomba wakristo kumuombea Marehemu kwani alikuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi .
 Alikuwa miongoni mwa mapadre  watatu walioambukizwa virusi vya Corona kwenye makao yao.
Marehemu alikuwa akikaa katika nyumba ya Mtakatifu Joseph Allamano huko Alpignano, Turin, Italia tangu kustaafu kwake. Alizaliwa Mwezi 1928 katika kijiji cha Kevote, Kaunti ya Embu.
Alihudhumu katika jimbo la Meru kwa muda mrefu zaidi,pia amekuwa Padre kwa miaka zaidi  ya sitini.
Mola ailaze roho pema peopni.
  • Ugonjwa wa Corona na walio kwenye hatari
  • Watu wenye umri wa miaka sitini na zaidi
  • Walio na ugonjwa wa kisukari
  • Ugonjwa wa moyo baadhi ya maradhi mengine.

Pamoja tuangamishe Corona

Jumanne, 28 Aprili 2020

COVID 19 Kenya



idadi ya maambukizi yaongezeka kenya

Idadi ya watu wanaoambukizwa ugonjwa wa COVID 19 imefikia 374 baada ya watu wengi 11 kupatikana na maambukizi.

Kati ya visa 11 mpya, saba ni kutoka Jimbo la Nairobi na nne kutoka Mombasa. Walioambukizwa wakiwa kati umri wa  miaka mitatu na 70.

Hii ni kwa mujibu wa taarifa za  Wizara ya Afya ya Kenya .

 Kaimu Katibu Mkuu wa Afya Rashid Aman,amesema  idadi ya watu wote waliopona sasa wamefika 124 baada ya watu wengine 10 kuopona baada ya masaa ishirini na nne.

Kuna visa vipya katika maeneo manne Nairobi,  manne yalikuwa kutoka Kawangware, na mengine kutoka maeneo ya Eastleigh, Manji na Kaloleni.

Dkt Aman ametowa wito kwa maafisa wa polisi kuhakikisha harakati na mbinu  za kuigia ndani na nje ya kaunti hizi mbili zinazingatiwa  kuzuia kuenea kwa virusi hivyo ambavyo vimewaambukiza zaidi ya watu milioni 3 na kuwauwa watu 212,337 ulimwenguni.

Wizara ilifafanua zaidi kwamba baa zitabaki kufungwa . wamiliki wa mikahawa waliruhusiwa  kufungua .
Kesi 374 za Covid-19 nchini zimesambaa kati ya Homa Bay (1), Kajiado (3), Kakamega (1), Kiambu (5), Kilifi (9), Kitui (2), Kwale (1), Mandera (8), Mombasa (97), Nairobi (241), Nakuru (2), Siaya (2) na Uasin Gishu (1).

Wakati huo huo, waziri wa maswala  ya Ndani Fred Matiangi alisema Jumanne kwamba kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab zitawekwa kizuizini kuanzia kesho ili kudhibiti janga hilo.


Jumamosi, 25 Aprili 2020

Malaria 2020

Siku ya malaria yaadhimishwa huku maambukizi  ya janga la Corona yakiendelea kuongezeka.

Jumatano, 22 Aprili 2020



COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania

Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania.
Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi  wakati wa maombi ya taifa  jijini Dar es Salaam leo.

 Majaliwa alisema kufikia jana  wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu.

Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona.
Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa .
Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili.
Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi kwa taifa
Tanzania imeendelea kutangaza maambukizi Zaidi katika Afrika Mashariki baadaya Kenya.
Hapo awali,Rais wa Tanzania ,Pombe magufuli alitangaza siku tatu za maombi kufuatia mripuko wa Corona.
Hii leo viongozi 
wa madhehebu mbalimbali ya kidini walikongamana kwa maombi maalumu kwenye mapambano dhidi ya janga la Corona 
Viongozi hao hawakuachwa nyuma katika harakati za kujikinga na virusi.walifalia barakoa na kuketi umbali wa zaidi ya mita moja kama inavyopendekezwa na wataalam wa afya wa WHO duniani.
      Kenya yaripoti visa 7(saba) leo
Kenya imeripoti visa zaidi leo yaani watu 303 sasa wameambukizwa virusi vya COVId 19.
Kufuatia ongezeko hili, Waziri wa Afya ,Mutahi Kagwe amesitisha usafiri wa hewa na barabara kuingia na kutoka jimbo la mandera ambapo maambukizi yameendelea kuongezeka kwa kasi.
Anasema hatua hii imechukuliwa ilikuepuka maambukizi baina ya jamii .








COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania

Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania.
Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi  wakati wa maombi ya taifa  jijini Dar es Salaam leo.

 Majaliwa alisema kufikia jana  wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu.

Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona.
Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa .
Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili.
Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi kwa taifa
Tanzania imeendelea kutangaza maambukizi Zaidi katika Afrika Mashariki baadaya Kenya.
Hapo awali,Rais wa Tanzania ,Pombe magufuli alitangaza siku tatu za maombi kufuatia mripuko wa Corona.




Virusi vya COVID 19


chimbuko la Virusi vya Corona 


Shirika la Afya Duniani, WHO limesema kuwa hakuna ushahidi kuwa  wa virusi vya Corona vilitengenezewa kwenye maabara.
Hata hivyo Msemaji  wa shirika hilo, Fadela Chaib amesema  ushahidi  uliopo unadhihirisha  kuwa virusi vya corona vilitoka kwenye wanyama nchini China mwishoni mwa 2019.
 Akihutubia  mkutano wa waandishi habari mjini Geneva, alisema kuna uwezekano mkubwa vilitoka kwenye popo.Zaidi ya hayo,anasema haijabainika ni vipi virusi hivyo vilitoka kwenye popo na kuingia kwa binaadamu.
 Hapo awali, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kuwa serikali yake inajaribu kubaini kama virusi hivyo vilitengenezwa kwenye maabara katika mji wa Wuhan nchini China, ambako janga la virusi vya corona lilianzia Desemba mwaka uliopita.
Kumekuwa na maoni na misimamo tofauti kuhusu ni jinsi gani virusi vya Corona vilikotoka huku wengi wakijadili kuwa vilitoka kwa wanyama huku wengine wakisema vilisababishwa au vilitengenezwa kwenye maabara.
Kulingana na tafiti za wataalam wa afya huko China baada ya mripuko awamu ya kwanza,iligunduliwa kuwa  watu 27 kati ya wagonjwa 41 waliokuwa wamelazwa hospitali katika awamu ya kwanza ya mlipuko corona waliwahi kufika katika soko la samaki la Huanan
Hivyo basi matokeo ya tafiti inadokeza uwezekano wa Matokeo ya maambukizi yalianza kusambaa kutoka soko hilo.
Isitoshe, kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) maambukizi  yalitoka kwa wanyama kabla ya kumuingia binadamu.




Jumanne, 21 Aprili 2020

Corona Virusi jikinge



Upuka maambukizi ya Corona;fuata masharti au maagizo

Tangu mlipuko wa virusi vya Corona kutangangwa kimekuwa na mijadala na maoni tofauti dhidi ya kijikinga na virusi.

Wataalamu wa afya wako kwenye harakati za kutafuta kinga ya maradhi haya huku Shirika la Afya Duniani likionya dhidi ya Imani potuvu kuhusu tiba ya corona inayotolewa na baadhi ya  watu.

Baadhi ya dhana za kupotosha kuhusu tiba ya COVID -19

  • ·         Kunywa vileo
  • ·         Kunywa chai ya rangi
  • ·         Kuoga maji moto
  • ·         Kukaa kwenye jua
  • ·         Ulaji wa vitunguu saumi na timu
  • ·         Mbu inaambukiza virusi vya Corona 


  • Hizi ni dhana potofu ambazo hazina ukweli wowote.


Hivyo basi, ni muhumu kuhakikisha :
  • ·         Nawa mikono mara kwa mara au tumia kitakasa mikono
  • ·         Funika mdomo na pua unapopiga chafya
  • ·         Usikaribiane na watu wala usiwe kwenye mkusanyiko wa watu
  • ·         Usisalimu kwa mikono
  • ·         Vaa barakoa
  • ·         Kaa nyumbani

Ukiwa na dalili zifuatazo ni muhimu kupata ushauri wa daktari haraka …
Dalili
  • ·         Homa
  • ·         Kukohoa
  • ·         Ugumu wa kupumua
  • ·         Maumivu mwilini
  • ·         Kuumwa na kichwa



Askofu Getrude Rwakatare


MAMA GETRUDE RWAKATARE AFARIKI DUNIA

Kifo cha Askofu Rwakatare kimepokelewa na waliomfahamu kwa huzuni na majonzi.

Mawanawe Muta Rwakatare,alitoa taarifa ya kifo cha mamake.Anasema Askofu alikuwa na matatizo ya moyo na alifariki hospitalini ambapo alipelekwa baada ya kuugua ghafla.
Mchungaji Rwakatare akaribisha watanzania kuombea Taifa - Mwananchi
 Alikuwa ni mtumishi wa Mungu,Mbunge maalum na mwanabiashara mashuhuri nchini Tanzania
Askofu Daktari mama Rwakata alikuwa na maneno na sauti  nyororo ya kumtoa nyoka pangoni.

Mahubiri yake yalikuwa na warsia na alinena kwa ukakamavu wa mama shujaa.

Nakumbuka wakati mmoja nilipozuru Dar es salam ,marafiki wangu wakanikaribisha kutembelea kanisa la Mlima wa moto pale mikocheni B.

Nilipoketi na kusikiriza mafunzo/mahubiri yake mama Rwakatare nilijihisi kama nimezaliwa tena kiroho, tangu wakati huo nilipenda kusikiliza mahubiri yake  kwenye televisioni .

Alikuwa kwenye mstari wa mbele kwenye maswala ya usawa wa jinsia hasa maswala na kina mama na maendeleo.
Wakati mmoja alisimulia historia ya maisha yake kimasomo,ndoa na jinsi alijitahidi kupata mali kama mwanamke mwenye juhudhi pasipo kumtegemea mumewe.

Mchungaji Rwaktare alizaliwa Kilombelo ,huko morogoro, akasomea Korogwe na baadaye akaenda nchini Kenya kwa masomo ya Chuo kikuu katika Chuo Kikuu Cha Nairobi.

Alikuwa ni msomi aliyekuwa na hamu ya kuona kila mtanzania amepata elimu ya hali ya juu.

Hii ilipelekea yeye kuanzisha shule za St Mary ambapo watanzania wengi walio kwenye nyaja mbalimbali nchini wamepitia.

Aliwarai akina mama kutia bidi katika shughuli zao za kila siku kwani bila bidii ,hakina faida.

Alikashfu uvivu.chimbuko la umaskini alisema ni uvivu.Alisema ni muhimu watu waajibike,watumike ,wajiajiri hasa vijana na akina mama.

Fahari na heshima ya mwanaume alisema ni kazi

Aliwatia moyo walokata tamaa maishani kwa kuwalisha chakula cha kiroho na kwa kutoa  mawaidha .

Mola ailaze roho yake palipo watakatifu wake …Amina

Alhamisi, 16 Aprili 2020

COVID 19



Shirika la Afya Duniani, (WHO) limetangaza ongezeka ya maambukizi na vifo vya virusi vya Corona.

Takwimu zinaonyesha ongezeko ya maambukizi hadi milioni 2 kufikia sasa,huku vifo vikiwa elfu 131.

Marekani na mataifa ya Uropa yanaongoza katika vifo na maambukizi duniani.

WHO chief: Coronavirus is a virus with 'unique characteristics ...Marekani  vifo elfu 28,326 na maambukizi elfu 637.
Ikifuatiwa na Italiano na vifo 21,645,Uhispania nayo ni ya tatu na maafa ya kiwango cha 18,579.

Ufaransa inachukua nafasi ya nne  na vifo Zaidi ya elfu 17 huku Uingereza ikiwa ya tano na vifo elfu 12.

Tarifaa hii inatolewa siku moja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha mswada wa fedha kwa Shirika la Afya Duniani kwa kile alichokitaja kama kutoa taarifa za kupotosha kuhusu maambukizi ya Corona na pia kuelekeza juhudi zake nyingi Uchina katika shughuli za kukabiliana na ugonjwa wa Corona.

Hata hivyo, hatua ya Trump imeshutumiwa na viongozi wa mataifa mbalimbali duniani kwani haukuwa wakati mwafaka wa kuchukua hatua kama hiyo; hasa wakati dunia inapotafuta shuluhu ya dharula kukomesha maambukizi ya COVID 19.

Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom, amesema kuwa nimatumaini yake Marekani ataendelea kuwa mshirika wa karibu wa shirika hilo kama ambavyo amekuwa kwa muda mrefu.

Mataifa tajiri duniani  G20 yametangaza kuahirisha malipo ya madeni yake kwa mataifa yaliyo na mikopo kwa muda wa mwaka mmoja.

Kufikia sasa, mataifa mengi yameanza kurejerea katika hali ya kawaida huku baadhi ya mengine yakichukua tahadhari kuhakikisha hali imekabiliwa.

Nchi ya Denmark na Ugeremani masomo yamerejea huku mataifa ya utaliano na uhispania wakirejea kazi kwa baadhi ya kampuni.

Nchini Kenya hatua zimechukuliwa na serikali kuhakikisha kila mtu anajikinga ipasavyo ilikuepuka maambukizi.

Hatua kali zimewekwa kwa wale watakao kiuka maagizo ya serikali.

Pia usafiri wa sehemu za majimbo zimekatizwa na wanaoishi miji ilioko karibu na jiji la Nairobi wanapaswa kuwa nyumbani ifikapo saa moja kamili.

Idadi ya maambukizi Kenya imefika 225 huku vifo vikiwa kumi hadi sasa.

Jimbo la Nairobi linaongoza katika maambukizi ya watu 163,Mombasa ikifuata na watu 36 Kilifi ikiwa na watu kumi huku mandera ikiwa na watu sita.

Jumatano, 15 Aprili 2020

Ken Walibora amefariki


Ken Walibora ameaga dunia.

Ken Walibora (@KenWalibora) | TwitterMwandishi wa Riwaya ya Siku Njema na wanahabari mtajika Ken walibora amefariki .

Inadaiwa mwanahabari/mtangazaji alipatikana katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali kuu ya Kenyatta.

Marehemu aligongwa na gari katika barabara ya Ladhies na gari la usafiri wa umma siku ya Ijumaa.

Hakika Walibora alitukuza kiswahili....

Walibora amechangia katika maendeleo ya Lugha hasa ya Kiswahili kwa kuandika vitabu kama vile Siku Njema na Kidagaa kimemwozea,Ndoto Ya Amerika ,nasikia sauti ya mama,Ndoto ya Almasi ,Kufa Kusikana na vingine vya kimombo.
Zaidi ya hayo,Walibora alifanya kazi na kampuni ya Utangazaji ya Nation kama mhariri wa kitengo cha kiswahili.
Baadaye alisafiri hadi Marekani alipokuwa mhadhiri wa lugha ya afrika.

Kifo chake kimetokea baadaya waandishi wawili wa kampuni ya Nation kugongwa na gari katikati mwa jiji la Nairobi.

Mola amlaze pema peponi ustadh,malenga Walibora


Donald Trump asitisha WHO msaada


Trump's WHO cutoff sends officials, allies scrambling - POLITICO
Shirika la Afya Duniani, (WHO) limetangaza ongezeka ya maambukizi na vifo vya virusi vya Corona.

Takwimu zinaonyesha ongezeko ya maambukizi hadi milioni 2 kufikia sasa,huku vifo vikiwa elfu 131.

Marekani na mataifa ya Uropa yanaongoza katika vifo na maambukizi duniani.

Marekani imerekodi vifo elfu 28,326 na maambukizi elfu 637.
Ikifuatiwa na Italiano na vifo 21,645,Uhispania nayo ni ya tatu na maafa ya kiwango cha 18,579.

Ufaransa inachukua nafasi ya nne  na vifo Zaidi ya elfu 17 huku Uingereza ikiwa ya tano na vifo elfu 12.

Tarifaa hii inatolewa siku moja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha mswada wa fedha kwa Shirika la Afya Duniani kwa kile alichokitaja kama kutoa taarifa za kupotosha kuhusu maambukizi ya Corona na pia kuelekeza juhudi zake nyingi Uchina katika shughuli za kukabiliana na ugonjwa wa Corona.

World Health Organization raises global virus risk to maximum ...Hata hivyo, hatua ya Trump imeshutumiwa na viongozi wa mataifa mbalimbali duniani kwani haukuwa wakati mwafaka wa kuchukua hatua kama hiyo; hasa wakati dunia inapotafuta shuluhu ya dharula kukomesha maambukizi ya COVID 19.

Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom, amesema kuwa nimatumaini yake Marekani ataendelea kuwa mshirika wa karibu wa shirika hilo kama ambavyo amekuwa kwa muda mrefu.

Mataifa tajiri duniani  G20 yametangaza kuahirisha malipo ya madeni yake kwa mataifa yaliyo na mikopo kwa muda wa mwaka mmoja.

Kufikia sasa, mataifa mengi yameanza kurejerea katika hali ya kawaida huku baadhi ya mengine yakichukua tahadhari kuhakikisha hali imekabiliwa.

Nchi ya Denmark na Ugeremani masomo yamerejea huku mataifa ya utaliano na uhispania wakirejea kazi kwa baadhi ya kampuni.

Nchini Kenya hatua zimechukuliwa na serikali kuhakikisha kila mtu anajikinga ipasavyo ilikuepuka maambukizi.

Hatua kali zimewekwa kwa wale watakao kiuka maagizo ya serikali.

Pia usafiri wa sehemu za majimbo zimekatizwa na wanaoishi miji ilioko karibu na jiji la Nairobi wanapaswa kuwa nyumbani ifikapo saa moja kamili.

Idadi ya maambukizi Kenya imefika 225 huku vifo vikiwa kumi hadi sasa.

Jimbo la Nairobi linaongoza katika maambukizi ya watu 163,Mombasa ikifuata na watu 36 Kilifi ikiwa na watu kumi huku mandera ikiwa na watu sita.