Jumatano, 1 Aprili 2020

Askofu Ndingi Mwana Nzeki afariki



 Mwana Nzeki ni shujaa,hakika shujaa ametuaga.
Aliyekuwa Askofu mstaafu wa Katoliki  jimbo la Nairobi alikuwa shujaa hakika.
ALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki... - GAZETI LA TAIFA LEO ...Marehumu askofu alikuwa mstari wa mbele kutetea wanyonge kutoka dhuruma hasa za wanasiasa  .
Alipokuwa Askofu wa Jimbo  la Nakuru alishuhudia mauaji ya kikabila jambo ambalo lilimghadhabisha hadi akakemea serikali iliyoongozwa na Mwenda zake Rais Daniel T Moi.
Iwe ni siasa au uongozi mbaya wa kisiasa yeye hakusita kukosoa serikali na wahusika .
Hakuogopa chochote,aliamini anafanya kazi ya Mungu na alifanya kwa moyo wake wote.
Ilikuwa ni husuni na majonzi hiyo jana  baadha ya kutangazwa kwa kifo chake .Kiongozi wa kanisa Katoliki nchini Kadinali John Njue ,ndiye aliyetangazwa kifo chake.
Kulingana na taarifa ya kadinali Njue, lifariki jana asubuhi katika makao ya viongozi wastaafu wa kanisa Katoliki jijini Nairobi baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Rais Uhuru,alitoa rambirambi zake huku akimtaja Askofu huyo kama kiongozi shujaa wa kidini aliyejawa na upendo .
Makamu wa rais William Ruto,Kiongozi wa ODM ,Raila Odinga na viongozi wengine wa kisiasa walimtaja Marehemu Askofu kama mtetezi wa wanyonge aliyepigania haki zao.
Alizaliwa mwaka wa 1931, Mwala kaunti ya Machakos. Baada ya kukamilisha masomo ya shule ya msingi alijiunga na mafunzo ya upadre katika seminari ilioko eneo la Kiserian, kaunti ya Kajiado.
Mola ailaze roho yake palipo watakatifyu wake…Amina

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni