Jumatano, 22 Aprili 2020

Virusi vya COVID 19


chimbuko la Virusi vya Corona 


Shirika la Afya Duniani, WHO limesema kuwa hakuna ushahidi kuwa  wa virusi vya Corona vilitengenezewa kwenye maabara.
Hata hivyo Msemaji  wa shirika hilo, Fadela Chaib amesema  ushahidi  uliopo unadhihirisha  kuwa virusi vya corona vilitoka kwenye wanyama nchini China mwishoni mwa 2019.
 Akihutubia  mkutano wa waandishi habari mjini Geneva, alisema kuna uwezekano mkubwa vilitoka kwenye popo.Zaidi ya hayo,anasema haijabainika ni vipi virusi hivyo vilitoka kwenye popo na kuingia kwa binaadamu.
 Hapo awali, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kuwa serikali yake inajaribu kubaini kama virusi hivyo vilitengenezwa kwenye maabara katika mji wa Wuhan nchini China, ambako janga la virusi vya corona lilianzia Desemba mwaka uliopita.
Kumekuwa na maoni na misimamo tofauti kuhusu ni jinsi gani virusi vya Corona vilikotoka huku wengi wakijadili kuwa vilitoka kwa wanyama huku wengine wakisema vilisababishwa au vilitengenezwa kwenye maabara.
Kulingana na tafiti za wataalam wa afya huko China baada ya mripuko awamu ya kwanza,iligunduliwa kuwa  watu 27 kati ya wagonjwa 41 waliokuwa wamelazwa hospitali katika awamu ya kwanza ya mlipuko corona waliwahi kufika katika soko la samaki la Huanan
Hivyo basi matokeo ya tafiti inadokeza uwezekano wa Matokeo ya maambukizi yalianza kusambaa kutoka soko hilo.
Isitoshe, kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) maambukizi  yalitoka kwa wanyama kabla ya kumuingia binadamu.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni