Jumanne, 28 Aprili 2020

COVID 19 Kenya



idadi ya maambukizi yaongezeka kenya

Idadi ya watu wanaoambukizwa ugonjwa wa COVID 19 imefikia 374 baada ya watu wengi 11 kupatikana na maambukizi.

Kati ya visa 11 mpya, saba ni kutoka Jimbo la Nairobi na nne kutoka Mombasa. Walioambukizwa wakiwa kati umri wa  miaka mitatu na 70.

Hii ni kwa mujibu wa taarifa za  Wizara ya Afya ya Kenya .

 Kaimu Katibu Mkuu wa Afya Rashid Aman,amesema  idadi ya watu wote waliopona sasa wamefika 124 baada ya watu wengine 10 kuopona baada ya masaa ishirini na nne.

Kuna visa vipya katika maeneo manne Nairobi,  manne yalikuwa kutoka Kawangware, na mengine kutoka maeneo ya Eastleigh, Manji na Kaloleni.

Dkt Aman ametowa wito kwa maafisa wa polisi kuhakikisha harakati na mbinu  za kuigia ndani na nje ya kaunti hizi mbili zinazingatiwa  kuzuia kuenea kwa virusi hivyo ambavyo vimewaambukiza zaidi ya watu milioni 3 na kuwauwa watu 212,337 ulimwenguni.

Wizara ilifafanua zaidi kwamba baa zitabaki kufungwa . wamiliki wa mikahawa waliruhusiwa  kufungua .
Kesi 374 za Covid-19 nchini zimesambaa kati ya Homa Bay (1), Kajiado (3), Kakamega (1), Kiambu (5), Kilifi (9), Kitui (2), Kwale (1), Mandera (8), Mombasa (97), Nairobi (241), Nakuru (2), Siaya (2) na Uasin Gishu (1).

Wakati huo huo, waziri wa maswala  ya Ndani Fred Matiangi alisema Jumanne kwamba kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab zitawekwa kizuizini kuanzia kesho ili kudhibiti janga hilo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni