Jumatano, 22 Aprili 2020



COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania

Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania.
Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi  wakati wa maombi ya taifa  jijini Dar es Salaam leo.

 Majaliwa alisema kufikia jana  wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu.

Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona.
Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa .
Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili.
Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi kwa taifa
Tanzania imeendelea kutangaza maambukizi Zaidi katika Afrika Mashariki baadaya Kenya.
Hapo awali,Rais wa Tanzania ,Pombe magufuli alitangaza siku tatu za maombi kufuatia mripuko wa Corona.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni