Ijumaa, 18 Desemba 2020

Pierre Buyoya afariki

 Aliyekuwa Rais was Burundi Pierre Buyoya afariki ncini Ufaransa.

Kulingana n'a binamuye, kiongozi huyo aliyetawala Burundi kwa kiimla alifiki baada ya kuugua maradhi ya COVID-19..


chanjo ya Corona kwa wanafunzi

CHANJO DHIDI YA COVID -19


Tangu virusi vya Corona kutangazwa  kama janga la ulimwengu,sekta nyingi zimeadhirika hususan ile ya elimu.

 Watoto wanaostahili kuwa shuleni wamelazimika kusalia nyumbani huku serikali ikitafuka mbinu za kuhakikisha masomo yemerejelewa bila kuhatarisha Maisha ya Watoto.

 Nchini Kenya hatua mwafaka tayari zimeafikiwa kuhakikisha kuwa baadhi ya wanafunzi wamerejea shuleni huku wakihakikisha masharti ya kukabiliana  na Virusi ya Corona inapewa kipao mbele.

 Isistoshe,kuna haja  ya kuwachanja Watoto Pamoja na waalimu punde tu chanjo zitakapofika kwenye nchi mbalimbali duniani.

 Kulingana na taarifa za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF chanjo dhidi ya COVID- 19 itakuwa hatua muhimu ya kurejesha hali ya masomo katika mstari wa kwanza.

Bi. Henrietta Fore, Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF anasema huku ugonjwa wa COVID-19 ukifika kilele na kupelekea shule kufungwa ,sekta ya elimu uliadhirika pakubwa huku asilimia 90 ya Watoto kote duniani wakibaki nyuma kimasomo.

Hata hivyo anashauri kuwa serikali zichukua hatua  kutoa chanjo kwa Watoto na wanaowatunza hasa walimu,baada ya wahudumu wa afya walio msitari wa mbele na makundi mengine yaliyo hatarini zaidi ya kuambukizwa COVID-19.

Ingawa kuna wale wanaohofia kurejea masomo kutahatarisha Maisha ya Watoto, Bi. Fore anasema kutofanya hivyo kutachangia Watoto wengi kukataa au kutoendelea na masomo katika umri mdogo na pia kwa wazazi wao kutoendelea na shughuli za kutafuta riziki -za kila siku.

Ingawa maamuzi ya kutoa chanjo hizo yako mikononi mwa serikali, “athari za kuendelea kukosa au kutohudhuria masomo ni kubwa sana hususan kwa watu wasiojiweza,amesema Bi. Fore.

Haya yanajili huku nchi ya Kenya ikitarajia kupokea chanjo dhidi ya virusi vya Korona kuanzia mwezi wa Januari mwaka wa 2021.

Chanjo hiyo ya Oxford University-AstraZeneca itawalenga Wahudumu wa afya, maafisa wa polisi, wakongwe na walimu.


Wengine watakao pata chanja kwa awamu ya kwanza ni wale ambao kazi zao zinawasabisha kuwa miongni mwa umati na wenye maradhi sugu ,imesema Wizara ya afya .

Waziri wa Afya Mutahi Kagwe, amesema kwamba Kenya itapokea chanjo milioni 24 kabla ya kushirikiana na kamapuni za taifa la Uchina.

Kagwe amesema kwamba Astrazeneca ni za bei nafuu ikilinganishwa na Pfizer ambayo  inastahili kuhifadhiwa katika mazingira ya -70° c.

Serikali inasema kuwa  Wakenya watapokea dozi hizo milioni 24 bila malipo kwani zimefadhiliwa na Shirka la Kitaifa la Chanjo GAVI.

 

 


Nyangarama Afariki Dunia-COVID

 Gavana Wa Jimbo La Nyamira Aaga Dunia

Gavana wa Kauti ya Nyamira John Obiero Nyagarama afariki dunia.

Nyagarama amekuwa akipokea matibabu katika Nairobi hospital iliyoko jijini Nairobi,kwa takriban mwezi mmoja.

Inasemekana Gavana Nyagarama alikuwa anaugua ugonjwa wa COVID-19.

Kulinagana na familia yake,alikuwa na matatizo ya kupumua baada ya mapafu yake kushindwa kufanya kazi.

Hata hivyo, Nyangarama amekuwa na matatizo ya kiafya ila familia yake imesita kusema alichokuwa anaungua .

Zaidi ya hayo, alisifika kwa kufanya miradi ya maendeleo kwenye kauti ya Nyamira, na pia kuwahimiza wakaazi umuhimu wa kujizuia kuambukizwa virusi vya Corona.

Pia
, alikuwa mkulima Hodari has awa zao la chai.Alifanya kazi katika sekta ya kilimo hususan majani chai na kupanda ngazi kwa kasi hasi akawa  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chai nchini kwa muda mrefu.

Hapo awali alifunza katika shule mbalimabli baada ya kufuzu kama mwalimu katika Chuo Kikuu cha Nairobi.Hadi kifo chake alikuwa na umri wa miaka 74.

Mola ailaze roho yake mahali pema peponi.

 

 

Alhamisi, 18 Juni 2020

dawa ya dexamethasone -corona


Virusi vya Corona na dawa ya dexamethasone 



Ni avueni kwa  wagonjwa wa COVID 19 baada ya Shirika la Afya Duniani(WHO) kukaribisha matokeo yanayoonyesha kuwa dawa ya dexamethasone inaweza kutibu na kuokoa maisha ya wagonjwa mahututi wanaougua COVID 19 au Corona.
Koronaavaayirasii fi Qoricha: 'Dexamethasone' qoricha akkamiiti ...
Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani (WHO),Dkt.Tedros Ghebreyesus anasema  utafiti huu ulifanyiwa Uingereza ambapo ,wagonjwa wa Corona waliohitaji Oksijeni na kapewa dawa hii,mmoja kati ya watano alipona.Pia waliokuwa kwenye mashine ya kusaidi kupumua walipopewa dawa ya dexamethasome,mmoja kati ya watatu alipona.

Akizungumza na wanahabari mjini Gevena,Uswisi,Dkt.Ghebreyesus alisema dawa hii imekuwepo kwenye orodha ya WHO ya dawa muhimu tangu miaka ya sabini na inapatikana kwa bei nafuu katika mataifa mengi duniani.

Dexamethasome ni dawa ambayo imekuwa ikitumika tangu 1960.matumishi yake yakiwa ni pamoja na kupunguza uvimbe katika maradhi tofauti mwingine ikiwemo ugonjwa wa saratani.

Wataalamu wa afya wanasisitiza kuwa dawa hii itumiwe chini ya uangalizi mkubwa wa kimatibabu,kwani ina nguvu sana.Inatunika hasa kwa magonjwa mahututi na wanaopata matatizo ya mapavu na uvimbe katika sehemu ya mzunguko wa mapavu na moyo.

Isitoshe,dawa hii inaadhari zake:

  • Kukosa usingizi
  • Kuvuja kwa damu
  • Kutoona vizuri
  • Kuongezeka kwa uzito mwilini

Kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani(WHO) watu Zaidi ya 5,000 wamefariki kutokana na COVOD 19 kwenye bara la Afrika

Ugonjwa huu unawashabuliwa kwa hali ya juu waliona maradhi mengi tayari,kama vile kisukari,ugonjwa wa moyo na ugonjwa wa presha.


Kenya

Huku hayo yakijiri,Serikali ya kenya imetoa onyo dhidi ya matumuzi ya dexamethasone kwa
wakenya hasa kwa sababu ya madhara yake.
vya COVID 19 vimeongezeka hadi 184, ambavyo ni vya juu zaidi kuripotiwa nchini
hii leo. Vifo vya korona sasa vimefika 107 baada ya watu wawili kufariki.





Jumatatu, 15 Juni 2020

Covid-19 Ikulu Kenya


COVID 19 yabisha hodi Ikuu Kenya

Wafanyakazi wanne wa Ikulu ya rais nchini Kenya wamepatikana na virus vya corona hayo yemedhibitishwa na  msemaji wa Ikulu Kanze Dena.
Dena amesema kuwa wafanyakazi hao waligunduliwa kuaambukizwa COVID-19 baada ya kufanyiwa uchunguzi Alhamisi wiki iliyopita.
Wakanyikazi hayo wa ikulu wanaendelea kupokea matibabu katika Hospitali ya rufaa ya Chuo Kikuu cha Kenyatta.
Zaidi ya hayo,Bi Dena amewahakikishia Wakenya kuwa Rais Kenyata na familia yake wake wako salama salimini na wamepatikana kutokuwa  na maambukizi ya corona.
Hii ni ishara kuwa kila mtu yuko katika hatari ya kuambukizwa Corona endapo hatua zilizowekwa na Shirika la Agya Duniani na Wizara ya Afya hayatazingatiwa.
Kuvaa barakoa, kuosha mikono na maji yanayotiririka na kujiepunga/kujitenga na sehemu ambapo kuwa umati ni baadhi ya masharti ya kuzingatiwa.
Ikulu pia imehakikisha kuwa ili kuzuia maambukizi ya Corona kuenea , wafanyakazi wote wanaoishi nje ya Ikulu pamoja na wageni wamedhibitiwa huku masharti ya wizara ya afya yakiendela kutekelezwa.
Jana waziri wa Afya ,Mutahi kagwe alitangaza kuwa idada ya watu, walioambukizwa virusi vya corona imeongezeka hadi 3,727.
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe, amesema  pia kuna ,jumla ya 1286  waliopona katika kipindi cha saa 24.
Hata hivyo ,waziri amewataka wakenya kuendelea kufuata mikakati iliyowekwa na serikali ilikukabiliana na janga hili.


Jumatano, 10 Juni 2020

Rais Pierre Nkurunziza -kifo


Mke wa Rais wa Burundi aendelea kupata matibabu huku mumewe akiombolezwa

Huku warundi na watu watabaka mbalimbali wakiendelea kuomboleza kifo cha aliyekuwa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza,Mkewe angali anapokea matibabu nchini kenya kutokana na kile kinachotajwa kama maaambukizi ya virusi vya Corona.

Bi Denise Nkurunziza amekuwa Nairobi kwa wiki mbili sasa,akiwa amelazwa katika hospital ya Agah Khan na matatizo ya kupumua ,ingawa hospitali hiyo imekataa kutoa taarifa ya anapoumwa Bi Nkurunziza.

Burundi: Perezida Pierre Nkurunziza yaryamiye ukuboko kw'abagabo ...Kabla ya kuhamishiwa Kenya kwa matibabu,uvumi ulienea ndani na nje ya Nchi ya Burundi kuwa Mke wa Rais alikuwa kaambukizwa virusi vya Corona na alikuwa katika hali mahututi.
Kuligana na hali yake ya kiafya,Bi Nkurunziza alisafirishwa nchini Kenya na Ndege ya shirika la Afya la AMREF .

Mwenda zake Rais Nkurunziza anadaiwa kufariki baada ya msituko wa moyo huku uvumi uliokuwa ukienea nchini kuwa pia yeye alikuwa akiugua virusi vya Corona kukipigwa.

Taarifa ya serikali ya Burundi iliyotolewa kwa umma inadhibitisha kuwa amefariki kutokana na mshtuko wa moyo.
Rais Nkurunziza ametawala Burundi kwa miongo mitatu yaani miaka kumi na tano na amefariki siku chache baada ya uchanguzi wa nchi hiyo,ambapo Generali Evariste Ndayisimiye alitangazwa mshindi wa uchaguzi huyo.

Nkurunziza alitalajiwa kumkabidhi mamlaka Rais huyo mteuliwa mwezi wa nane ,mwaka huu.
Serikali ya Burundi imetanga maobolezi ya kitaifa huku bendera ya nchi hiyo ikipeperushwa nusu mlingoti.

Mola awape afueni wenye majonzi.

Presha au shinikisho la damu

Mshtuko wa moyo unatokea wakati damu inapiga kwa wingi na mishipa ikiwa miyembamba. Watu wengi hufariki ghafla baadha ya mstuko wa moyo. Wataalam wa afya wanasema kuwa hali hii inauwa watu wengi bila kuonyesha dalili huku wakisisitisha umuhimu wa kupimwa mara kwa mara.
Kipimo cha shinikizo la damu kawaida ni 100–140 mmHg kipimo cha juu na 60–90 mmHg kikiwa kipimo cha chini. Shinikizo la juu la damu hutokea kipimo kikiwa zaidi ya 140/90 mmHg kwa muda mrefu.
Ugonjwa huu isipogunduliwa mapewa unaweza kusababisha madhara ya kiafya.





Jumatatu, 18 Mei 2020


Shirika la Afyan duniani linafanya kikao hii leo mjini Geneva kujadili maswala ya COVID 19

Mkutano huu wa siku mbili unaendelea huku Taiwan ikipinga hatua ya kutengwa katika vikao vya baraza la shirika la afya duniani WHO huku ikisema itakuwa ni hasara kutohudhuria kikao hiki ikizingatiwa kuwa imefanikisha juhudi zake za kukabiliana na virusi vya Corona.

Taiwan na nchi nyingine kadhaa zimelitaka shirika hilo kuialika katika mkutano huo unaofanyika moja kwa moja kupitia mitandao.

Haya yanajili huku uhusiano baina ya Uchina na marekani ukiendelea kuzorota.

Hapo awali Marekani ambaye ni muhisani mkuu wa WHO ilitangaza kusimamisha  msaada wake wa kifedha huku nchi hiyo ikilaumu Shirika hilo kwa kushirikiana na kuipendelea Uchina katika harakati zake za kukabiliana na janga la COVID 19.

 Waziri wa Afya na Ustawi wa Taiwan, Chen Shih-Chung amenukuliwa akilaumu hatua ya kutoshirikishwa kwenye baraza la afya la umoja wamataifa.

Taiwan ni nchi ya visiwani katika Asia ya Mashariki upande wa kusini-mashariki wa China ina serikali yake tangu mwaka 1949 lakini Beijing inaiangalia kama sehemu ya nchi yake kufuatia historia ya nchi hizo.
Baadhi ya wanaohudhuria kikao hiki maalum ni marais wa mataifa mbalimbali ya dunia,wataalam wa afya na wageni wengine mashuhuri.

Mkuu wa shirika la Afya Duniani Tedro Adhanom anasema kuwa huu hiki ni kikao muhimu sana tangu  kuzinduliwa  1948.watu zaidi ya elfu 310,000 wamefariki kufuatia maambukizi ya Corona kote duniani huku millioni 4.7 wakiambukizwa hadi sasa.
Baadhi ya waliochangia katika mazungumzo ni Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaposa na waziri wa Afya Kenya ,Mutahi Kagwe .


Ijumaa, 1 Mei 2020

Antonio Guerres -Corona

Corona au COVID-19.

Huku siku ya uhuru wa vyombo vya habari ikiadhimishwa tarehe 3 Mei kote duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wanahabari na wafanyakazi katika vyombo vya habari wana majukumu muhimu katika kusaidia ulimwenguni kusambaza habari ipasavyo kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.

Alisema ni vema serikali kuwapatia nafasi na uhuru waandishi kutekeleza majukumu yao bila hofu,kuingiliwa au kutishiwa.

Siku ya uhuru was waandishi was habari huadhimishwa kila mwaka; maudhui ya mwaka huu ikiwa,uandishi wa habari bila uoga wala upendeleo,.
Tangu mlipuko was COVID 19 wanahabari wamejipata pambaya n'a selikali tofauti kufuatia j'insiste wanavyo ripoti maambukizi ya Corona. 

Hivi majuzi Tanzania ilistumu vikali habari kuwa kuna idadi kubwa ya maambukizi nchini humo. 

Serikali ya Kenya piano ili kashfu taarifa kuwa idadi ya maambukizi ni zaidi kuliko inavyotangazwa n'a selikali.

Wanahabari pia wanahitaji kulindwa wanapoenda kufanya mahojiano na wataalamu wa afya au wenye maambukizi.

Katika shughuli zao za kila siku wao hukabiliana n'a tishio baada ya nyingine n'a ni jukumu la selikali kuwapatia ulinzi hasa wakati huu was janga hili la Corona.

Fauka ya hayo,Bwana Guterres amesema katika vita dhidi ya virusi vya Corona, wanahabari wanaelimisha jamii jinsi ya kuepuka kuambukizwa Corona na kuwa hii italeta tofauti kubwa kupunguza maambukizi n'a kuokoa maisha .

Isitoshe,Guterres amekumbusha kuwa waandishi kuwezeshwa kufanya kazi zao kwa kupewa nafasi n'a mazingira bora.

Augustine Philip Mahiga

Aliyekuwa Waziri wa Sheria, Tanzania, Augustine Philip Mahiga afariki dunia ghafla huko Dodoma.
Rais Pombe Maghufuli ametangaza .

Jumatano, 29 Aprili 2020

Silas Njiru-Askofu


Bishp silas njiru | Malimwengu KEAskofu mstaafu Silas Njiru Afariki dunia
Virusi vya Corona vimepokonya kanisa katoliki na Kenya kwa jumla Askofu Mstaafu wa Jimbo la Meru,Silas Njiru .
Askofu Njiru alifariki mapema Jumanne nchini Italia baada ya kuambukizwa Covid-19.

Askofu wa Meru Salesius Mugambi ambaye alichukua hatamu za uongozi wa jimbo hilo baada ya kustaafu kwa marehemu, alisema Askofu huyo mstaafu alikuwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Rivoli ambapo alikuwa amelazwa kwa siku tatu.
Hapo awali Asofu wa jimbo la Embu kupitia ujumbe kwenye mtando, aliomba wakristo kumuombea Marehemu kwani alikuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi .
 Alikuwa miongoni mwa mapadre  watatu walioambukizwa virusi vya Corona kwenye makao yao.
Marehemu alikuwa akikaa katika nyumba ya Mtakatifu Joseph Allamano huko Alpignano, Turin, Italia tangu kustaafu kwake. Alizaliwa Mwezi 1928 katika kijiji cha Kevote, Kaunti ya Embu.
Alihudhumu katika jimbo la Meru kwa muda mrefu zaidi,pia amekuwa Padre kwa miaka zaidi  ya sitini.
Mola ailaze roho pema peopni.
  • Ugonjwa wa Corona na walio kwenye hatari
  • Watu wenye umri wa miaka sitini na zaidi
  • Walio na ugonjwa wa kisukari
  • Ugonjwa wa moyo baadhi ya maradhi mengine.

Pamoja tuangamishe Corona

Jumanne, 28 Aprili 2020

COVID 19 Kenya



idadi ya maambukizi yaongezeka kenya

Idadi ya watu wanaoambukizwa ugonjwa wa COVID 19 imefikia 374 baada ya watu wengi 11 kupatikana na maambukizi.

Kati ya visa 11 mpya, saba ni kutoka Jimbo la Nairobi na nne kutoka Mombasa. Walioambukizwa wakiwa kati umri wa  miaka mitatu na 70.

Hii ni kwa mujibu wa taarifa za  Wizara ya Afya ya Kenya .

 Kaimu Katibu Mkuu wa Afya Rashid Aman,amesema  idadi ya watu wote waliopona sasa wamefika 124 baada ya watu wengine 10 kuopona baada ya masaa ishirini na nne.

Kuna visa vipya katika maeneo manne Nairobi,  manne yalikuwa kutoka Kawangware, na mengine kutoka maeneo ya Eastleigh, Manji na Kaloleni.

Dkt Aman ametowa wito kwa maafisa wa polisi kuhakikisha harakati na mbinu  za kuigia ndani na nje ya kaunti hizi mbili zinazingatiwa  kuzuia kuenea kwa virusi hivyo ambavyo vimewaambukiza zaidi ya watu milioni 3 na kuwauwa watu 212,337 ulimwenguni.

Wizara ilifafanua zaidi kwamba baa zitabaki kufungwa . wamiliki wa mikahawa waliruhusiwa  kufungua .
Kesi 374 za Covid-19 nchini zimesambaa kati ya Homa Bay (1), Kajiado (3), Kakamega (1), Kiambu (5), Kilifi (9), Kitui (2), Kwale (1), Mandera (8), Mombasa (97), Nairobi (241), Nakuru (2), Siaya (2) na Uasin Gishu (1).

Wakati huo huo, waziri wa maswala  ya Ndani Fred Matiangi alisema Jumanne kwamba kambi za wakimbizi za Kakuma na Dadaab zitawekwa kizuizini kuanzia kesho ili kudhibiti janga hilo.


Jumamosi, 25 Aprili 2020

Malaria 2020

Siku ya malaria yaadhimishwa huku maambukizi  ya janga la Corona yakiendelea kuongezeka.

Jumatano, 22 Aprili 2020



COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania

Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania.
Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi  wakati wa maombi ya taifa  jijini Dar es Salaam leo.

 Majaliwa alisema kufikia jana  wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu.

Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona.
Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa .
Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili.
Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi kwa taifa
Tanzania imeendelea kutangaza maambukizi Zaidi katika Afrika Mashariki baadaya Kenya.
Hapo awali,Rais wa Tanzania ,Pombe magufuli alitangaza siku tatu za maombi kufuatia mripuko wa Corona.
Hii leo viongozi 
wa madhehebu mbalimbali ya kidini walikongamana kwa maombi maalumu kwenye mapambano dhidi ya janga la Corona 
Viongozi hao hawakuachwa nyuma katika harakati za kujikinga na virusi.walifalia barakoa na kuketi umbali wa zaidi ya mita moja kama inavyopendekezwa na wataalam wa afya wa WHO duniani.
      Kenya yaripoti visa 7(saba) leo
Kenya imeripoti visa zaidi leo yaani watu 303 sasa wameambukizwa virusi vya COVId 19.
Kufuatia ongezeko hili, Waziri wa Afya ,Mutahi Kagwe amesitisha usafiri wa hewa na barabara kuingia na kutoka jimbo la mandera ambapo maambukizi yameendelea kuongezeka kwa kasi.
Anasema hatua hii imechukuliwa ilikuepuka maambukizi baina ya jamii .








COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania

Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania.
Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi  wakati wa maombi ya taifa  jijini Dar es Salaam leo.

 Majaliwa alisema kufikia jana  wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu.

Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona.
Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa .
Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili.
Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi kwa taifa
Tanzania imeendelea kutangaza maambukizi Zaidi katika Afrika Mashariki baadaya Kenya.
Hapo awali,Rais wa Tanzania ,Pombe magufuli alitangaza siku tatu za maombi kufuatia mripuko wa Corona.




Virusi vya COVID 19


chimbuko la Virusi vya Corona 


Shirika la Afya Duniani, WHO limesema kuwa hakuna ushahidi kuwa  wa virusi vya Corona vilitengenezewa kwenye maabara.
Hata hivyo Msemaji  wa shirika hilo, Fadela Chaib amesema  ushahidi  uliopo unadhihirisha  kuwa virusi vya corona vilitoka kwenye wanyama nchini China mwishoni mwa 2019.
 Akihutubia  mkutano wa waandishi habari mjini Geneva, alisema kuna uwezekano mkubwa vilitoka kwenye popo.Zaidi ya hayo,anasema haijabainika ni vipi virusi hivyo vilitoka kwenye popo na kuingia kwa binaadamu.
 Hapo awali, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kuwa serikali yake inajaribu kubaini kama virusi hivyo vilitengenezwa kwenye maabara katika mji wa Wuhan nchini China, ambako janga la virusi vya corona lilianzia Desemba mwaka uliopita.
Kumekuwa na maoni na misimamo tofauti kuhusu ni jinsi gani virusi vya Corona vilikotoka huku wengi wakijadili kuwa vilitoka kwa wanyama huku wengine wakisema vilisababishwa au vilitengenezwa kwenye maabara.
Kulingana na tafiti za wataalam wa afya huko China baada ya mripuko awamu ya kwanza,iligunduliwa kuwa  watu 27 kati ya wagonjwa 41 waliokuwa wamelazwa hospitali katika awamu ya kwanza ya mlipuko corona waliwahi kufika katika soko la samaki la Huanan
Hivyo basi matokeo ya tafiti inadokeza uwezekano wa Matokeo ya maambukizi yalianza kusambaa kutoka soko hilo.
Isitoshe, kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) maambukizi  yalitoka kwa wanyama kabla ya kumuingia binadamu.