Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2020

Pierre Buyoya afariki

 Aliyekuwa Rais was Burundi Pierre Buyoya afariki ncini Ufaransa. Kulingana n'a binamuye, kiongozi huyo aliyetawala Burundi kwa kiimla alifiki baada ya kuugua maradhi ya COVID-19..

chanjo ya Corona kwa wanafunzi

Picha
CHANJO DHIDI YA COVID -19 Tangu virusi vya Corona kutangazwa  kama janga la ulimwengu,sekta nyingi zimeadhirika hususan ile ya elimu.  Watoto wanaostahili kuwa shuleni wamelazimika kusalia nyumbani huku serikali ikitafuka mbinu za kuhakikisha masomo yemerejelewa bila kuhatarisha Maisha ya Watoto.  Nchini Kenya hatua mwafaka tayari zimeafikiwa kuhakikisha kuwa baadhi ya wanafunzi wamerejea shuleni huku wakihakikisha masharti ya kukabiliana  na Virusi ya Corona inapewa kipao mbele.  Isistoshe,kuna haja  ya kuwachanja Watoto Pamoja na waalimu punde tu chanjo zitakapofika kwenye nchi mbalimbali duniani.  Kulingana na taarifa za  shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia  Watoto,  UNICEF  chanjo dhidi ya COVID- 19 itakuwa hatua muhimu ya kurejesha hali ya masomo katika mstari wa kwanza. Bi. Henrietta Fore,  Mkurugenzi Mtendaji wa  UNICEF anasema huku ugonjwa wa COVID-19 ukifika kilele na kupelekea shule kufungwa ,sekta...

Nyangarama Afariki Dunia-COVID

Picha
  Gavana Wa Jimbo La Nyamira Aaga Dunia Gavana wa Kauti ya Nyamira John Obiero Nyagarama afariki dunia. Nyagarama amekuwa akipokea matibabu katika Nairobi hospital iliyoko jijini Nairobi,kwa takriban mwezi mmoja. Inasemekana Gavana Nyagarama alikuwa anaugua ugonjwa wa COVID-19. Kulinagana na familia yake,alikuwa na matatizo ya kupumua baada ya mapafu yake kushindwa kufanya kazi. Hata hivyo, Nyangarama amekuwa na matatizo ya kiafya ila familia yake imesita kusema alichokuwa anaungua . Zaidi ya hayo, alisifika kwa kufanya miradi ya maendeleo kwenye kauti ya Nyamira, na pia kuwahimiza wakaazi umuhimu wa kujizuia kuambukizwa virusi vya Corona. Pia , alikuwa mkulima Hodari has awa zao la chai.Alifanya kazi katika sekta ya kilimo hususan majani chai na kupanda ngazi kwa kasi hasi akawa   Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chai nchini kwa muda mrefu. Hapo awali alifunza katika shule mbalimabli baada ya kufuzu kama mwalimu katika Chuo Kikuu cha Nairobi.Hadi kifo chake alikuw...

dawa ya dexamethasone -corona

Picha
Virusi vya Corona na dawa ya  dexamethasone   Ni avueni kwa  wagonjwa wa COVID 19 baada ya Shirika la Afya Duniani(WHO) kukaribisha matokeo yanayoonyesha kuwa dawa ya dexamethasone inaweza kutibu na kuokoa maisha ya wagonjwa mahututi wanaougua COVID 19 au Corona. Mkurugenzi mkuu wa shirika la Afya Duniani (WHO),Dkt.Tedros Ghebreyesus anasema    utafiti huu ulifanyiwa Uingereza ambapo ,wagonjwa wa Corona waliohitaji Oksijeni na kapewa dawa hii,mmoja kati ya watano alipona.Pia waliokuwa kwenye mashine ya kusaidi kupumua walipopewa dawa ya dexamethasome,mmoja kati ya watatu alipona. Akizungumza na wanahabari mjini Gevena,Uswisi,Dkt.Ghebreyesus alisema dawa hii imekuwepo kwenye orodha ya WHO ya dawa muhimu tangu miaka ya sabini na inapatikana kwa bei nafuu katika mataifa mengi duniani. Dexamethasome ni dawa ambayo imekuwa ikitumika tangu 1960.matumishi yake yakiwa ni pamoja na kupunguza uvimbe katika maradhi tofauti mwingine ikiwemo ugonjwa wa s...

Covid-19 Ikulu Kenya

COVID 19 yabisha hodi Ikuu Kenya W afanyakazi wanne wa Ikulu ya rais nchini Kenya wamepatikana na virus vya corona hayo yemedhibitishwa na  msemaji wa Ikulu Kanze Dena. Dena amesema kuwa wafanyakazi hao waligunduliwa kuaambukizwa COVID-19 baada ya kufanyiwa uchunguzi Alhamisi wiki iliyopita. Wakanyikazi hayo wa ikulu wanaendelea kupokea matibabu katika Hospitali ya rufaa ya Chuo Kikuu cha Kenyatta. Zaidi ya hayo,Bi Dena amewahakikishia Wakenya kuwa Rais Kenyata na familia yake wake wako salama salimini na wamepatikana kutokuwa   na maambukizi ya corona. Hii ni ishara kuwa kila mtu yuko katika hatari ya kuambukizwa Corona endapo hatua zilizowekwa na Shirika la Agya Duniani na Wizara ya Afya hayatazingatiwa. Kuvaa barakoa, kuosha mikono na maji yanayotiririka na kujiepunga/kujitenga na sehemu ambapo kuwa umati ni baadhi ya masharti ya kuzingatiwa. Ikulu pia imehakikisha kuwa ili kuzuia maambukizi ya Corona kuenea , wafanyakazi wote wanaoishi nje ya Ikulu pamoja...

Rais Pierre Nkurunziza -kifo

Picha
Mke wa Rais wa Burundi aendelea kupata matibabu huku mumewe akiombolezwa Huku warundi na watu watabaka mbalimbali wakiendelea kuomboleza kifo cha aliyekuwa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza,Mkewe angali anapokea matibabu nchini kenya kutokana na kile kinachotajwa kama maaambukizi ya virusi vya Corona. Bi Denise Nkurunziza amekuwa Nairobi kwa wiki mbili sasa,akiwa amelazwa katika hospital ya Agah Khan na matatizo ya kupumua ,ingawa hospitali hiyo imekataa kutoa taarifa ya anapoumwa Bi Nkurunziza. Kabla ya kuhamishiwa Kenya kwa matibabu,uvumi ulienea ndani na nje ya Nchi ya Burundi kuwa Mke wa Rais alikuwa kaambukizwa virusi vya Corona na alikuwa katika hali mahututi. Kuligana na hali yake ya kiafya,Bi Nkurunziza alisafirishwa nchini Kenya na Ndege ya shirika la Afya la AMREF . Mwenda zake Rais Nkurunziza anadaiwa kufariki baada ya msituko wa moyo huku uvumi uliokuwa ukienea nchini kuwa pia yeye alikuwa akiugua virusi vya Corona kukipigwa. Taarifa ya serikali ya Burundi iliyo...
Shirika la Afyan duniani linafanya kikao hii leo mjini Geneva kujadili maswala ya COVID 19 WHO assembly Mkutano huu wa siku mbili unaendelea huku Taiwan ikipinga hatua ya kutengwa katika vikao vya baraza la shirika la afya duniani WHO huku ikisema itakuwa ni hasara kutohudhuria kikao hiki ikizingatiwa kuwa imefanikisha juhudi zake za kukabiliana na virusi vya Corona. Taiwan na nchi nyingine kadhaa zimelitaka shirika hilo kuialika katika mkutano huo unaofanyika moja kwa moja kupitia mitandao. Haya yanajili huku uhusiano baina ya Uchina na marekani ukiendelea kuzorota. Hapo awali Marekani ambaye ni muhisani mkuu wa WHO ilitangaza kusimamisha  msaada wake wa kifedha huku nchi hiyo ikilaumu Shirika hilo kwa kushirikiana na kuipendelea Uchina katika harakati zake za kukabiliana na janga la COVID 19.  Waziri wa Afya na Ustawi wa Taiwan, Chen Shih-Chung amenukuliwa akilaumu hatua ya kutoshirikishwa kwenye baraza la afya la umoja wamataifa. Taiwan ...

Antonio Guerres -Corona

Corona au COVID-19. Huku siku ya uhuru wa vyombo vya habari ikiadhimishwa tarehe 3 Mei kote duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wanahabari na wafanyakazi katika vyombo vya habari wana majukumu muhimu katika kusaidia ulimwenguni kusambaza habari ipasavyo kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19. Alisema ni vema serikali kuwapatia nafasi na uhuru waandishi kutekeleza majukumu yao bila hofu,kuingiliwa au kutishiwa. Siku ya uhuru was waandishi was habari huadhimishwa kila mwaka; maudhui ya mwaka huu ikiwa,uandishi wa habari bila uoga wala upendeleo,. Tangu mlipuko was COVID 19 wanahabari wamejipata pambaya n'a selikali tofauti kufuatia j'insiste wanavyo ripoti maambukizi ya Corona.  Hivi majuzi Tanzania ilistumu vikali habari kuwa kuna idadi kubwa ya maambukizi nchini humo.  Serikali ya Kenya piano ili kashfu taarifa kuwa idadi ya maambukizi ni zaidi kuliko inavyotangazwa n'a selikali. Wanahabari pia wanahitaji kulindwa wanapoen...

Augustine Philip Mahiga

Picha
Aliyekuwa Waziri wa Sheria, Tanzania, Augustine Philip Mahiga afariki dunia ghafla huko Dodoma. Rais Pombe Maghufuli ametangaza .

Silas Njiru-Askofu

Picha
Askofu mstaafu Silas Njiru Afariki dunia Virusi vya Corona vimepokonya kanisa katoliki na Kenya kwa jumla Askofu Mstaafu wa Jimbo la Meru,Silas Njiru . Askofu Njiru alifariki mapema Jumanne nchini Italia baada ya kuambukizwa Covid-19. Askofu wa Meru Salesius Mugambi ambaye alichukua hatamu za uongozi wa jimbo hilo baada ya kustaafu kwa marehemu, alisema Askofu huyo mstaafu alikuwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Rivoli ambapo alikuwa amelazwa kwa siku tatu. Hapo awali Asofu wa jimbo la Embu kupitia ujumbe kwenye mtando, aliomba wakristo kumuombea Marehemu kwani alikuwa katika chumba cha wagonjwa mahututi .   Alikuwa miongoni mwa mapadre   watatu walioambukizwa virusi vya Corona kwenye makao yao. Marehemu alikuwa akikaa katika nyumba ya Mtakatifu Joseph Allamano huko Alpignano, Turin, Italia tangu kustaafu kwake. Alizaliwa Mwezi 1928 katika kijiji cha Kevote, Kaunti ya Embu. Alihudhumu katika jimbo la Meru kwa muda mrefu zaidi,pia amekuwa Padre kwa miaka...

COVID 19 Kenya

idadi ya maambukizi yaongezeka kenya Idadi ya watu wanaoambukizwa ugonjwa wa COVID 19 imefikia 374 baada ya watu wengi 11 kupatikana na maambukizi. Kati ya visa 11 mpya, saba ni kutoka Jimbo la Nairobi na nne kutoka Mombasa. Walioambukizwa wakiwa kati umri wa   miaka mitatu na 70. Hii ni kwa mujibu wa taarifa za   Wizara ya Afya ya Kenya .   Kaimu Katibu Mkuu wa Afya Rashid Aman,amesema   idadi ya watu wote waliopona sasa wamefika 124 baada ya watu wengine 10 kuopona baada ya masaa ishirini na nne. Kuna visa vipya katika maeneo manne Nairobi,   manne yalikuwa kutoka Kawangware, na mengine kutoka maeneo ya Eastleigh, Manji na Kaloleni. Dkt Aman ametowa wito kwa maafisa wa polisi kuhakikisha harakati na mbinu   za kuigia ndani na nje ya kaunti hizi mbili zinazingatiwa   kuzuia kuenea kwa virusi hivyo ambavyo vimewaambukiza zaidi ya watu milioni 3 na kuwauwa watu 212,337 ulimwenguni. Wizara ilifafanua zaidi kwamba baa zitab...

Malaria 2020

Siku ya malaria yaadhimishwa huku maambukizi  ya janga la Corona yakiendelea kuongezeka.
COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania. Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284. Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi   wakati wa maombi ya taifa   jijini Dar es Salaam leo.  Majaliwa alisema kufikia jana   wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu. Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona. Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa . Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili. Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi ...
COVID 19 Maambukizi yaongezeka Tanzania Idadi ya wagonjwa wa COVID 19 imekuwa ikiongezeka kwa kasi nchini Tanzania. Hii leo visa 30(thelathini) vimeripotiwa huku idadi ya maambukizi ikifika 284. Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa litoa taarifa ya maambukizi zaidi   wakati wa maombi ya taifa   jijini Dar es Salaam leo.  Majaliwa alisema kufikia jana   wagonjwa 256 wanaendelea vizuri huku saba wakiwa kwenye uangalizi maalumu. Idadi ya waliofariki ni 10 huku 11 wakipona. Waziri Mkuu ,Bw. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti ili kuhakikisha kuwa maambukizi ya virusi vya Corona vimedhibitiwa . Amesema serikali inatoa eimu kwa umma jinsi ya kujikinga,kamati ya kitaifa imeundwa ili kufuatilia hali ya ugonjwa nchini na pia timu ya wataalamu wa afya imeundwa ili kushughulikia swala hili. Bw.majaliwa amewataka watanzania kuchukua tahadhari kwa kufuata maagizo ya wataalamu wa afya na serikali ili kuepuka athari Zaidi ...

Virusi vya COVID 19

chimbuko la Virusi vya Corona  Shirika la Afya Duniani, WHO limesema kuwa hakuna ushahidi kuwa  wa virusi vya Corona vilitengenezewa kwenye maabara. Hata hivyo Msemaji  wa shirika hilo, Fadela Chaib amesema  ushahidi  uliopo unadhihirisha  kuwa virusi vya corona vilitoka kwenye wanyama nchini China mwishoni mwa 2019.  Akihutubia  mkutano wa waandishi habari mjini Geneva, alisema kuna uwezekano mkubwa vilitoka kwenye popo.Zaidi ya hayo,anasema haijabainika ni vipi virusi hivyo vilitoka kwenye popo na kuingia kwa binaadamu.  Hapo awali, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kuwa serikali yake inajaribu kubaini kama virusi hivyo vilitengenezwa kwenye maabara katika mji wa Wuhan nchini China, ambako janga la virusi vya corona lilianzia Desemba mwaka uliopita. Kumekuwa na maoni na misimamo tofauti kuhusu ni jinsi gani virusi vya Corona vilikotoka huku wengi wakijadili kuwa vilitoka kwa wanyama huku wengine wakisema vilisababishwa au...