Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2011

siku ya ukimwi duniani

Leo ni maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani

kongamano la uzazi mpango Dakar,Senegal

Picha
Kongamano kuhusu afya ya uzazi yaanza leo jijini Dakar nchini Senegal. Mkutano huu unafanyika huku karibu watu millioni 900 kote duniani wakikumbatia uzazi wa mpango. Hata hivyo, sio wote wanaoweza kufanya uzazi wa mpango wakati wanapotaka kufuatia changamoto kadha wa kadha. Mkutano huu utawajumuisha watafiti wa afya,madaktari na wadau wengine katika sekta ya afya. Kufanyika kwa mkutano huu katika Afrika Magharibi,ni jambo la muhimu ikifahamika kuwa nchi za Afrika Magharibi zinaongoza kwa idadi ya watu kwani mpango wa uzazi ungali haujapewa kipao mbele. Pia kupata hutuma ya uzazi wa mpango ni shinda. Inaaminika kuwa wazazi wengi ambao wangependa kupanga uzazi wanasubuka sana.Hata kabla wapate huduma hiyo muhimu wanagundua kuwa ni wajawazito.Idadi ya wanandoa walio kwenye hali hii ni zaidi ya millioni 215 kote duniani.   Uzazi wa mpango u nawezesha wanandoa kufanya maamuzi ya uzazi na ni moja ya njia ya gharama nafuu kwa ajili ya kuboresha afya ...

FGM (ukeketaji) Kenya

Ukeketaji Ni asubuni na mapema,jua linapoanza kuchomoza,katika kijiji kimoja katika Mkoa wa Mashariki. Kundi la akina mama linafululiza hadi kwa mama mwenzao, huku wakiimba nyimbo za kitamaduni. Kisa na maana ; hajakeketwa. Nia yao haswa ni kutumia nguvu kumkeketa kwani ni kero kwa wanawake wa kijiji chao. Kulingana na mila na desturi ya jamii hiyo ni sharti mwanamke akeketwe anapokaribia kuvunja ungo.Lakini kwa mama Matani* aliolewa kabla hajakeketwa. La kuhuzunisha ni kwamba yeye ni mjamzito na kitendo hiki kinaweza kuhatarisha maisha yake. Kwa bahati nzuri,anaepuka gadhabu ya akina mama hao baada ya chifu wa kijiji hicho kuingilia kati.Wanarudi makwao huku wakiapa kumuadhibu mama Matani* baadaye. Wakati wakujifungua ,yule mama hana budi kuwaita baadhi ya wale wanawake kumsaidia kujifungua. Sasa wanapata nafasi ya kumkeketa katika ile harakati ya kuzaa.Anajifungua mtoto na afya zake,anakeketwa na sasa ni mama kamili…..unyama ulioje?  Hii si hadithi bali ndivyo hali ilivyo katika ...

wakunga wa jadi na uzazi

Wakunga wa jadi na uzazi Katika kitongoji duni cha Korogocho,kundi la akina mama wajawazito wamepiga foleni wakisubiri kuhudumiwa. Baadhi yao wana uchungu ambao unadhihirika wazi unapowatazama. wana matumaini watapata afueni punde tu watakapomwona mama ambaye wanamuenzi. Mama huyu,Jacinta Akinyi, anajulikana kama daktari katika kijiji hiki.Hakika ni kuwa hana elimu yeyote katika taaluma ya udaktari. Yeye ni mkunga ambaye ana juhudi kama ya mchwa."Daktari" huamka asubuhi na mapema ili kuwahudumia akina mama ambao hawana uwezo wakutafuta matibabu au uchunguzi wanapokuwa katika hali ya ujauzito,katika hospitali za umma. Gharama ya kujifungua hapa nchini Kenya ni ghari mno,ikilinganishwa na ya wakunga.  Pia hali ya ukosefu wa usalama katika  mitaa duni ni changamoto kwa mama anayepata uchungu wa kujifungua wakati wa usiku. Mama Ona ni  baadhi ya akina mama wanaosubiri kujifungua. ingia kwenye chumba ambacho ndani kuna kitanda ambacho kimefichwa na pasia. mkunga akotayari k...

family planning(uzazi wa mpango)

Picha
Aina ya uzazi wa mpango Kuna   aina za uzazi wa mpango ambazo   mama au baba anaweza kutumia ili kuepuka kupata watoto wasiotarajiwa. Aina ya uzazi wa mpango Mpira au kondomu Kuna kondomu za akina baba na mama pia. mwanamume anapotumia kondomu inazuia mbegu zake kuingia kwenye mji wa uzazi wa mwanamke. -Ni rahisi kutumia -inakinga magonjwa ya zinaa na virusi vya HIV -Inazuia mwanamke kupata mimba isiotarajiwa Shindano(Depo Provera) Hii njia inafaa kwa mama ambaye hapendi kumeza vidonge na ambaye ameshazaa. Mwanamke hupata sindano hii ya homoni kila baada ya miezi mitatu. Hata hivyo mwanamke anapochagua kutumia aina hii ya uzazi wa mpango ni sharti aelewe kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo atakubana nayo kama vile;Kukosa hedhi au kupata hedhi kiasi kidogo. Pia kuna uwezekano wa kukawia kupata mtoto baada ya kuacha kutumia shindano kwa matarajio ya kutunga mimba. Vijiti Hivi ni vijiti vya plastiki vinavyowekwa chini ya ngozi ya mama.vinatolewa kila baada ya miaka mi...

population (idadi ya watu)

Huku idadi ya watu ikifikia billioni 7 duniani, kuna haja ya kuudwa kwa mikakati mwafaka, ili kukabiliana na changamoto zinazoabatana na ongezeko la watu.   Kulingana na takwimu zilizotolewa na umoja wa mataifa, idadi ya watu, inakadiriwa kuongezeka hadi billioni 9 ifikapo mwaka wa 2050. Barani Afrika hivi sasa idadi imefika billioni moja na inatarajiwa kuongezeka marudufu ifikapo 2050. Zaidi ya hayo, Bara la Afrika lina kibarua kigumu kutafuta shuluhu la haraka na la kudumu   ili kuhakikisha idadi ya   watu imedhibitiwa. Umaskini, uhaba wa vituo vya afya,upungufu wa madawa ni baadhi tu ya changamoto nyingi ambazo zimeendelea kuwa tishio. Ili kufikia malengo ya milenia ya afya sharti maswala ya elimu, matibabu(afya), usalama wa chakula na ajira yatiliwe maanani. Baadhi ya suluhu ni kuimarisha kampeni ya uzazi wa mpango.Hata hiyo kampeni hizo zisiwalenge pekee akina mama bali akina baba wahusishwe pia. Kwa muda mrefu mwanamke ndiye anayelengwa na uzazi wa mpango h...

shindano ya homoni ya depo provera

Uzazi wa mpango Ni ile hali ya mume na mkewe kukumbaliana jinzi au namna ya kupunguza mimba zisizotarajiwa. Serikali ya kenya imetilia mkazo umuhimu uzazi wa mpango.Zaidi ya hayo, kuna namna   na aina tofauti za uzazi wa mpango. Kuna vidonge vya kumeza, shindano ijulikanayo kama Depo provera, Vijiti, kitanzi, mpira wa mama au baba,kufunga kizazi kwa mama au baba na njia za asili. Ukweli ni kuwa, ni mpira pekee kati ya   aina zote za mpango wa uzazi inayozuia maambukizi ya ugonjwa. Aina zinginezo hazizui kupata magonjwa ya zinaa na pia virusi vya ukimwi. Bali na hayo, kuna dhana potofu kwa baadhi ya watu   wanaoamini kuwa matumishi ya auna hizi zote za uzazi wa mpango zinazuia maambukizi ya magonjwa ya zinaa na virusi ya ukimwi. Kulingana na utafiti uliofanywa na shirika moja la afya la Marekani na kuchapishwa na jarida la The Lancet, akina mama wanaotumia aina hii ya upangaji uzazi wako   hatarini ya kuambukizwa au kuwaambukiza waume wao virusi vya HIV,kuliko w...

saratani ya matiti

Saratani haina huruma Huku mwezi wa kumi ukiwa mwezi wa kupambana na ugonjwa wa saratani,ugonjwa huu unaendelea kuwa tishio kwa wengi.Kwa muda wa chini ya mwezi mmoja sasa,Kenya na pia   ulimwengu kwa ujumla imepoteza watu mashuhuri kutokana na Saratani. Mwenda zake Mama Wangari Maathai, ammbaye atakumbukwa kwa kulinda na kuhifadhi mazingira. Mwanzilishi wa kampuni ya Apple Steve Jobs ambaye aligobe katika nyanja ya technologia ya habari(alibuni mitandao) Mwingine ni Dkt Margaret Ogolla ,mtaalam wa afya ya watoto. Wa karibuni kufa saratani ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa ,Moijo Ole Keiwua aliyefariki siku moja tuu baada ya maziko ya Prof. Wangari Maathai. Saratani haichangui wala kubagua Kila mwezi wa Kumi, kampeni za   mapambano dhidi ya ugonjwa wa saratani inafanyika.Kila kituo cha afya na pia watalaamu wa afya wanakuwa kwenye mstari wa mbele kuendeleza elimu na matiba.Hospitali ya Aga Khan ina kitengo maalum   cha ugonjwa wa saratani.Pia uchunguzi wa saratani u...

Ovarian Cancer(saratani ya mfuko wa mayai)

Hii leo nitaandika zaidi na kuwaelimisha kuhusu saratani ya mfuko wa mayai yaani ovarian cancer. Je wajua kuhusu Saratani ya kifuko cha mayai ya uzazi ? Mwanamke ana vifuko viwili vidogo vilivyo kila upande wa   mfuko wake wa uzazi.Kwa mujibu wa tafiti,ni vigumu kuitambua saratani hii. Hivyo basi ni muhimu kutembelea daktari kila mwaka kwa uchukuzi wa kina.Dalili zake huonekana ugonjwa ukiwa umeenea mno. Walio   kwenye hatari ya kupata saratani hii ni v      -Wanawake wenye zaidi ya umri wa miaka 50 wako hatarini ya kuambikizwa ugonjwa huu. v      mwanamke tasa v      Ikiwa umewahi kuwa na saratani ya matiti v      Ikiwa kuna mtu wa familia ambaye amewahi kuugua ugonjwa huu. v      Kupata hedhi katika umri mdogo Hata hivyo, kama saratani yingine,inapogunduliwa mapema mtu anaweza kupona. Ni muhimu kula vyakula kama mboga, matunda ambavyo vinafahamika kupunguza hatari ya s...

wasifu wa Mama Wangari Maathai

Picha
Taarifa ya   kifo cha aliyekuwa mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel, Wangari Maathai, imepokelewa kwa huzuni. Watu wa tabaka mbalimbali wamenukuliwa wakitoa rambi rambi zao, huku wakimumiminia sifa chungu nzima . Ni wazi kuwa   kifo chake Maathai si pigo tu kwa wanaharaki wa mazingira nchini Kenya lakini kwa ulimwengu wote. Prof.Maathai akipanda mti Mama Mathaai aliaga dunia katika hospitali ya Nairobi   alikokuwa akitibiwa saratani ya mfuko wa uzazi(Ovarian Cancer) Umaarufu wa Mathaai ulitokana na ari yake ya Mazingira.Alikuwa kwenye mstari wa mbele kuelimisha wakenya na ulimwengu kwa ujumla umuhimu wa   kuhifadhi na kutunza mazingira. Pia alipigia debe jitihada za kutimiza lengo la milenia la kutunza na kulinda mazingira.  Karne tatu zilizopita, Maathai aliasisi shirika la mazingira nchini Kenya, Kenya Green Belt Movement. Alikuwa mama shujaa na pia   mkakamavu ambaye hakutishwa na yeyote.Alifanya kazi yake aliyoienzi kwa dhati. Wanyakuzi...

Prof.Wangari Mathaai

Picha
 Kifo cha shujaa wa Mazingira   Mama Wangari Maathai  Hongera Mama Mathaai kwa kazi yako nzuri ulioifanya.  Chemichemi za maji ukahakikisha zimelindwa. Shughuli ya ukataji miti misituni ukapigwa marufuku. Upanzi wa bangi Mlima Kenya ukakoma. Majereha ukapata kwa ajili ya mangizira. Katunukiwa Tuzo ya Nobeli kwa ukakamavu wako Hongera! Hongera! Mama Mathaai Mola akuweke pema peponi.

Polio(ugonjwa wa kupooza)

Serikali ya Kenya imezindua kampeini ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa upooza Septemba 23, 2011.Kampeni hiyo inalenga maeneo ambaye dalili ya ugonjwa huu imeanza onekana, kama vile Migori, Homa-Bay, Kisii, Nyamira na Transmara. .watoto walio chini ya miaka mitano watachanjwa. Hivi majuzi waziri wa Afya ya Umma, Beth Mugo alitangaza kuwa Kenya inakabiliwa na hatari   ya mkurupuko wa ugonjwa wa kupooza baada ya kijana mwenye umri wa miaka mitatu kupatikana virusi ya polio katika Wilaya ya Rongo, Mkoani Nyanza. Ugonjwa wa polio husababiswa na virusi na kwa hivyo ni vingumu kutibiwa, punde tu mtu anapoambukizwa. Mwongozo wa shirika la Afya duniani(WHO) unabainisha kuwa ili kudhibiti mzunguko wa virusi pori vya ugonjwa wa kupooza,ni muhimu kutoa chanjo za zaidi kwa njia ya kampeni kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 5 angalau kwa awamu mbili. Chanjo hii inatolewa na wataalam wa afya kwa njia ya matone kinywani kwa watoto wote, bila kujali kama walipata chanjo hiyo hapo awal...

saratani ya shingo ya uzazi (Cervical cancer)

Picha
  Ikiwa kuna ugonjwa ambao unasababisha vifo vya   wanawake wengi hapa nchi na duniani kwa ujumla, basi si mwingine ila ule wa saratani. Kuna aina kadhaa za saratani zinazo waathiri wanawake. Saratani ya shingo ya kizazi ni baadhi tu ya aina kadhaa za ugonjwa huu hatari. Mama Hannah Mwendeo* anafahamu vyema jinsi ugonjwa huu umekuwa tishio kwa wanawake wengi. "kabla madaktari kugundua maradhi niliyokuwa nikiugua, nilikuwa nina maumivu sana.Pia nilikuwa napata hedhi kila wakati,lakini si kufahamu kwamba nilikuwa tayari naugua saratani ya shingo ya uzazi. Kwa bahati nzuri.watalamu wa afya walitambua ni saratani ya shingo ya uzazi na papo hapo alianza matibabu". Kwa sasa amepona na anatowa wito kwa aki mama wenzake wajipimishe mapema ili kuepana na hatari au tishio la ugonjwa huu. Takwimu zilizotolewa na   shirika la afya duniani (WHO) , asilimia 3.2 ya wanawake nchini Kenya, walio kati ya miaka 18-69 hupimwa kila baada ya miaka mitatu ikilinganishwa na wanawake ...