Jumanne, 18 Desemba 2012

WHO Malaria Kenya


Kenya yatoa ripoti zisizo kamili

Serikali ya Kenya imepiga hatua kukabiliana na ugonjwa wa malaria,ingawa hatua zake hazijaridhisha Shirika la Afya Duniani.






Kulingana na ripoti iliyotolewa rasmi na Shirika la Afya Duniani(WHO),tathmini ya maendeleo ya Kenya kupambana na malaria haiwezi kufanywa kwa sababu takwimu zake si kamili kudhibitisha juhudi zake za kuukabili ugonjwa wa malaria.

WHO imetaja Kenya kuwa miongoni mwa nchi saba katika Mashariki na Kusini mwa Afrika ambazo viwango vya maambukizi vingali juu,huku huduma za afya zikiwa mbali na wananchi.


Zaidi ya hayo, serikali ya Kenya ilitoa ripoti kudhibitisha kutumia Dollar za Marekani 2,700,000 katika mipango yake ya kupambana na malaria katika mwaka 2010.Hata hivyo hakuna takwimu zinapatikana ama zilizotolewa katika kipindi za  2011.


Katika kipindi za 2010 Kenya ilipata Dollar za Marekani 39,100,000 kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa iliyofadhiliwa Kimataifa wa Kupambana na Ukimwi , Kifua Kikuu na Malaria(Global Fund).Ufadhili huo ulipunguzwa hadi Dollar za Marekani $ 12,200,000 mwaka 2011.



Rwanda,Zanzibar na Eritrea zimetajwa kama nchi ambazo zimepiga hatua  katika juhudi za kuukabili ugonjwa huu.Idadi ya wagonjwa waliolazwa hospitalini Rwanda pia ilipungua kwa asili mia 75 mwaka wa 2000-2011.Haya yakiwa mafanikio makubwa.

 

Shirika la Afya Duniani imesema kuwa  harakati za kudhibiti ugonjwa huo ilipata msukumo mkubwa katika kipindi cha mwaka 2004 na 2009, lakini mwamko huo ulishuka katika kipindi cha mwaka 2010 na 2012.Jambo ambalo si lakuridhisha.

Shirika la Afya duniani (WHO), imezinduliwa  rasmi ripoti  hii ya mwaka 2012 inayoaangazia tatizo la Malaria katika mji Mkuu wa Liberia, Monrovia ,huku Rais Ellen Johnson Sirleaf, akilalama kuwa ripoti hii imeonyesha kushuka kwa jitihada za kukabiliana na kasi ya ugonjwa huo.

Zaidi ya watu  660,000 wakiwemo watoto wa umri chini ya miaka mitano warifariki kutokana na ugonjwa wa malaria mwaka jana.














 Malaria

Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vinavyojulikana kama Plasmodium ambavyo huenezwa na mbu jike aina ya anopheles.
Dalili za malaria
  • Homa,maumivu ya kichwa
  • Maumivu ya mwili
  • Tumbo kuuma,kuharisha
  • Kichefuchefu,kutapika
  • Kupumua kwa shida
  • Kizunguzungu
  • Kutokwa jasho
  • Kutetemeka
  • Kifua kuuma
  • Kukosa hamu ya kula
  • Upungufu mkubwa wa damu mwilini

Jumamosi, 15 Desemba 2012

Mandela hospitali



 
Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, anaendelea kupokea matibabu hospitali mjini Pretoria ambako anatibiwa kwa ugonjwa wa mapafu.

Mzee Mandela alipelekwa na kulazwa hospitali, Jumamosi(wiki moja iliyopita).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Rais Jacob Zuma, aliyemtembelea, Mandela naendelea kupata nafuu.

Mapema mwaka huu, Mandela alilazwa hospitali ili kutibiwa matatizo ya tumbo yaliyokuwa yamemsumbua kwa muda mrefu.

Homa ya mapafu, husababishwa na viini tete vijulikanavyo kama (Streptococcus pneumoniae) na huathiri sehemu za kupumua kwenye mapafu.

Bwana Mandela amewahi kutibiwa kwa mara nyingine ugojwa wa kifua kikuu unaoathiri mapafu.

Magonjwa mengi ya mapafu hutibiwa kwa madawa , mgonjwa kupumzika au kupata vinywaji vingi.
  
Wazee na watu ambaom hawakinga ya mwili ndiyo huadhiriwa na maradhi haya.
Bwana Mandela ana miaka 94.

Jumatatu, 10 Desemba 2012

mkataba wa Kyoto


 

Hatimaye mkutano wa kujadili mabadiliko ya hali ya hewa mjini Doha umeafiki kurefushwa Mkataba wa Kyoto hata baada ya  nchi ya  Urusi kujaribu kuyapinga mafikiano hayo.


Wajumbe katika mkutano huyo, walijikaza kisabuni ili kupata suluhu katika hoja ambayo hakika ilikuwa ya dharula.


Maji taka
Mkutano huu uliwaleta pamoja wajumbe zaidi ya 17,000 kutoka nchi 200 duniani, uliafiki  kurefushwa Mkataba wa Kyoto unaodhibiti uzalishaji gesi za nyumba ya kioo hadi mwaka 2020.  

Isitoshe,nchi 27 za Umoja wa Ulaya, Australia na Uswisi na nchi nyingine nane zenye maendeleo ya viwanda zimekubali kushikamana na makubalino ya kuzuia uzalishaji wa gesi hizo hadi mwaka 2020.

Hata hivyo,Marekani imekataa kutia saini Mkataba wa Kyoto.

Pia  makubaliano hayo hayazihusishi nchi zinazochafua kwa kiasi kikubwa mazingira kama China na India.

Katika hotuba yake , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon,aliunga mkono hatua hiyo na kuzisitiza kuwa ni jukumu la, serikali kwa ushirikiano na wananchi, makundi ya kibiashara na jumuiya za kiraia, kuchukua hatua zaidi.  

Zaidi ya hayo, aliongeza kuwa, ili kuhakikisha dunia inakuwa salama kutokana na matumizi ya gesi chafu ni lazima nchi wanachama zikubaliane na mpango wa kuhakikisha zinapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya Carbon ili kunusuru tabaka la hewa.




 Mkutano huo ni wa 18 na  unafanyika kwa mara ya kwanza katika eneo la Ghuba ya Uajemi . Kwenye sherehe za ufunguzi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Maite Nkoana-Mashabane amekabidhi uongozi wa COP kwa Naibu Waziri Mkuu wa Qatar, Abdullah bin Hamad al-Attiyah.


Wajumbe kwenye mkutano huo walionyesha kudoridhika na kugawanyika kuhusu azimio la Kyoto la mwaka 1997 linalozitaka nchi tajiri kuzilipa fidia nchi masikini zinazoathirika na gesi za sumu zinazotoka katika viwanda vyao. Mkataba wa Kyoto ambao ulianza kufanya kazi mwaka 2005, haujawa na athari kubwa katika suala la kupunguza uchafuzi wa mazingira kwani nchi kubwa kama Marekani na China zimeshindwa kutekeleza azimio hilo.

Marekani ilikataa kusaini mkataba huo nayo China ikakataa kuutekeleza licha ya kuusaini. Canada kwa upande wake ilijiondoa kwenye mkataba wa Kyoto mwaka jana.
Mkataba wa Kyoto unazitaka nchi wanachama hasa zile zenye viwanda vingi kupunguza matumizi ya Carbon pamoja na kutoa fedha za kutosha kwa nchi zinazoendelea ili kuzipa uwezo wa kukabiliana na uharibifu wa tabaka la hewa.

Wataalamu wa masuala ya mazingira wanasema kuwa iwapo nchi za Marekani, Canada, China, Urusi na Uingereza hazitakubali kwa sasa kupunguza matumizi ya Carbon basi dunia hasa nchi zinazoendelea zinakabiliwa na hatari kubwa ya kukumbwa na hali joto ambayo ni hatari kwa mazingira na viumbe hai.

Mkataba huu ulitarajiwa kukamilika baadaye mwaka huu.


Jumanne, 4 Desemba 2012

pamoja tuangamize saratani



Ni muhimu kudumisha usafi kinywani.Kusungua meno baada ya kula ilikuepikana na magonjwa kama vile  Saratani ya mdomo.saratani hii husambaa kinywani kwenye ulimi na koromeo.Ugonjwa huu huchukua muda mrefu kabla kutambuli.Wanaovuta sigara,kuvuta tumbako au kunywa pombe wamo hatarini mwa kupata saratani ya mdomo.
Saratani ya mdomo ina inaweza kutibiwa unaweza kitibiwa ukiwahiwa mapema.
Ishara ya saratani yam domo ni kama zifuatazo; 
  • Uvimbe sehemu yoyote mdomoni, ambao hauponi kutokuwa na damu kwa urahisi.
  • Kufa ganzi mdomoni.
  • Kuhisi uchungu unapo tafuna, kumeza chakula ulimi unapotumika.
  • Kubadilika kwa sauti.
  • Kuumwa na sikio.
  • Koo linalowasha bila kupona.

pamoja tuangamize saratani



Ijumaa, 24 Agosti 2012

Martin Shikuku aaga dunia-Saratani


Ugonjwa wa saratani umetupokonya mwanasiasa mkongwe mzee Martin Shikuku.

Mzee Shikuku aliaga dunia katika hospitali ya Texas ambayo ni kituo cha  kipekee cha matibabu cha ugonjwa wa saratani.

Shikuku alikuwa akipata matibabu katika kituo hicho kwa miezi kadha.
Shujaa Shikuku alikuwa tayari alijizika akiwa hai kwa kujichimbia kaburi na kukamilisha kushughuli zingine ambazo zinaambatana na maziko.

Mbunge huyo wa zamani wa Butere alikuwa mstari wa mbele katika harakati ya kutaka mfumo wa vyama vingi na pia mtetezi wa haki za wanyonge.

Alijipata matatani na Uongozi wa rais mstaafu Daniel Moi alipoungana na viongozi wengine kuaada mkutano wa hadhara katika uwanja wa kamukunji, kutetea mvumo wa vyama vingi.

Alifungwa lakini hakukoma kumkosoa viongozi wafisadi na waliojipenda na kusahau kuwakilisha wananchi inavyostahili.

Kwake hayati Shikuku,siasa ilikuwa ni witu wala si kujinufaisha.Miezi miwili iliyopita Waziri Mkuu Raila Odinga alimtembelea hopitalini na kuahidi kuwa serikali ingemlipia gharama ya hospitali. 

Hakika Shikuku ulikuwa mzalendo.

Mungu alilaze roho ya hayati mahali pema peponi.

Jumapili, 29 Julai 2012

Waziri wa afya ya umma Beth Mugo apona kansa.ugonjwa wa kanza ume kuwa tishio hapa nchini Kenya na pia mataifa mengi ya Afrika.

hata hivyo kulingana na waziri beth Mugo ugonjwa huu unaweza kudhibitiwa na kupoona endapo utagunduliwa mapema.


Akizungumza jana baadha ya kuasiri kutoka Marekani ambako amekuewa akipokea matibabu ya kansa, waziri Mugo ametangaza kuwa kenya itafungua kituo cha Kansa nchini ilikuwatibu watu wanaougua ugonjwa huo.
Bi mugo aligunduliwa kuugua kanza ya matiti na kwa bahati nzuri iligunduliwa kabla haijaenea na kwa sasa anasema ako salama salimini.

Pia waziri mugo alionya wakenya kuhakikisha kuwa wanaishi kwenye mazingira safi, kwani uhalibifu wa mazingira hunachangia kuenea kwa ugonjwa hatari wa kansa.

"Hewa safi, mazingira mema na lishe bora ni muhimu kwa kuepa maradhi ya kansa.
Ni jukumu letu kama wakenya kudumisha usafi na pia upanzi wa miti ili kupata hewa safi.Hii itakuwa ni njia moja ya kuepuka maradhi hatari ya kansa.

Hivi majuzi rais Mwai kibaki aliidhinisha mswada wa kansa nchini,hii inapika hatua kupwa ya kukabiliana na ugonjwa huu.

matibabu ya kasa hapa nchini yamekuwa wa changamoto kadha wa kadha; kama vile ukosefu wa vifaa vya ukaguzi wa saratani, kampeni ya kuwafahamisha wananchi madhara na dalili za saratani,ghalama ya juu ya kutibu ugonjwa huu baadhi ya matatizo mengine.

Sadifa ni kuwa waziri wa afya ya umma na mwenzake wa humuda za afya Anyang Nyongo wamekuwa wakiugua saratani lakini wote wamepona, baada ya kupokea matibabu marekani.

Baadhi ya saratani ambayo inaadhiri wa kenya wa kike ni;saratani ya sehemu ya uzazi na ile ya matiti, huku wanaume wakiugua saratani ya koo na ya prostate.

Endapo serikali itachukua jukumu ya kutafuta yamna ya kukomesha kuenea kwa saratani hapa nchini ,itakuwa afueni kwa wananchi ambao gharama ya matibabu imekuwa ni ghali mno hadi wanaamua kutotafuta matibabu.


Baadhi ya wanakenya mashuhuri wanaugua saratani ni aliyekuwa mbunge wa Butere bwana martin shikuku.Tunamuombea afueni ya haraka,


Jumatano, 18 Julai 2012

Tohara-Ujeremani


Utata kuhusu tohara ya wanaume imetatuliwa baada ya Kansela wa Ujerumani kuunga mkono jamii za Kiyaudi na za Kiislaamu zinazo taka kitendo cha kutahiriwa kiendelee katika jamii zao.


Mseamji wa Kansela Angela Merkel, Steffen Seibert alisema " kutailiwa kwa watoto wa kiume ni kitendo ambacho kinakwenda sambamba na imani ya dini hizo na hakuna adhabu itakayo tolewa.

"Na ieleweke serikali inaruhusu haki ya kiimani na Wayahudi na Waislaam ni Wajeruamani hivyo wanahaki sawa na Wajerumani wangine."

Kuungwa mkuno huko kwa kitendo cha kutailiwa kumekuja baaada ya daktari mmoja kutokutwa na hatia ya kusababisha maumivu kwa mtoto aliye mtairi, ambapo ilidaiwa mtoto huyo alikutwa na matatizo ya kiafya kutokana kutailiwa huko.

Hata hivyo kitendo cha kutailiwa kimekuwa kinaleta mvutano katika jamii nchi Ujerumani huku wengine wakipinga na wengine wakiunga mkono.

Tohara ya mwanaume ni ile hali ya ukataji wa ngozi ya mbele inayoficha kichwa cha uume.Kulingana na wataalamu wa afya mwanamke ambaye mumewe ametailiwa ana uwezekano mdogo wa kuambukizwa Virusi Vya Ukimwi.Tohara ufanywa kwa sababu mbalimbali;za kidini kitamaduni,kiafya na kwa sababu za kudumisha usafi.

 


kongamano la afya ya uzazi London


Katika juhudi zake za kuboresha sera za uzazi , jumuia ya kimataifa  imeada mkutano wa kujadili uzazi wa mpango nchini  Ungereza.

Mkutano huu wa kimataifa utajadili Uzazi wa Mpango kwa nchi maskini zaidi duniani.

Baadhi ya viongozi wa Afrika walioalikwa kwenye  mkutano huu ni pamoja na ; Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete , Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Mwenyeji wa mkutano huu ni Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameroun.

Mkutano ,huu wa siku moja umedhaminiwa na Serikali ya Uingereza, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) na Taasisi ya Bill and Belinda Gates Foundation.

Ni mara ya kwanza mkutano wa aina hii unafanyika nchini Uingereza ,na utafanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Queen Elizabeth.

Inakisiwa  utaanzisha Mchakato wa Dunia ambao utalenga kuwawezesha wanawake wapatao milioni 120 katika nchi masikini zaidi duniani kupata habari, huduma na mahitaji ya kupanga uzazi bora zaidi na kuokoa maisha yao ifikapo mwaka 2020.

Isitoshe, mkutano huo ni nafasi ya pamoja ya kuiwezesha jumuia ya kimataifa kuonyesha dhamira zaidi katika huduma za uzazi bora ambazo kwa kiasi fulani zitachangia kuongeza kasi katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia nambari nne  kupunguza vifo vya watoto  na nambari tano kuboresha afya za akinamama.

Inakadiriwa kuwa zitahitaji kiasi cha dola za Marekani bilioni 10 kwa miaka minane ijayo kuanzia sasa 2012 hadi 2020 ili kudumisha huduma za sasa za uzazi bora duniani. Kiasi cha dola bilioni nne za ziada zitahitaji ili kuweza kuwafikisha wanawake milioni 120 katika nchi masikini zaidi ambao kwa sasa hawapati huduma hizo katika miaka hiyo minane ijayo.

Alhamisi, 5 Julai 2012

Arafat

Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat watoa majibu nusu.


marehemu Arafat wakati akiwa mwenye afya nzuri

marehemu Arafat baada ya kuugua
 
 Uchunguzi wa kisayansi uliyofanywa kuhusu kifo cha aliyekuwa kiongozi na rais wa Wapalestina umetoa majibu nusu tangu kuanza kwa uchunguzi huo.
Rais Yasir Arafat ambaye alifariki dunia nchini Ufaransa ambapo alipelekwa kwa ajili yamatibabu baada ya kuugua wakati akiwa amefungiwa  kutoka katika mji wa Ramallah na serikali Izrael.
 
Dr Francois Bochud ambaye ni mtaalamu wa Radiophysique iliyopo nchini Switzerland alisema " naweza kusema tumekuta aina ya gesi inayo julikana kama polonium-210 ambayo inaweza kuwa chanzo ca kifo chake na tunaweza kupata jibu sahihi ikiwa baadhi ya viungo vya marehemu Yasir Arafat vitapatikana kwa  uchunguzi zaidi."
 
Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat ulikuja baada ya mkewe Suha Arafat  kuruhusu uchunguzi kuendelea na kutoa ruhusa ya kuwa mwili wa Yasir Araf ufukuliwe kwa uchunguzi zaidi  na kuiomba serikali ya Wapalestina kushirikiana naye.

Wasifu wa arafat
Alikuwa kiongozi shupavu wa Palestina  aliyeenziwa na wale alioongoza.

Alhamisi, 29 Machi 2012

Kifua kikuu (TB)





Hatua za Kenya

Kenya imepiga  hatua madhubuti  katika juhudi zake za kukabiliana na ugonjwa wa kifua kikuu.

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani, Kenya imeorodheswa 15 kwenye orodha ya nchi 22 ambazo ugonjwa wa kifua kikuu ungali ni tishio.

Zaidi ya hayo, Shirika la Afya Duniani linaarifu kuwa juhudi za pamoja zimesaidia kupunguza vifo kwa asilimia 40 tangu mwaka 1990.

 Watu milioni 46 wameponywa kuanzia mwaka 1995 kutokana na juhudi za Umoja wa Mataifa, serikali mbalimbali, wafadhili, makundi ya kijamii, washirika binafsi, wataalamu wa afya, na makumi ya maelfu ya watumishi wa idara za afya pamoja na familia na jumuiya zilizoathirika

Umaskini na Virusi vya ukimwi unachangia pakubwa  katika maambukizi ya  kifua kikuu katika nchi zinazoendelea.

Kwa kawaida, wagonjwa ambao wanapatikana na magonjwa ya kuambukiza mara kwa mara hutengwa kuzuia kueneza ugonjwa.Hii hufanyika katika wodi maalum katika hospitali za serikali.

Mkurugenzi wa maradhi ya kifua kikuu katika Wizara ya Afya ,Kenya Dkt. Joseph sitienei anasema orodha hii ni wazi kuwa Kenya imepiga hatua ya haraka ya kuhakikisha kuwa ugonjwa wa kifua kikuu umedhibitiwa.

Mwaka jana wagonjwa wawili wa kifua kikuu walitiwa baloni kwa madai kuwa walikata kumeza tembe zao kama walivyo agizwa na watalaamu wa afya.

Ingawa hatua ya selikali ilikemewa na wadau wa haki za binadamu, serikali ilichukua hatua kali dhidi ya wawili hao, kwa lengo la kuokoa maisha yao.

Kutozingatia maagizo ya daktari au kukosa tiba ya ugonjwa huu, ni hatari kwa maisha ya mwenye maradhi haya.

Mwishoni mwa mwaka 2009 Kenya ilikuwa na wagonjwa 110,065 wa TB.

Mwaka 2009, Kenya ilikuwa na matukio 500 ya TB sugu kwa madawa mengi ijulikanayo kama MDR-TB, idadi ambayo imeshuka hadi 334 mwaka huu.

Ni wagonjwa 117 tu waliotumia tiba.Idadi hii imepungua hadi 101 kote nchini.

Kulingana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki – Moon, Mnamo mwaka 2010 pekee, takriban watu milioni tisa waliambukizwa  maradhi ya kifua kikuu, ambapo watu 1.4 miongoni mwao walifariki, huku asilimia 95 ya vifo vikitokea katika nchi zinazoendelea.


Moon ametoa wito kuwepo kwa mshikamano wa kimataifa utakaohakikisha watu wote wakohuru dhidi ya hofu kuambukizwa kifua kikuu.alisema kuna haja ya kukomesha upuuzaji na kutilia maanani juhudi za kupunguza vifo zaidi.

 MDR-TB ni sugu kwa madawa mengi ya mstari wa kwanza. Hata hivyo, inaweza kutibiwa kwa kutumia tiba ya muda mrefu yenye gharama kubwa ya madawa ya mstari wa pili, ambayo yana madhara zaidi.

Kumtibu mgonjwa mmoja kuhitaji madawa yenye thamani ya zaidi ya dola 16,250.


Kifua kikuu ni ugonjwa ambukizi nambari mbili kwa mauaji ulimwenguni.


 
kifua kikuu



Kifua Kikuu (TB) ni ugonjwa ambao kwa kawaida huathiri mapafu. Kifua Kikuu wakati mwingine huathiri sehemu nyengine za mwili, kama vile ubongo, figo, au uti wa mgongo. Ugonjwa wa Kifua Kikuu unaweza kusababisha kifo usipotibiwa.

Viini vya Kifua Kikuu husambazwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kupitia hewa. Viini vya Kifua Kikuu huwekwa hewani wakati mtu aliye na ugonjwa wa Kifua Kikuu anakohoa, kupiga chafya, kucheka, au kuimba. 

Jumatatu, 27 Februari 2012

Mzee Nelson Mandela apata matibabu

Aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini mzee Nelson Mandela aendelea kupata nafuu baada ya kutoka hospitalini , alikolazwa kutokana na maumivu ya tumbo ambaye yamekuwa yakimtatiza kwa muda mrefu.

Hapo awali, taarifa kutoka ofisi ya Rais Jacob Zuma ilisema Mzee Nelson Mandela alilazwa hospitalini na akawaomba  Waafrika Kusini kumuombea nafuu ya haraka.

Mzee Mandela, mwenye umri wa miaka 93 hajaonekana hadharani kwa muda mrefu sasa kufuatia kudorora kwa afya yake .

Wananchi wengi nchini Afrika Kusini walipokea habari za kulazwa kwake hospitalini kwa hofu na huzuni tele, lakini wakasema wanaendelea kumuombea apate afueni ya haraka.

Mbali na hayo,mzee Mandela aligunduliwa  kuugua saratani ya tezi dume,2001 na baada ya matibabu akapona, kwani iligunduliwa mapema.

Alikuwa Rais wa kwanza mweusi katika nchi hiyo kuanzia mwaka 1994 na kisha akaachia ngazi mwaka 1999.

Mandela anatambulika kote duniani kwa juhudi zake za kupambana na utawala wa kibaguzi wa Makaburu kwa muda mrefu na baadaye kuikomboa Afrika Kusini kutoka mikononi mwa wabaguzi hao wa rangi katika muongo wa tisini.


Pia sisi hapa nchini Kenya tunashukuru Mola kwa kumlinda mzee Mandela na pia tunamuombea ampate afueni.

Alhamisi, 23 Februari 2012

Njenga Karume aaga dunia

Former Kenyan Defense Minister NJenga Karume Dies Of Cancer: Sources
Marehemu Njenga Karume
Aliyekuwa waziri wa ulinzi na mbunge wa zamani wa Kiambaa, Njenga karume amefariki dunia.

Karume ameaga dunia katika hospitali ya Karen hapa Nairobi ,alipokuwa akipokea matibabu, baada ya kuugua saratani. Marehemu Karume amefariki akiwa na umri wa miaka 83.

Rais Mwai Kibaki ametoa salamu zake za rambi rambi kwa jamaa na marafiki wa Marehemu huku akisema amempoteza rafiki wa dhati.

Karume alikuwa kigogo wa siasa na alimuunga mkono rais Mwai Kibaki katika juhudi zake za kuimarisha siasa za chama cha Democratic party(DP).

Karume alikuwa mwanabiashara mashuhuri ambaye alikuwa na bidii kama za mchwa.Alijizatiti kuwa mmojawa  matajiri watajika hapa nchini,licha ya kuanzia chini sana.

Katika kitabu chake, alichoandika kuhusu maisha yake, Karume alisema vile alijitahidi kutoka uchomaji wa makaa hadi dhahabu.
Anatajwa pia kama aliyepigania uhuru, aliyehakikisha tamaduni zinahifadhiwa.

Alikuwa mbunge wa kiamba lakini 2007 alipoteza kiti chake, aliposhindwa na mbunge wa sasa mheshimiwa Stanley Githunguri.

Alikuwa pia mwanzilishi wa kundi la Gikuyu Embu Meru Association(GEMA) na mstahiki mzee wa jamii ya Gikuyu.

Wiki mbili kabla ya kifo chake uvumi ulienezwa kuwa Karume alikuwa amefariki.Kufuatia uvumi huo Rais Kibaki alimtembelea nyumbani kwake huku Cianda, Kiamba katika jimbo la Kiambu.

Mungu ailaze roho yake Karume pema peponi.