WHO Malaria Kenya
Kenya yatoa ripoti zisizo kamili Serikali ya Kenya imepiga hatua kukabiliana na ugonjwa wa malaria,ingawa hatua zake hazijaridhisha Shirika la Afya Duniani. Kulingana na ripoti iliyotolewa rasmi na Shirika la Afya Duniani(WHO),tathmini ya maendeleo ya Kenya kupambana na malaria haiwezi kufanywa kwa sababu takwimu zake si kamili kudhibitisha juhudi zake za kuukabili ugonjwa wa malaria. WHO imetaja Kenya kuwa miongoni mwa nchi saba katika Mashariki na Kusini mwa Afrika ambazo viwango vya maambukizi vingali juu,huku huduma za afya zikiwa mbali na wananchi. Zaidi ya hayo, serikali ya Kenya ilitoa ripoti kudhibitisha kutumia Dollar za Marekani 2,700,000 katika mipango yake ya kupambana na malaria katika mwaka 2010.Hata hivyo hakuna takwimu zinapatikana ama zilizotolewa katika kipindi za 2011. Katika kipindi za 2010 Kenya ilipata Dollar za Marekani 39,100,000 kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa iliyofadhiliwa Kimataifa wa Kupambana na Ukimwi , K...